Msaada: Dawa nzuri ya kuua nzi

Jamani hii chumvi mi naiogopa niliwahi kuinyunyizia kwenye nyumba ya watu mmh naona niliamsha yaliolala.... kesho yake nilibeba pochi na nguo za kazini nikaacha nyumba, nilirudi baada ya miezi miwili kurudia vitu vyangu.
Ilikuwaje?😀
 
Kwanza hizo kamba au waya ondoa kabisa maana ndio choo chao hicho
Naona hujui hivyo vyeusi ni nini

Zingatia usafi sana
Ikishindikana hapo basi mwambie mwenye nyumba unaenda Sumbawanga mwezi ujao umletee nini?
Yaani hata kabla ya kuuweka huo waya bado mziki wa hao nzi kwa ndani ya nyumba usipime!!
 
Inauzwaje?
 
Nenda kigoma au Malawi haraka sana
 
Nenda maduka ya dawa za mifugo kuna dawa ipo kwenye pakiti jina nimesahau uwiiii inaua mpk huruma ukimwaga leo hata ukideki nzi akitua kesho anakufa
Nahisi tatizo sio kuua tatizo wao kuja, sitaki waje kabisa. Nataka dawa ya kuzuia wasije
 
Nenda maduka ya dawa za mifugo kuna dawa ipo kwenye pakiti jina nimesahau uwiiii inaua mpk huruma ukimwaga leo hata ukideki nzi akitua kesho anakufa

Yes ni ya unga mweupe kama sukari hivi ,ni balaa halafu inauzwa simple tu haizidi jero kwa pakti.
 
Nahisi tatizo sio kuua tatizo wao kuja, sitaki waje kabisa. Nataka dawa ya kuzuia wasije

Mbona nyuma kama sio safi ukiingalia? Ebu safisha vizuri na sabuni ya unga ,loweka kitambaa kwenye maji yenye sabuni ya unga kisha safisha madirisha na kuta/floor.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…