Msaada kuhusu elimu na Vyeo Jeshini

Msaada kuhusu elimu na Vyeo Jeshini

Anawaza cheo hahaha.
Kwanza itabidi aanzie JKT akitoka huko ndipo TMA itafuata hatapata ULUTENI USU kama ilivyokuwa zamani bali ataanza na sergeant (sajini) Bachelor degree zimekuwa nyingi sana jeshini kama mchele .
.
Bana kule hakufai kuna hivi vitu
1. Mwendo mkali
2. Tumekomaa
3. Heavy heart
4. Vunja viungo

Heavy heart ni shenzi kuna mwenzao aclamatization ni shida simkatishi tamaa mdogo wako ila ajiandae psychologically
.
mimi sio mwanajeshi
Mmhh mkuu sasa mbona nina ndugu yangu ana Diploma ila hivi sasa ninavyoandika ana nyota mbili na hajafikisha hata miaka minne jeshini

Halafu hivi mazoezi yote hayo wanafanya wote wanaume na wanawake au kuna mazoezi ambayo wanawake wanakuwa excluded?
 
Mpaka mi naondoka niliacha mambo yakiwa hivi..

Form 6 - nyota mbili (luteni) kuna mtu namjua kapata hicho cheo.

Bachelor degree - nyota tatu (captain).

Lazima apite Jkt miezi 6 ya kujitolea, baada ya hapo atapiga kozi ya TPDF yaani bakabaka kwa muda usiopungua miezi 4 hadi 6. Baada ya hapo ndio ataenda monduli kupiga kozi ya cadet officer kwa muda miezi 9. Baada ya mlolongo wote huo ndio ataweza kuwa afisa wa jeshi.

Kuhusu mshahara nakumbuka captain wetu aliyekua na nyota 3 alikua anachukua m3 kasoro hivi, kutokana na kauli mwenyewe. Na wenye nyota 2 inacheza kwenye m2 mbili kasoro point kidogo (kwa hapa am not sure).

Naongea from my experience ya miaka 5 nyuma, labda mambo yabadilike hivi sasa.

I hope nimesaidia.
Umesaidia sana mkuu yaani umejibu mule mule ila nitajaribu kufuatilia na kwa sasa kama mambo yamebadilika

Shukrani sana
 
Kuna wenzake wana masters bado wanajitolea huko JKT mwaka wa 3 sasa.

Jeshini hamna mshahara kuna 'posho' tu.
Mmhh haya mambo yanachanganya sana yaani mtu ana masters ila bado anasota JKT miaka 3?

Mbona nina ndugu yangu mwingine ana diploma lakini hivi sasa ninavyoandika ana nyota mbili na hajafikisha hata miaka minne jeshini au labda jeshini ni connections tu?
 
Hmmm...okay its yo experience we can't judge you.
Experience yangu me ya miaka miwili iliyopita plus na huu wa 3.nachokumbuka ni mwal.wetu alikuwa na nyota mbili na alikuwa na masters.
My friend Ana elimu ya form 6 ni private ndo kapata this August anaenda kozi ya usalama. Haina nyota hiyooo
Oohh huyo mwalimu wenu alichukua muda gani hadi kupata nyota mbili?
 
Sasa mbona unatuchora wakati mtu wa kumfanyia reference unae
Mmhh mkuu sasa mbona nina ndugu yangu ana Diploma ila hivi sasa ninavyoandika ana nyota mbili na hajafikisha hata miaka minne jeshini

Halafu hivi mazoezi yote hayo wanafanya wote wanaume na wanawake au kuna mazoezi ambayo wanawake wanakuwa excluded?
 
Mwambie aje huku kwetu kwenye Jeshi usu ale maisha. Hao masajini au Makoplo wanakula mili hazipungui 3. private huku tunaita Ranger anakula Milion 2 na laki 3. Thou mishahara ipo according to Scheme of service na sio Vyeo vya kijeshi. View attachment 1170837
Anha kwahiyo mshahara unategemea na mtu anafanyia kazi kitengo gani huko jeshini?
 
Mnaopenda kwenda jeshi sababu ya mishahara kuna siku mtagharimika tu... Every choice has its consequences.

I wish jeshi letu lingekuwa kama marekani. Maana wenzetu mpaka magenral wanaenda operation.

Bongo ingekuwa hivo basi watu wangekuwa wanaenda jeshini kwa kujitoa na siyo kwa ajili ya njaa ya pesa...
Hapana mkuu haendi kwa sababu ya pesa anaenda kwa sababu anapenda jeshi ila tu anahitaji kujua kuhusu course zake na hilo la mshahara ni kama swali la nyongeza tu ila yeye jeshi analipenda

Halafu sijaelewa hapo uliposema marekani hadi mageneral wanaenda operation yaani inakuwaje? Na je hawa wa tanzania hawaendi?
 
Mmhh haya mambo yanachanganya sana yaani mtu ana masters ila bado anasota JKT miaka 3?

Mbona nina ndugu yangu mwingine ana diploma lakini hivi sasa ninavyoandika ana nyota mbili na hajafikisha hata miaka minne jeshini au labda jeshini ni connections tu?
Nadhani mambo yamebadirika saizi, nakupa hii ni experience kutoka kwa jamaa zangu nliomaliza nao form six 2015

Kabla yetu, yaani waliomaliza six mwaka 2014 walikua wakienda jkt kwa mujibu wakabakizwa jeshini walifanya course kwa muda wa miezi 9 Tu then wakapata nyota but kwa tuliomaliza 2015 mambo yalibadirika kidogo maana Mimi kuna jamaa zangu walibakizwa jeshini wakakaa kwanza kwa muda wa mwaka mzima bila kufanya chochote just wapo Tu kambini wanaamka, wanakula na kulala ili kupimwa uvumilivu.

Baada ya hapo mwaka uliofata 2016 walipelekwa course ya miezi mitatu, maana wao walikua wamepitia jkt after form6 so ile miezi mitatu waliyopekekwa course ilikua kukamilisha miezi sita ndipo wakapata bakabaka, wakafanya kazi mpaka 2018, ndipo wakapelekwa Monduli kwa ajili ya course ya uafisa (nyota), na course ya uafisa kwa sasa hivi ni kama mtu anaechukua degree, so kwa mtu alietoka six anasoma uafisa kwa muda wa miaka mitatu kama anaechukua bachelor, but kama ana degree tayari huyo basi anafanya course kwa muda wa miezi Tisa tuu

Zamani ilikua mtu mwenye bachelor anenda moja kwa moja kufanya course ya uafisa (nyota) kama akichaguliwa kujiunga na jeshi, but kwa sasa si hivo tena, mtu mwenye bachelor akichaguliwa anaenda kuanza course ya ucadet kwa muda wa miezi 6 (wanaita kumtoa uraia wa kawaida) baada ya hapo anapata bakabaka then anasubiri intake ya kwenda kusoma uafisa (nyota) kwa muda wa miezi Tisa ila inategemea na mambo mengi kama vile Afya, connection, nidhamu, so kwa sasa mtu kuishia ucadet (bakabaka) ingawa ana degree yake ni kitu cha kawaida Sana kama amekosa vitu nilivyovitaja hapo , hope nimesaidia kwa namna moja ama nyingine.

NB: ukimaliza course ya uafisa kama Umetokea form six au Una bachelor unapata nyota moja (ingawa hapa sina uhakika Sana kama nimekosea watanisahihisha wengine)
 
Itamchukua takribani miaka miaka 2 kasoro hivi kutoka jkt hadi kuwa officer wa nyota moja (Luteni - usu)
Hapo ni nje na kusubirishwa kabla ya kwenda kozi yaani tunaasume ameenda smoothly mwanzo mwisho
Duuh aise kwahiyo inaweza kuchukua hata miezi mtu kusubiri kutoka kwenye course moja kwenda nyingine?
 
Mmhh mkuu sasa mbona nina ndugu yangu ana Diploma ila hivi sasa ninavyoandika ana nyota mbili na hajafikisha hata miaka minne jeshini
Halafu hivi mazoezi yote hayo wanafanya wote wanaume na wanawake au kuna mazoezi ambayo wanawake wanakuwa excluded?

Sasa hayo maswali si ungemuuliza huyo ndugu yako.??

Tatizo umei set akili yako kitu fulani alafu unakuja kuuliza ,unaambia ukweli unaukataa..

Jeshini sikuhizi ni kama enzi za nyerere uzalendo kwanza mbwembwe nyingine baadae..

Ataanza JKT, kisha atasota kwa muda fulani kupimwa uvumilivu, kisha atpewa bakabaka, kisha itamchukua muda si chini ya mwaka mmoja kuwa mwanajeshi wa kawaida, baada ya hapo atapelekwa kusoma u afisa(miezi 9), lakini hii yote inategemea connection pia so anaweza sota zaidi..
 
Msomi ukienda jeshini kwa ajiri ya ukosefu wa ajira kwa fani uliyosemea ipo siku utakuja jijutia huo uamuzi. Nenda jeshini kwa kupenda mwenyewe binafsi toka moyoni mwako..
Yeah yeye analipenda jeshi.

Na kwanini umesema hivyo mkuu?
 
Utaratibu sasa hivi umebadilia

MOJA: Askari anayetakiwa awe na nyota kwa UMRI ni chini ya miaka 23 kushuka chini,kwa experience yangu Uncle angu mda huu anapiga hiyo course ya uafsa.

MBILI: Hata kama utakuwa na Masters ni lazima uanzie chini yani nyota moja lakini kabla ya hapo utaratibu ulikuwa mwenye degree mfano ya MD atachukua nyota tatu.

TATU: course ya Uafsa ni miezi 9 na sio chini ya hapo.

Nb: Kuna uncle wangu mkubwa ana elimu ya form six lakini hakupata cheo chochote ila alivaa UKOPLO kwa Sababu ya fani yake CLINICAL OFFICER.

Jeshini usipokuwa na refa utapiga mihayo Sana utashangaa wa darasa la saba anavaa bakabaka ila mwenye Degree ya Engendering anarudi nyumbani.
Na hata mimi ndicho nilichogundua kwamba jeshini ni connection tu maana kila mtu anaongea lake

Nina ndugu yangu ana diploma ila hivi sasa ana nyota mbili na hajafikisha hata miaka minne jeshini
 
Kama unawaza vyeo jeshini utapata tabu sana kwa nyakati hizi na degree yako bora ukalime nyanya ziwe resources viwandani huko. Jeshi linahitaji kwanza kuwa na self committment na kupenda sio vipaumbele vya vyeo na mishahara.
 
Usisikize porojo za watu, hakuna mtu anayesota JKT zaidi ya miaka miwili, JKT mwisho wa kukaa ni miwili tu na baada ya hapo kama hukupata ajira ni nyumbani.
Sawa Sawa Mkuu
 
Back
Top Bottom