Nimekuwa mteja wa mtandao mmoja wa simu hapa nchini kwa zaidi ya miaka 20 sasa. Licha ya kupata huduma bora katika kipindi chote hicho, hata hivyo hivi karibuni nimekuwa Nikishuhudia wizi wa fedha nilizokuwa nikitunza kama akiba kwenye account yangu ya simu. Yaani unaamka tu asubuhi unataka kutumia sehemu ya fedha hizo unakuta hela takribani yote ilishapigwa!
Ukifuatilia sana unaishia kuombwa tu msamaha na hela kurejeshewa kwa maelezo kuwa wizi huo unasababishwa na wafanyakazi wasio waaminifu! Imefika mahali Nimekosa kabisa imani na huduma zao kwani hii ni ishara kuwa huenda hata taarifa za mawasiliano yangu zikawa hatarini kutokana na uwepo wa wafanyakazi hao wasio waaminifu.
Nawezaje kupata msaada wa kisheria ili hatua stahiki dhidi ya uhuni huu ziweze kuchukuliwa kwa lengo la kukomesha kabisa tatizo hili?
Nitashukuru kwa msaada wenu.
Ukifuatilia sana unaishia kuombwa tu msamaha na hela kurejeshewa kwa maelezo kuwa wizi huo unasababishwa na wafanyakazi wasio waaminifu! Imefika mahali Nimekosa kabisa imani na huduma zao kwani hii ni ishara kuwa huenda hata taarifa za mawasiliano yangu zikawa hatarini kutokana na uwepo wa wafanyakazi hao wasio waaminifu.
Nawezaje kupata msaada wa kisheria ili hatua stahiki dhidi ya uhuni huu ziweze kuchukuliwa kwa lengo la kukomesha kabisa tatizo hili?
Nitashukuru kwa msaada wenu.