Mala zote hua hawafiki mbali hurudi na kukuta milango imefungwa,mimi nilisomesha mwanamke from diploma to degree nikiwa nae Ndani hapa jijini Mwanza,alipomaliza na kuajiliwa na serekali ndipo kivumbi kilipoanza,siwezi kuyasema yote hapa ila ilikua ni wakati mgumu hujawahi ona,na mwisho wa siku mimi nikiwa kazini nje ya jiji,niliporudi ijumaa kwa ajili ya week end nyumbani nilikuta kuna nguo zangu tu ndani ktk nyumba ya kupanga,kama mwanaume amini usiamini sikuumia nikajua huyu ni MUNGU kaniepusha na mengi,nikabeba zile begi na kuishia Hotel then nikasonga mbele na maisha,sasa ni miaka mitatu na nimeoa mwanamke mzuri kwangu kuliko alivyokua,hapa nina taklibani msg zake hazipungui hamsini akijutia maamuzi yake na anapita kwa marafiki zangu akiwasihi waniombe nimsamehe.kwa kipindi nisichokua nae nilipooa mke mwingine ktk miaka miwili sasa njia zangu zimekua za baraka hata kutoka kwenye maisha ya kupanga na kua na nyumba yangu na maendeleo mengine,wanaume wote wenye hekima hupenda wanawake watulivu na wasikivu,ndipo baraka za MUNGU huingia ndani ya nyumba,wanawake wameharibiwa na ile hali ya kujiona wamesoma na wanaweza kuendesha maisha zaidi hata ya baadhi ya wanaume,lakini mwanaume atabaki kua mwanaume,kamwe uumbaji wa MUNGU hautabadilika,nikutoe hofu kijana mtoa mada usibabaike muache aende zake na siku akirudi kamwe usimkaribishe,waweza karibisha kifo.wanawake kwa sasa ni wengi kama mchanga,anaemchezea mwanaume hajitambui tu,hua hawaoni mbele wako kama watoto.