Msaada: Aliyewahi kufikia hatua hii- Alitokaje?

Msaada: Aliyewahi kufikia hatua hii- Alitokaje?

Mkuu usikate tamaa, kuna wakati tunapimwa tu but with time it gets off!

Inahuzunisha sana, huwez amini kuna kijana nina mazungumzo nae anauza figo yake m35 ili atumie ktk maisha yake. Kweli maisha ni magumu, ila umefanya vyema kwani hapa hutatoka kapa.

Jaribu kubadili mazingira, hata bush nenda tu mkuu, au kama ukipata upenyo jichomeke kwa wakimbizi wanaopelekwa abroad. Nimekutana na watz kibao wanaojifanya congolese kumbe walijichomeka na kuletwa huku ka refugees.

All in all Mungu akutangulie, ukifanikiwa uje kutoa mrejesho
 
''Hizo ni issue nilizofanya bila kujali elimu yangu ya Degree ya BA. Lengo lilikua kupata pesa ya nauli wakati nikiwa dar na ya kununulia bahasha kwa ajili ya job applications.'' kama una degree hiyo mbona rahisi. anzisha msaada wa masomo ya ziada kama umekosa shule ya kujiegesha hapo bongo mbona fasta tu utatoka?
 
kupita majaribio kama haya ndiyo ubinadamu wenyewe ila wako wachache wanakuta kila kitu kutoka kwenye familia..
 
Pole sana mkuu. Ni kweli maisha yamekua magumu kwa kila mtu. Pengine hio ndio inapelekea uone ndugu zako wa Dar si wakarimu, huwezi jua nawenyewe wanapigika kiasi gani.

Ushauri wangu; bado unanafasi hutakiwi kukata tamaa. Wewe ni kijana na Mungu amekupa afya njema. Unachotakiwa kwanza kua positive na maisha na kua na malengo ya muda mfupi na mrefu.
Sifahamu uwezo wako kielimu baada ya kumaliza chuo, ila kuna watu wametoa wazo la kujitolea kwa muda kufundisha, nafikiri wazo lao ni zuri.

Pili, umezungumzia umewahi kufanya kazi za vibarua lakini hazijasaidia. Je umewahi kutazama fursa nyingine zinazopatikana?? Mfano, unaweza kufanya vibarua ukapata mtaji kidogo hata wa kufanya biashara stendi au sokoni ( kutegemea na mtaji wako) meanwhile unaendelea kusaka fursa zilizopo.

Tatu, tengeneza network ya watu uliosoma nao. Sio wote watakua wabaya unaweza kupata michongo mingine ya maisha.

My take; kujifungia ndani na kusononeka sio suluhu ya shida zako. Ni wakati wa kutumia vipawa vyako na uwezo wa kufikiria. Hata huko kanisani ukiwa unaenda kila siku halafu hutoi sadaka una hatari ya kutengwa ( mengi japo sio yote yako kibiashara zaidi). Shida ameumbiwa mwanadamu ni jukumu letu kuzikabili!
 
Pole sn Mkuu!

Mkuu Km utaweza jitahidi kupata nguvu ya pesa uende Dar, huko fulsa ni nyingi na mzunguko Wa pesa ni mkubwa kuliko huku kwetu bara! Km unaweza ukapata makazi Dar ni vema ukaenda huko na ukifika usichague kazi Km unatafuta. Kwani Ukipata kz yeyote ile kwanza itakupa uwezo Wa kukaa mjini Na pia itakupa connection mbalimbali. Kikubwa uweke malengo na uyatekeleze na uwajibike. Angalia kwa huko Dar starehe ni nyingi sn Km utapitiwa utashindwa kutimiza malengo yako!

Km ukifika Dar kwa lengo moja na ukawajibika vizuri. Ni miaka mitatu tu utakua umepata msingi Kiasi!

Kwa mikoani Mkuu ni kugumu!

Mzunguko Wa pesa uko chini, nafasi za ajira sio nyingi Na ata mikopo sio mingi!

Kumbe Shinyanga. Mimi Nisikushauri Uje Dar Mapema. Lima Viazi Vitamu Vingi Mkuu, Kama Vikiwa Tayari Ni Pm Tuone Namna Ya Kuvisafirisha Vinasoko Kubwa Sana Dar. Tafuta Kamtaj Then Upige Mishe Ya Viazi
 
Sasa MKUU GAZETI, Naomba Umrahiishie Kazi The Need, Amesota Saaana. Muwasiliane Umuelekeze Hizo Dawa Kisha Aje Na Majina Makubwa Zaidi, Akipata Pesa Apumzike
 
Ndugu wanajf....nimejaribu kila mbinu za kupambana na maisha kasoro kuiba mpaka sasa sijafanikiwa...ndio kwanza naona maisha yanazidi kua magumu sana.


Anything u mention, nimejaribu bila mafanikio. Is like upo kwenye ulingo wa ngumi na unapigana na Mohamed Ally au Cheka. Kila ukirusha ngumi moja...unamiminiwa 30 za haraka haraka tena zenye maumivu mpaka unaanguka huku damu zikikutoka.


Sasa nimeamua kumuomba Mungu tu...naenda kwenye maombezi mbalimbali. Sometimes nafunga na kuomba...

Nimekua mtu wa kushinda ndani tu. Naona giza tu mbele yangu. Nipo lonely sana. Sina kazi wala kitu chochote cha kuniingizia kipato.


Kazi nimetafuta sana bila mafanikio. Biashara nimefanya pia.



Mpaka sasa sijakata tamaa kuomba ajira na kufikiria mbinu za kupata pesa. But nimekua wa kukaa tu sina uelekeo.


Kwa yeyote aliyewahi kua na hali hii...ilikuaje akajikuta anaanza kupata neema?

Pole sana..
Amini ushafanikiwa.. Naku'pm fursa za hapo Shy.. Usiache kunipa mresho!
 
Au kwa faida ya wengine pia ngoja niweke hapa,

A) Hapo Meatu, akija Salum Mbuzi (former mp) kutembelea wapiga kura wake, muombe privacy. Mueleze elimu yako, mwambie shida yako. Nakuhakikishia pamoja na ukorofi wake lakini ni mtu mzuri sana.. Amefungua viwanda vipya na hana profshno staff.. Utapata ajira, hasa akiona wewe ni wa Meatu.. anawajali sana watu wa huko.. au kama unaweza mfate kiwandani kwake, JAMBO.

B) Kuna mgodi unaitwa Mwakitolyo, ni mpya, upo kakola. pale kuna fursa nyingi. Jaribu kwenda.

C) Nenda Maswa, Mwabomba, kuna migodi midogo midogo, dhahabu inapatikana pale, usisikilize maneno ya watu, nenda na nyanja hyo.

D) Jaribu kwenda Mhunze kwenye minada ya mbuzi mara nyingi. Ongea na watu mbalimbali hasa wageni wanaokuja kununua mbuzi kwa jumla, wambie elimu yako.. Nakuhakikishia unaweza kuwa partner na wao.

E) Ili yote hapo juu yafanikiwe, basi penda kusali sana. Muda mzuri wa kuomba Mungu ni saa 8 usiku.. ambapo kila kitu kimetulia na unapigana na nguvu za wachawi ambao ndio muda wao!

BYE
 
Pole ndugu, kwanza nakuomba katika kipindi hiki usijishughulishe na mambo ya ulevi kwani utaharibikiwa zaidi, pili kazana kumwomba Mungu utapata njia ya kutokea. Mimi nilipitia njia kama yako utafikiri umecopy, ilifika wakati hata nikiona mtu anatoa noti ya elfu moja nashangaa amepataje ila nilipoamua kumtegemea Mungu nilipata kazi na sasa hivi nina biashara zangu binafsi. Mtegemee sana Mungu.

Mpe mwanga zaidi ulifanya nini na nini ukapata hiyo kazi na biashara umetoa maelezo mengi lakini sijaona uahauri wa maana uliompa.
 
Asiache Kuleta Mrejesho Jf

Yah! Ni kweli.

Na nimemshauri, si kwamba mimi nimefanikiwa, la hasha! Isipokuwa nafahamu fursa nyingi zipo mikoani kuliko Dar. Dar imebaki kuishi kiujanja ujanja tu. Nimezunguka mikoa mingi na kujua potentiality ya kila mkoa.. For graduates, if ur upcountry, never never ever think of coming to Dar, a place is jammed.. Huko mkoani opportunities ni nyingi sana.. Since many higher learning institutions zipo Dar, then wengi wa wanafunzi kutoka mikoani wakija huku kusoma hawarudi kwao (wameshaona mataa na wametembelea Kigamboni) so inasababisha mikoani kuwe na upungufu wa wasomi..

Hapo ndio pa kupigia bao kama upo huko..

FIND THA OPPORTUNITY..
KNOW THA OPPORTUNITY..
USE THA OPPORTUNITY..

HELP OTHERS TO KNOW!!
 
Ntuzu. ..ushauri wako ni mzuri. Ila dar sio kwepesi namna hiyo. Nimekaa huko kwa mwaka mzima...mpaka nikaamua kubeba tofali ili niwe napata pesa ya kula na nauli. Maisha yalikua magumu sana. Ndugu wa Dar wengi ni wachoyo....vyakula wanaona kama unamaliza. Ndugu wa Dar hawapendi wageni kama mimi tegemezi. Wanataka ukienda kwao...ufanye shughuli na ue unarudi usiku sio kukaa kaa tu ovyo. Na ue na uwezo wa kula mtaani.

Hapo ndiyo ilikuwa fursa ambayo ingekufanya utoke inaonekana wewe unatatizo la kisaikolojia na ni muoga sana wa maisha sidhani kwa mtu wa jinsi yako kama unaweza ukatoka kwa kufikiri utapata kazi kwa urahisi,

jua unaponyayasika ndipo akili inapanuka ubongo unakuwa scrached sasa wewe ukakakimbia dar kwa kuogopa tofali na kunyanyaswa naamini kama ungekomaa kubeba tofali ungejua jinsi ya kuvyatua tofali ambapo kila mfuko inapata sh 3000 na unaweza ukafyatua hata mifuko mitano kwa siku.
 
Thousand miles started with a single step
Trust in God alone
Be courageous
Start with something even volunteering
 
Kumbe Wasukuma wakiona ndugu anapata tabu katika maisha wanafurahia. Sikujua aisee. Ok. Mkuu nenda mgodini ukahangaike ukifanikwa kupata kibarua unafanya kazi hata miezi sita unachukua chako unaondoka maana mazingira ya mgodini pia sio mazuri ila ni rahisi kupata kazi kwakuwa kila siku watu wanapata job na kuacha.
 
Mlalamikaji pole sana kwa changamoto unazokutana nazo, lakina unaomba ushauri wakati huohuo umetufunga mawazo yetu tusiyalete kwako, ulipoandika "anything u mention" nimeshajaribu una maana gani.
Wewe ni msomi whatch out ur wording, jiuze vizuri ie degree yako ni nini? umemaliza mwaka gani? chuo gani, weaknes and strength kama kweli unahitaji ushauri inabidi uwashawishi watu kama kweli ni msomi.
Mimi nijuayo changamoto kwa wasomi ni kupata kazi kazi ambayo ni ndoto zako (dream job) lakini kama ni kazi ilimradi mkono uende kinywani zipo, kuna shule za kata na wazazi zinahitaji walimu, njoo kigoma ufundishe Uvinza, Luchugi, Ujiji sekondari ni wewe tu wakati huo huo unanyemelea ajiri za Halmashauri ya Kigoma, Uvinza, Buhingu, Kakonko, Kibondo kuna halmashauri mpya kwa hiyo kuna shida ya watumishi.
 
Pole sana kaka, Mungu yupo pamoja nawe hapo chagua upi ni ushauri mzuri na kuu fanyia kazi ipasavyo
 
Asante kwa ushauri mzuri sana. Nitatoa taarifa kesho ama kesho kutwa nitakua wapi kati ya sehemu ulizotaja. Though ndio kulala nje...maisha ya kisela...huna rafiki wala nini...hujui utakua unalala vipi au kula vipi.

Naamini Mungu ni fundi. Hata wewe umeandika hayo ni kwa grace ya Mungu tu. Mungu kashika vidole vyako unishauri ivyo.


Asante sana sexilogist.
 
Kwa wenye emmanuel tv...ibada imeanza. Lets watch it live from the Synagogue Church of All Nations,Nigeria.


Live broadcasting
 
Back
Top Bottom