Zamaulid
JF-Expert Member
- May 25, 2009
- 18,656
- 13,481
Sasa mmoja akifa itakuwa taraka!! Sheria inaruhusu kuachana pale mmoja anapokuwa mzinifu!Sheria ya talaka za kikristo ni lazima mmoja afe!!!!!
Sasa mmoja akifa itakuwa taraka!! Sheria inaruhusu kuachana pale mmoja anapokuwa mzinifu!Sheria ya talaka za kikristo ni lazima mmoja afe!!!!!
Procedure ni kwamba, ukitaka talaka lazima upitie baraza la usuluhishi, ikishindikana watakupa form ambayo inakuruhusu kwenda mahakamani, sasa hiyo form ndio utampa wakili wako, umuelezee matatizo yooooote, from there ndo ataona kama sababu yako ya kutaka talaka inakubalika kisheria. Madhumuni ya ulazimu wa kupitia baraza la usuluhishi ni kwa sababu mahakama haitaki kuvunja ndoa,marriage is a sacred union. Lazima waone kwamba ndoa yenu/mahusiano yenu yamefika kilele kabisa na hakuna namna ya kurudiana.
Baraza la kata alienda,wamekua kama wanamzingua hivi coz mwenzie(mkewe) alienda akasema uongo kwenye baraza kuwa wameshapatana,so baraza wakafuta hilo shauri. Inabidi aende akafungue tena hilo shauri kwenye baraza,au?
Huyo mwanamke inaonekana ana sauti hapo mtaani kuliko kaka yako. Sasa inabidi pesa itumike mwambie kaka yako ampe pesa/ rushwa huyo mtendaji wa kata ili apeleke upya malalmiko na kikao cha usuluhishi kiitishwe. Kwenye kikao akomae kuonyesha weakness za wife ambazo kimsingi ndio sababu zinatambulika kisheria kuwa akipatikana nazo basi hapo ndoa hamna na inabidi talaka itolewe. Mfano kama mke ni mzinzi, mkatili/abusive kwake na watoto. Hivyo baraza la usuluhishi litatoa certificate ya kuonesha usuluhishi umeshindikana, akishapata hiyo anyookee kwa lawyer ili mchakato wa kupeleka madai ya talaka katika mahakam husika uanze.
Nashukuru Daisy,kaka ameondoka nyumbani kwake huu ni mwezi wa 3 sasa,ameamua aishi mwenyewe. Walifikia pabaya coz alishamjeruhi kaka mara kadhaa,alishamuwekea sumu kwenye chakula na sasa anampigia simu kumtishia kuwa atamfanyia kitu mbaya kama hatarudi nyumbani kuishi na yeye(mwanamke). Ngoja nimwambie aurudishe mchakato baraza la usuluhishi kata.
Sheria ya talaka za kikristo ni lazima mmoja afe!!!!!
Tena mwambie aandike kabisa barua kwa mtendaji wa kata akieleza hizo complaints dhidi ya mkewe, aipeleke kwa dispatch ipokelewe hapo ofisini ili muda ukipita say 3 months na hakuna kikao cha usuluhishi kimeitishwa, then anaweza kupeleka petition yake mahakamani bila kuwa na hiyo certificate na uthibitisho kuwa alipeleka malalamiko kata lakini kikao hakikuitwa itamsaidia kuonensha kwamba nia na jitihada za kupeleka mgogoro kwenye reconciliation board alifanya lakini inaonekana kuna extraordinary circumstances zilizopelekea hiyo bodi kushindwa kufanya usuluhishi na ku-issue the appropriate certificate.
Je, mumesaidia kuinusuru hiyo ndoa ya ndugu yenu kwa kufunga na kuomba sana, Mungu hapendi kuachana jamani.Habari zenu wadau!Kuna kaka angu amefikia kikomo cha uvumilivu kwenye ndoa yake(ya kiksristo) na ameamua kuivunja. Hajui taratibu za kufuata ili afanikiwe kutoa talaka. Msaada please kwa waijuao sheria
Dini gani ?
Cheti cha ndoa kina gharama? Na kama kinagharama ni kiasi gani? Je,wanandoa wa dini zote wanacheti cha aina moja?
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Ok,nimekusoma.Je,kama nimeoa na mimi nikawa source ya matatizo ndani ya ndoa lakini bado nampenda mwenzangu na mwenzangu(mke) akaitaji tuachane,Je anauwezo wakutoa/kuomba taraka kisheria?!
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Kulingana na sheria hiyo tafsiri ya ndoa ni nini
Je waweza kukaa/ishi na mwanamke/mwanaume kwa muda gani itatafsirika kuwa ndoa?