Click Hapa
JF-Expert Member
- Jan 27, 2013
- 479
- 206
Mkuu,
Kuna mambo mengi ya kuendelea kujiuliza na kufanya utafiti wa kutosha.
Mfano: Kuna kampuni/jamaa wanakuja nchini kutokea nje ya nchi na sanasana ni Wahindi, wanaweka kambi humu nchini na hasa mashambani huko, wananunua mazao kama Ufuta, Choroko, Mbaazi, Dengu na mazao mengine ya jamii ya Mikundekunde, wanapopeleka huwa hatupajui na hakuna anayejishughulisha kujua huwa wanayapeleka wapi, kwa kifupi hapa namaanisha MASOKO.
Kama bidhaa hizi zipo hapa nchini kwetu kwanini sisi tunaishia tu kuwauzia hawa wanaotulangua, ina maana sisi hatuwezi kupeleka huko wanapopeleka wao.
Hebu tufunguke vijana. Na kwa sasa nina imani na serikali tulonayo.
