NyaniMzee
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 396
- 727
Wana JF, na hasa wale wenye weledi na mambo ya ndoa.
Mke wangu niko naye miaka 3. Tuna mtoto 1 wa miaka 3. Nimemfungulia biashara nzuri, anaingiza pesa nzuri tu kwa siku. Usafiri nimempa wa kumpeleka kazini kwake na kumuwahisha home. Tatizo moja linanikwaza: nikitaka kujua maswala yanayohusu pesa au marafiki zake hata wa kike tu, basi majibu yake huwa ni mkato na ya jeuri, na hachelewi kusema usinisimange au kama umechoka niambie.
Kuepuka shari mimi huwa najishusha na kumtuliza kuwa haikuwa kwa nia ya kumkwaza bali kama mume nina haki kujua. Hajui kusema samahani hata pale anapogundua alikosea kauli. Sasa haya maisha dawa yake nini? Nami sitaki kuzurura, napenda niishi naye kama ahadi ya ndoa.
Wakuu mawazo yenu please!
Mke wangu niko naye miaka 3. Tuna mtoto 1 wa miaka 3. Nimemfungulia biashara nzuri, anaingiza pesa nzuri tu kwa siku. Usafiri nimempa wa kumpeleka kazini kwake na kumuwahisha home. Tatizo moja linanikwaza: nikitaka kujua maswala yanayohusu pesa au marafiki zake hata wa kike tu, basi majibu yake huwa ni mkato na ya jeuri, na hachelewi kusema usinisimange au kama umechoka niambie.
Kuepuka shari mimi huwa najishusha na kumtuliza kuwa haikuwa kwa nia ya kumkwaza bali kama mume nina haki kujua. Hajui kusema samahani hata pale anapogundua alikosea kauli. Sasa haya maisha dawa yake nini? Nami sitaki kuzurura, napenda niishi naye kama ahadi ya ndoa.
Wakuu mawazo yenu please!