Mrema ataka CHADEMA wasibembelezwe

Mrema ataka CHADEMA wasibembelezwe

huyu mzee anatudhalilisha sana wachaga aisee maana huyu inamsumbua njaa atanyenyekea mpaka kero khaa
 
View attachment 386824

Mwenyekiti wa bodi ya Parole, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labor Party (TLP) Augustine Mrema ameunyooshea kidole mpango wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wa kufanya maandamano nchi mzima Septemba 1,kupitia Operesheni waliyoipa jina la UKUTA.

Akizungumza muda mfupi baada ya Msajili wa vyama vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi kutangaza kuvialika vyama vya siasa kwenye Baraza la vyama vya siasa kwa lengo la kufanya mazungumzo kuhusu hali ya kisiasa nchini, Mrema amekosoa mpango huo akidai umelenga kuwabembeleza Chadema.

Chanzo 😀ar24
Na yeye ajitahidi apakatwe basi kama anaona CDM wanapendelewa!
 
Mzee yupo sawa
Hawa si wakubembereza
Watavimba vichwa hawa,
Sikio halizidi kichwa
Kwanini wabembelezwe!!!


Hatushangai, utakapokuwa na motojuu, a.k.a Akili yenye akili utaelewa, kwa sasa unasumbuliwa na mihemuko ya chini, below belt!
 
Huyu mzee kinyonga kwelikweli, alipompa siku 7 Makonda azuie bodaboda katikati ya jiji alitoa sababu kuwa hataki kuona watu wanaingia jela kwa wingi halafu yeye apate kazi kuubwa kukagua mienendo na kupendekeza waachiwe. Leo badala ya kupongeza uamuzi wa jaji kuzuia watu kwenda jela yeye anapinga. Akili za kenge hizi kukimbia manyunyu kwenda kujificha mtoni.
 
huyo mzee ilitakiwa astaafu tuu akatulie kijijini huko hizi kazi za kupeana na mtu uwezo wa kufikiri umefika mwisho hakuna jipya la maana atakalosema kila kukicha ni matamko ya ovyo ovyo tuu.
 
Huyu mzee akiwa amalala utadhani kafa sura yake ilivyo sasa.
Halafu anaongea.!!
 
Mrema naye bwana. Anataka awe mashuhuri kuliko uwezo wa nafasi aliopewa.
Wanashindana kwa matamko ya mwendokasi.
 
Mrema, mwenyekiti wa TLP, unajiaibisha. Interview ya Parole hukufanya, umebebwa tu, TLP imekufia mkononi, kwani unataka kuanzisha chama cha kisiasa cha Parole Mrema party?. Pumzika, siasa imekutupa mkono huna mvuto kama zamani.
Tumia muda wako kuongea na wafungwa
 
View attachment 386824

Mwenyekiti wa bodi ya Parole, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labor Party (TLP) Augustine Mrema ameunyooshea kidole mpango wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wa kufanya maandamano nchi mzima Septemba 1,kupitia Operesheni waliyoipa jina la UKUTA.

Akizungumza muda mfupi baada ya Msajili wa vyama vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi kutangaza kuvialika vyama vya siasa kwenye Baraza la vyama vya siasa kwa lengo la kufanya mazungumzo kuhusu hali ya kisiasa nchini, Mrema amekosoa mpango huo akidai umelenga kuwabembeleza Chadema.

Chanzo 😀ar24
Anataka kulipa fadhila....
 
Mrema tumsamehe tu nawaombeni nyote wana JF, huyu mzee wetu inabidi aibukeibuke kila fursa inapojitokeza ili asimalizike kbs hata ktk magazeti ya udaku maana ktk medani za siasa hayupo tena.
 
Back
Top Bottom