Msaada: Anatumia kiwanja changu kuweza kufika kwake

Saitot

JF-Expert Member
Apr 3, 2013
613
151
Ndugu marafiki nahitaji ushauri wenu, nimefanikiwa kujenga nyumba yangu eneo fulani mkoani Mbeya.

Lakini kuna jirani yangu ambaye anatumia eneo la kiwanja changu ili aweze kufika kwake na ni mbele ya nyumba yangu.

Nimeshamwambia kwa mdomo na kwa maandishi kwamba natahitaji kutumia eneo hilo , hivyo atafute sehemu nyingine ya yeye kuweza kufika kwake, lakini naona kuna aina ya kiburi na uchonganishi kwa majirani wengine kwamba namzibia njia.

Kwa sasa ninapoandika na kuomba ushauri kwenu nipo masomoni Muhimbili, lakini kabla ya kuja hapa nilishamwandikia maelezo ya kutumia eneo hilo kwa mwaka 2016 mwaka ambao masomo yangu nitakuwa nimemaliza.

Lakini bado ninapokuwa likizo sioni jitihada anazozifanya kutafuta njia mbadala, ndugu zangu sitapenda kufanya jambo bila kuwa na maamuzi sahihi hivyo basi nalileta kwenu nipate ufumbuzi.

Ahsante
 
Jambo kubwa la kuangalia ni je ukiziba hilo eneo kwa matumizi yako huyo jirani yako ana namna ya kufika kwake je kuna njia mbadala!?km hamna ni vyema mkajadiliana na hata kumuuzia hilo eneo maana hakuna maana ya kumzibia njia hasa mkizingatia wote mpo kwenye eneo lisilopimwa hivyo ni jukumu lenu nyote kuhakikisha eneo lenu linafika kwa urahisi!
 
Uwanja ni wako, fanya upendavyo, ndo maana watu wenye uwezo wanaweka uzio, baadaye utaanza kuona mara mtu analima
 
Lazima muongee.muuzie iyo sehemu kama hana njia ya kupita.maana viwanja vyenu wote havijapimwa.bisha.
 
Ikiwa ni jirani yako na kupita kwake sasa hakukuathiri vyovyote nadhani mwache atumie till pale utakapohitaji privacy uzungushe ukuta!
 
Mkuu tafuta namna nzuri ya kulimaliza hilo suala make uungwana ni vitendo mkuu.
Ebu fikiria tu, wewe leo hii upo dar ukitaka kufika mbeya lazima usafiri kwa bus kupitia barabara ambayo yalikuwa ni mashamba ya watu lakini hawakuwa wagumu kuruhusu hiyo barabara au njia kupita.
Naimani hata wewe ili upafikie kwako lazima upite viwanjani mwa watu kadhaa.
Ustawi wa jamii siku zote huanza na mtu, so fanya uwe wa kwanza!!
 
Je wewe ukipita kwenda kwako hupiti kwa mtu, kama kwako kunapitika weka fence, kama kwenda kwako na wewe mpaka ukatize kwa mtu tegemea na wewe kufungiwa njia!
 
Fanya utaratibu ujenge ukuta

Majirani wakorofi wanaanzaga hivyo hivyo , mwisho mnadumbuana kwa ugomvi mkubwa

Hao majirani wengine kama imewauma sana wampe wao njia

Kwanza atanunuaje kiwanja bila kujua atafika vipi kwake???
 
Mmh hyo roho.mbaya ss mwenzio.apite wapi kaeni myazungumze dunia hii tunapita HV vyote tutaviacha
 
nawashukuru wote kaka na dada kwa ushauri wenye weredi , nimepata majibu kutoka kwa wengi nawapenda wana jamii forum.
 
kama hakuna njia inayoweza kumfikisha kwake naomba uvute subira. au mpe maoni kwamba ungekuwa wew ungefanya nini kupata njia nyingine. fanya hayo bila jazba utakuwa na aman.
 
kama hakuna njia inayoweza kumfikisha kwake naomba uvute subira. au mpe maoni kwamba ungekuwa wew ungefanya nini kupata njia nyingine. fanya hayo bila jazba utakuwa na aman.

Ahsante Pedama , ni kweli sina amani na ndicho nnachokitafuta.
 
Back
Top Bottom