Msaada kuhusu elimu na Vyeo Jeshini

Msaada kuhusu elimu na Vyeo Jeshini

Hapana mkuu haendi kwa sababu ya pesa anaenda kwa sababu anapenda jeshi ila tu anahitaji kujua kuhusu course zake na hilo la mshahara ni kama swali la nyongeza tu ila yeye jeshi analipenda

Halafu sijaelewa hapo uliposema marekani hadi mageneral wanaenda operation yaani inakuwaje? Na je hawa wa tanzania hawaendi?
Yeah US magenaral wanaenda operation na wanapigana kama wanajeshi wengine. Kuna general mmoja jina limenitoka ila alishakuwa waziri wa ulinzi nchini marekani.
 
Habari zenu wakuu.

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu, nina mdogo wangu wa kike anahitaji kwenda jeshini ili aje kuwa mwanajeshi officer yaani mwenye nyota, na elimu yake ni bachelor degree.

Kwa anayefahamu, ninaomba kujua jeshini inahitajika elimu gani ili mtu aweze kuwa officer yaani kuwa na nyota? Pia ningependa kujua na mishahara ya kila cheo kama ikiwezekana.

Na je, course za officers huwa zinachukua muda gani kuhitimu hadi apewe hicho cheo? Yaani kuanzia JKT hadi TMA jumla ni muda gani na je kama anataka kuwa officer ni lazima apitie kwanza JKT au anaweza hata kwenda TMA moja kwa moja?

Kwa anayejua chochote kuhusiana na haya mambo msaada tafadhali.
Kwanza ana bachelor ya masomo gani?. Kama udaktari au Masuala ya IT sawa. Ila nje ya hapo, akapambanie tu bahati yake anaweza asipate anachokitaka.
 
Mkuu umeniacha hoi kweli iyo kazi ni uzalendo tu sio kwenda kufuata pesa
Every soldier Think to be General.Sasa unataka kuwa askari huna nia ya kuwa kiongozi maana yake utakuwa private sugu na mkorofi usiyekuwa na tija jeshini. Utaratibu kwanza JKT apige jalamba la kufa MTU kisha JWTZ yaani hapo ukifika Unaanza tena A yaani kule JKT kama ulikuwa umetoka chumbani kwenda chooni tu hapo Sasa mziki wake kama kutembea kwa mguu kutoka Kagera kwenda Mtwara .Baada ya kuwa soilder kinachofuata kupiga malindo ya kufa MTU Yale ya hatari tupu si unajua ukianza kazi wanasema kuruta si MTU unafananishwa na Roboti ukishahenya hapo ndiyo upige peper la Officer cadate ukifaulu ndiyo upelekwe Monduli hapo maamaaaa utajuta kwanini uliamua kuwa askari maana haki za binadamu zinaishia getini hapo ni mwendo wa ubabe mapokezi tu mapushapu kama 300 kwa mpigo mmoja kisha karinyekarinye zingine zinaendelea yaani pale kuna ile mikamanda ya kimasai na kikurya elimu kubwa mwili nyumba anapiga ngumi noma halafu hanaga cha kuogopa na huna cha kumtisha .Apo mwendo wa mbwa mwanzo .Mpaka JPM akuvishe Nyota Si kazi ya mchezo mchezo ndiyo maana kwa wale wanawake hata kupata watoto inakuwaga shughuli kweli .Kwa ufupi jeshi si lelemama connection yake kwenye elimu ya chuo kikuu ipo kwenye kipindi cha ratiba za kazi za kawaida mfano We we daktari utakwenda hospitali,Mwanasheria mahakama za kijeshi na Military Police leader,Muhasibu mambo ya pesa ,Sasa kabla ya kukabidhiwa kwenye fani yako mziki wake inakubidi ufungue moyo maana Yale za mazoezi kwamba ukichoka unaacha Bali ni mafunzo hivyo hata ukichoka lazima umalize silabasi na lazima ufaulu. imba kidogo "MAJESHI SI LELEMAMA HAYAHITAJI KUBEMBELEZANA ' mara2
 
Mkuu yeye kasema analipenda jeshi na ataenda bila kujali vikwazo vitakavyojitokeza ila mimi ndo nimemsaidia kuuliza tu
Sawa nimekusoma boss, kwa mshahara now days kupo poa si kama zamani! akikunjua moyo fresh tu, kuna mambo mengi mazuri si vema kuweka kila kitu hapa.kwa upande wa vyeo mifumo imekuwa ikibadilika mara kwa Mara ( no specific formula) ila kwa sasa utaratibu ni lazima uanze na vyeo vya chini kabla ya nyota ya kwanza hasa kwa askari wa muda mchache kazini, Kama access ipo aende tu atafurahi mwenyewe ni uvumilivu na nidhamu kwa sana mengine atayakuta huko huko.
 
Kama anapenda basi hawezikuona shida yeyote, passion ndiyo kila kitu kwenye mafanikio ya maisha yetu ya kila siku.

Once you find out what your passion is. You will live the life that matters
Exactly.
 
Kwanza ana bachelor ya masomo gani?. Kama udaktari au Masuala ya IT sawa. Ila nje ya hapo, akapambanie tu bahati yake anaweza asipate anachokitaka.
Nnachoshangaa wanziacha sana za engineering na kuzipa kipaombele sana hyo ya udaktari wakt awamu hii mh raisi ametokea kuliamin jeshi( jkt) na kulipa miradi Mkubwa sana ya kitaifa inahitajika watalamu wa kutosha kwenye nyanja ya uhandisi kutimiiza na kuendana na matakwa ya amri jeshi mkuu
 
Hahahaha wewe jamaa umenichekesha
Every soldier Think to be General.Sasa unataka kuwa askari huna nia ya kuwa kiongozi maana yake utakuwa private sugu na mkorofi usiyekuwa na tija jeshini. Utaratibu kwanza JKT apige jalamba la kufa MTU kisha JWTZ yaani hapo ukifika Unaanza tena A yaani kule JKT kama ulikuwa umetoka chumbani kwenda chooni tu hapo Sasa mziki wake kama kutembea kwa mguu kutoka Kagera kwenda Mtwara .Baada ya kuwa soilder kinachofuata kupiga malindo ya kufa MTU Yale ya hatari tupu si unajua ukianza kazi wanasema kuruta si MTU unafananishwa na Roboti ukishahenya hapo ndiyo upige peper la Officer cadate ukifaulu ndiyo upelekwe Monduli hapo maamaaaa utajuta kwanini uliamua kuwa askari maana haki za binadamu zinaishia getini hapo ni mwendo wa ubabe mapokezi tu mapushapu kama 300 kwa mpigo mmoja kisha karinyekarinye zingine zinaendelea yaani pale kuna ile mikamanda ya kimasai na kikurya elimu kubwa mwili nyumba anapiga ngumi noma halafu hanaga cha kuogopa na huna cha kumtisha .Apo mwendo wa mbwa mwanzo .Mpaka JPM akuvishe Nyota Si kazi ya mchezo mchezo ndiyo maana kwa wale wanawake hata kupata watoto inakuwaga shughuli kweli .Kwa ufupi jeshi si lelemama connection yake kwenye elimu ya chuo kikuu ipo kwenye kipindi cha ratiba za kazi za kawaida mfano We we daktari utakwenda hospitali,Mwanasheria mahakama za kijeshi na Military Police leader,Muhasibu mambo ya pesa ,Sasa kabla ya kukabidhiwa kwenye fani yako mziki wake inakubidi ufungue moyo maana Yale za mazoezi kwamba ukichoka unaacha Bali ni mafunzo hivyo hata ukichoka lazima umalize silabasi na lazima ufaulu. imba kidogo "MAJESHI SI LELEMAMA HAYAHITAJI KUBEMBELEZANA ' mara2
 
Duh ila kwa yeye ataweza tu maana kapenda mwenyewe
Inategemea na fani yake ila kwa sasa huyo mdogo wako na bachelor degree yake aende uone degree zimekuwa kama mchele jeshini kwanza hazitakiwi zinafanyiwa figisu sana kwa sababu maalumu.
.
Mazoezi ni ya wote usiombe yakukute utakunywa maji sana
 
Back
Top Bottom