The Finest
JF-Expert Member
- Jul 14, 2010
- 21,605
- 6,080
SAWEBOY I like your ideaMkuu pole kwa hayo yanakukuta. Kwa kuwa anasema kama umemchoka umwambie tu hapo lazima kuna jambo limejificha na wala usidhani masihara, kuna kitu anajivunia tu na wewe anakuona kwa sasa huwezi kumbabaisha especially kama kuna mtu pembeni na hiyo ni ngumu wewe kujua. Kwa kujihami usijue ndio maana anakujia juu coz ameshajua udhaifu wako kuwa akikupnadishia wewe unaua soo kwa kuwa mpole.
USHAURI MZURI
1. Wewe ndiye uliyemfungulia biashara anayofanya na kupata kipato kizuri tu, pia usafiri umempatia (ana bahati sana ya kupendwa ila hapendeki huyu dada) kwa hiyo hakuna tatizo la wewe kumuogopa, hapo unaibiwa mkuu lazima kuna mtu ana-msugua pembeni bila wewe kujua. Chukua hatua haraka mkuu/ tena faster! Hatua gani sasa ya kuchukua?
2. Mtegee ishu kidogo tu, muulize kwa upoleeee kabisa akikujia juu, we ni mwanume na ndio uliyemuoa hivyo mrudishe kwao kwa mapunziko bila kumwambia lini utamfuata au mwambie rudi nyumbani kwenu na utakapoona umebadilika tabia na kutambua mimi ni mume wako hapo ndipo urudi lakini usirudi kabla ya miezi 6 au 3 hata kama akijua kosa lake!
3. Endapo ukiona amefurahia kurudi kwao na huku anakujibu kwa jeuri basi ujue hapo huna ndoa mkuu lazima ujue kuna mtu anachakachua tu hiyo kitu but ukiona anakuwa mpole ghafla usibadili uamuzi muache aende akajifunze na akirudi kuja kutubu hatarudia tena.
NB: akifurahia kurudi kwao basi ndani ya mwezi 1 utajua nani anasugua huyo mashine na hapo ndo utajua jeuri ya mkeo inatoka wapi.
Pili usimruhusu kuondoka na mtoto, mwambie aende na mtoto amwache home lkn akilazimisha basi muachie mtoto aende nae!
CHUKUA HATUA HARAKA SANA MKUU