Okay ngoja nikacheki then nitaleta feedbackKwa budget hii itabidi utafute laptop yenye igp ya intel hd 4600 ambayo utaipata kwenye processor yoyote ya laptop inayoanziwa na 4 na kuishiwa na m.
i3 4000m
i3 4100m
i5 4200m
i5 4300m
i7 4600m
Morogoro road mjini zipo nyingi hizi laptop pitia maduka mbali mbali ziangalie chagua utakayopenda. Kama unaona ngumu pick unazohisi zinafaa leta specs zake hapa wadau watakusaidia kuchagua nzuri
Kuna gpu za aina mbili
1. Inayokuja na cpu (igp) ambayo inakuwa integrated na processor
2.gpu isiokuja na cpu (dedicated) ambayo inakuwa mara nyingi ni ya nvidia au amd/ati
Hizi gpu zinazokuja na cpu (igp) hasa za intel zinakuja na technology kama quick sync ambazo zinafanya rendering upesi sana hivyo kuondoa umuhimu wa gpu za nvidia na amd kwenye mashine za bei rahisi.
Kuhusu kuunguruma inamaana power supply na mafeni/cooling system yamezidiwa uwezo na yanafanya kazi kubwa nje ya uwezo wao.
Kuhusu gpu nzuri inayokufaa inabidi useme budget yako na unataka laptop au desktop
Nimepitia hapa nimeona hicho ulichosemaNimeigoogle hapa hiyo tofauti ya dedicated na integrated , it seems dedicated ni superior na bei iko juu kuliko integrated
Nimepitia hapa nimeona hicho ulichosema
Graphics Cards: Integrated vs. Dedicated - TopTenREVIEWS
Hii thread nimejitahidi lakini naona nyota tuu-ngoja nipite
Dell Precision M4600
(Intel Core i7 2920XM,
NVIDIA Quadro 2000M) RAM 4 GB, 500 GB HDD
Naomba review yako hapa mkuu Chief-Mkwawa
Nimeigoogle hapa hiyo tofauti ya dedicated na integrated , it seems dedicated ni superior na bei iko juu kuliko integrated
Laptop nzuri kaka, hio processor japo ni generation ya zamani (2nd generation/sandy bridge) ila bado ina nguvu sana. Ina core 4 na thread 8 hivyo kitu chochote utakachotupia itafanya. Pia single thread perfomance ni nzuri.
Hio gpu imekuwa optimized kwa watu wa design/video/3d/graphics editing pia unaweza cheza games ila kwa hd haitoweza kuhandle full hd/2k/4k games.
Kitu ambacho nitahofia kwa hio laptop ni upataji moto maana processor yake ina tdp ya watts 55 na gpu pia itaongeza watts nyengine
Sipati picha adapter yake ipoje.
Yap kiuhalisia dedicated ni nzuri ila si dedicated zote ni nzuri.
Mimi nilizunguka madukani dar gpu nyingi ni nvidia gt 610 na amd 5450.
Hizi gpu ni mbaya kupitiliza na bei wanazoziuza ni 100,000 hadi 450,000. Unanunua gpu unajua una upgrade pc kumbe kiuhalisia una downgrade. Angalia passmark score za hizo gpu compare na intel hd 4600 ambayo ni igp.
Intel hd 4600 = 717
Nvidia gt 610 = 357
Amd 5450 = 231
Hivyo unaona igp inaipita kiurahisi dedicated.
Pia kuna igp kama iris pro zinachuana na dediacated za kati kama gtx 750
Hii kitu wakuu inasimamia sh. Ngap kwa duka
*Manufacture: Dell
*Model: Latitude E6440
*Processor: Intel(R) Core(TM) i5-4300M CPU @ 2.60GHz 2.60 GHz
*RAM 8
Habari za wakati huu wakuu,,,
Nina laptop yangu aina ya Acer inatatizo la internal mouse (touch pad) hairespond.
Hivyo nalazimika kutumia usb mouse..naomba msaada wenu jinsi ya kurekebisha hili.
Inaweza chezea laki 9 hivi
Aisee wakuu huu uzi ulikuwaga wap skuzote, hebu nsaidien kuhusu hii machine ya
Hp envy 17 leap motion
Intel core i7 4710MQ 2.5gjz 3.5ghz turbo
Ram 16 gb ddr4 upgrade, 4gb vga dedicated card, 4gb nvidia card,
17.3 inch screen optional 1080p resolution.
Sasa wakuu sijaelewa kitu, mashine yangu ya kwanza ilikataa kuplay fifa 15 ambayo nayo ni ilikuwa envy 15 core i5 2.4ghz 8gb ram, intel hd graphics. nkaamua kuuza na kununua hyo kutoka Uk.
sijaelewa hapo kweny 4gb vga dedicated na 4gb vga nvidia wanamaana gani. Nkilinganisha na maelezo yenu ndo najichanganya kabisaa
mara ya kwanza nlihis ram na processor corei5 and above ndo mpango mzima kweny game kumbe kuna issue za graphics tena.
Kitu Nachohofia nshanunua mashine kwa ghali sana af isije kataa game zingine thou fifa 15 inaplay fresh. Ina miez 2 tu