lukindo
JF-Expert Member
- Mar 20, 2010
- 8,466
- 9,028
habari wana jf
sina uhakika sana na jukwaa nililoingia na naomba kama nimekosea mods ipeleke kunakostahili.
Nimepewa hii kitu kwenye daldala jana usiku kama 'change' ya nauli na sikuwa na mashaka juu yake kwa vile niliamini na mpaka sasa naamini kuwa ni Fedha Halali kwa Malipo ya Shiling Mia Tano, 500/-!
Leo asubuhi nilivyojaribu kumpatia konda kwenye daladala akanitolea matusi na kuikataa, ikanibidi nifanye maarifa ya ziada ili kufika nilikokuwa naenda.
Nilipofika nilikokuwa naenda nikaitoa kununua maandazi, wakakataa pia.
Ndipo nikaenda kwenye kibanda cha vocha ili angalau nipate uwezo wa 'kubeep' kwa bahati mbaya nako wameikataa.
Wote wanasema sio pesa, sasa wana jf nauliza ni kitu gani hiki!!??
Nawasilisha
sina uhakika sana na jukwaa nililoingia na naomba kama nimekosea mods ipeleke kunakostahili.
Nimepewa hii kitu kwenye daldala jana usiku kama 'change' ya nauli na sikuwa na mashaka juu yake kwa vile niliamini na mpaka sasa naamini kuwa ni Fedha Halali kwa Malipo ya Shiling Mia Tano, 500/-!
Leo asubuhi nilivyojaribu kumpatia konda kwenye daladala akanitolea matusi na kuikataa, ikanibidi nifanye maarifa ya ziada ili kufika nilikokuwa naenda.
Nilipofika nilikokuwa naenda nikaitoa kununua maandazi, wakakataa pia.
Ndipo nikaenda kwenye kibanda cha vocha ili angalau nipate uwezo wa 'kubeep' kwa bahati mbaya nako wameikataa.
Wote wanasema sio pesa, sasa wana jf nauliza ni kitu gani hiki!!??
Nawasilisha