Serikali haijazuia uhuru wa mtu kujieleza (freedom of expression). Ndiyo maana Tanzania ina utitiri wa vyombo vya habari kuliko nchi yo yote nyingine hapa duniani. Serikali inachotaka uhuru huo wa kujieleza usivuke mipaka ya sheria, kanuni na taratibu zinazotoa uhuru huo. Uhuru wa mtu unaishia pale pua ya mwenzake inaanzia.
Serikali inachotakataza ni lugha isiyo na staha isiyozingatia maadili na inayoweza kusababisha uvunjifu amani na inayokiuka utamaduni wa mtanzania, katika kuhoji au kukosoa serikali au mtu mwingine ye yote. Kwa mfano utakuta mtu anamkosoa spika wa bunge mwenye umri sawa na baba yake akisema, 'Wewe fala, kwa nini unazuia wanafunzi wa kike wenye mimba wasiende shule wakiwa na mimba zao? Kama si ufala ni nini? Haujui kuwa huko ni kukiuka haki za watoto?'
Au utakuta mtu anamkosoa mkuu wa nchi kwa kuanza kwa kumkejeli na kumwita uchwara na majina mengine ya ajabu ajabu. Mtu unakuta anaenda msikitini na kuwahamasisha waislamu waifanyie vurugu serikali iliyowekwa madarakani kwa njia za kidemokrasia.
Hivyo serikali ya awamu ya tano pia inawanyoosha hawa wote wanaotumia vibaya uhuru wao huo wa kujieleza. Lazima sheria, kanuni na taratibu za kujieleza zizingatiwe.
Hata huko ndani ya bunge ambako wabunge wanakuwa na uhuru mpana zaidi wa kujieleza (express themselves) bado hauko unlimited, unamipaka yake iliyowekwa na kanuni za bunge. Huku mitaani uhuru huo ni finyu zaidi ukiulinganisha na ule walionao wabunge wakiwa ndani ya bunge. Hata huko Marekani ambako wewe mrembo wetu uko, uhuru huo wa kujieleza una mipaka yake, tena ni finyu kuliko ya kwetu. Wewe jaribu kuitisha vijivyombo vya habari vyenye kiwango kama cha Ayo TV halafu umuambia Trump kwamba ni fala, lofa, uchwara, mshenzi na kuwataka waislamu wamshughulikie kwani anawabagua; lazima cha moto utakipata immediately.
Wanachotupita Wamerekanam ni kuwa wao wanaijua mipaka yao ya freedom of expression kwa mjibu wa sheria zao na wanaizingatia, hivyo ni mara chake kujikuta ndani ya mikono ya sheria. Tatizo la nchi letu bado tuna mimbulula wengi wasiojua mipaka ya uhuru wao wa kujieleza. Wanafikiri hauna mipaka na hivyo kujiropokea tu. Na wanasiasa wa upinzani ndiyo wanaongoza kwenye kundi hili na wanawafundisha wafuasi wao. Hawa ndiyo wanaonyooshwa kwani bila kufanya hivyo amani ya nchi yetu itapotea ndani ya muda mfupi. Lazima watanyooka.