Mramba anasafishwa?


You are absolutely correct 100%.He was been by Reginald Salakana wa CHADEMA.
 

You are absolutely correct 100%.He lost to Reginald Salakana wa CHADEMA.
 
 
 
wandugu,

..all politics is LOCAL. kinachoendelea hapa ni kwamba: ama wananchi hawana habari na vita dhidi ya mafisadi, au wana mambo yao LOCAL ambayo kwa busara zao wanaona yana umuhimu kuliko vita dhidi ya ufisadi.

..halafu sijui kwanini wengine tumefikia mpaka mahala tukaanza kuwabeza wananchi wa Rombo, na uwezo wao wa kuchambua masuala ya kisiasa, na maslahi yao binafsi.

..hawa wananchi tunaowabeza na kuwalaani hapa JF ndiyo hao hao ambao mwaka 95walimpiga chini Basil Mramba na kuchagua mgombea wa CHADEMA -- chama kipenzi hapa JF.

..kwa taarifa tu 1995 wakati wana Rombo wanapigia kura Chadema, hata shujaa wetu Dr.Wilbroad Slaa alikuwa akibeba kadi ya CCM!!!

..sasa ni wangapi hapa walipigia kura wapinzani au chadema mwaka 95, 2000, au 2005?

..kuna baadhi ya wana JF ambao wametembea na kuishi ASIA,ULAYA, na MAREKANI, lakini bado wanabeba kadi ya chama cha kifisadi kama CCM. watu kama hao wana haki gani ya kujiona wako enlightened kisiasa kuliko wananchi wavuja jasho wa Rombo ambao wana historia ya kutorudisha incumbents bungeni na kupigia kura upinzani?

..tutafute issues ambazo ni local na ziwasilishwe kwa wananchi na wasemaji ambao wanaheshimika na jamii husika. hata kama ni masuala ya ufisadi tujaribu kuwaelimisha wananchi jinsi yanavyoathiri maisha yao ya kila siku.

..WANANCHI WA ROMBO WALIPIGIA KURA WAPINZANI 1995. HAWA SIYO WAPUMBAVU KAMA WENGI MNAVYOWAANDIKA HAPA. KAZI YA KUWASHAWISHI KUCHAGUA UPINZANI TENA INAWEZA KUWA RAHISI KULIKO MAENEO YANAYOCHAGUA CCM SIKU ZOTE.
 
Last edited:
Nafikiri kuwa kuna wakati Mafisadi wanaamua kutumia media kuudanganya umma, na wakati huohuo kufikisha ujume wao kwa wananchi kuwa Mzee anakuja. Kama taarifa ilivyo haina uhakika kuwa ni wakina nani watampokea kwa kishindo, wengi watakuwa ni Mafisadi wenzake lakini pia kuwalaghai wananchi ili wafike ndio maana neno KISHINDO limetumika.
Wananchi wa Tanzania wanahitaji bado kueleweshwa, kuwa na upeo na viongozi wao nadhani kama mwananchi wa kawaida akielewa kiongozi bora ni nani; basi maendeleo yatapatikana na sio kiongozi bora kujielewa yeye ni kiongozi bora.
 
Mkuu Joka Kuu,

Ubarikiwe sana na maneno yako.Ndiyo maana nikasema mafisadi wamejipokea na kujipongeza wenyewe.Waache kuwasingizia au kuwaingiza mkenge wananchi wa Rombo
 


Alirudi tena CCM mwaka 2008...huenda anajiandaa kugombea tena 2010.




Mkuu,

Upo sahihi kabisa ni Mwaka 2000.

Ahsante
 


...kuwa mke wa mtu siku hizi sio tiketi ya kutokuwa na msela.......tena siku hizi wake za vigogo wakipata wasela wanakolea sana ....wanasema kila kitu...just kwa kuwa wanakuwa so deep na yule wanayempata kwani hawezi kuwa wazi kupata mwingine kama anavyotaka....

..mwanamke msela kama sofia ...anaweza asiwe na mume lakini pia anakuwa huru kuchukuliwa na mwanamume yeyote pale anapojisikia....sometimes one night stand man....sasa sidhani kama anaweza kuwa wazi namna hiyo...kwani hakuna enough intimancy...tena mara nyingi wanawake wengi maarufu siku hizi hupendelea wanaume wasela wasiokuwa na uelewa mkubwa...wa mambo zaidi ya "yale"...kwa kuofia akichukuliwa na mjanja anaweza kumuuza...so anakuwa falafala tu wala hutaamini...kama anazungusha mzigo wa ajabu...

pia kumbuka CONDY RICE naye ni single lady.....na katika list ya alio wa date yumo....waziri wa mambo ya nje wa canada,italia,and fomer uk foregn.....but pia wanajuwa wazi kuweka mstari kamili kati ya chumbani na kwenye gorvernment business.........

...ni mwanamke mjinga mwennye nafasi serikalini au kokote ambaye hatamshangaa mwanamume aliyemdate anaaza kumuuliza mambo ya kazini kwake...wakati kazi waliyoifuata walipo inajulikana.....mtu akiaaza kukuuliza mambo ya kazini sehemu kama hizo lazima atakuwa ametumwa anataka kukufanya "samson"

so .....lets put aside bedroom affairs au kuolewa na kutokuolewa au kuoa na kutoaooa kwenye kazi!!!!...unless otherwise!
 

The great question that has never been answered and which I have not yet been able to answer, despite my thirty years of research into the 'Amani na Utulivu' soul, is 'WHAT IS WRONG WITH US TANZANIANS?'
 
Mramba, Mgonja, Yona wote toka mkoa wa Kilimanjaro
 
Same as wanaowatetea..... talk abt birds of the same feather flock together....
 
Mramba, Mgonja, Yona wote toka mkoa wa Kilimanjaro


Ufisadi hauna kwao ndugu....wengine muda wao tu haujafika.....mkubwa wao kwani katokea wapi? subiri kidogo...
 

Wakati wa vita vya wahujumu uchumi tulikuwa na majemedari wa kweli waliokuwa wanauchukia ufisadi... mtu ungeanzia wapi?? Tatizo la sasa ni kuwa serikali haiuchukii kweli ufisadi. Ni usanii tu unatumika. Kesi za kina hao Mramba ni kupoteza lengo tu lakini mafisadi wa kweli bado hawajaguswa. Kina Mramba na mafisadi wengine wana skendo ambazo kama Serikali ingetaka kufanya kweli wangeozea jela...
 
WHAT IS WRONG WITH US TANZANIANS?'

- Mkuu Hauxtable ubarikiwe na hapa tupo ukurasa mmoja. I mean umesikia leo huko Chicago, yaani yule Governor wao bado hajawa indicted, anatuhumiwa tu na kesi bado lakini tayari wamemu-impeach,

- Sisi kiongozi aliyetoka rumande na kesi bado inaendelea anapokewa na kushangiliwa na wananchi aliowaibia na kuna mpaka wakulu humu JF wanaodai kuwa eti ni sawa sawa!, wooi! mfumwa mrungu!
 

FMES,

..nilichopinga mimi ni ile hali ya kuwabeza na kuwakejeli wananchi wa Rombo. unajua ulikwenda mbali mpaka kuukusanya mkoa mzima wa Kilimanjaro, na kuhoji elimu na uelewa wa wananchi wake.

..cha msingi hapa ni kuwa karibu na kuwaelimisha wananchi wa Rombo kuhusu ufisadi na athari zake. tena tunahitaji kuwa na subira na uvumilivu kwelikweli ukizingatia kwamba Mramba kama mbunge alikuwa karibu sana na wananchi wake.

NB:

..hivi ni kwanini CCM haijawafuta uanachama Basil Mramba na Daniel Yona?
 
Jokakuu na mimi naanza kuhoji uelewa wa wananchi wa kilimanjaro iam frm thr lkn siko kama wale........
 
1.
..nilichopinga mimi ni ile hali ya kuwabeza na kuwakejeli wananchi wa Rombo. unajua ulikwenda mbali mpaka kuukusanya mkoa mzima wa Kilimanjaro, na kuhoji elimu na uelewa wa wananchi wake.

- Mkuu Joka Kuu unajua huwa sipendi kuandikia mate na wino ukiwepo, hivi unaweza linganisha hao wananchi wa Rombo na wananchi wa Chunya? au wa huko Mbeya? Sasa unafikiri tofauti yao ni nini kama sio elimu? Huko Chunya wao knowing what they know already kuhusu ujinga wa viongozi wetu walimsalimia kwa mawe tena mkuu wa kaya, sasa imagine mbunge wa huko Chunya aibe, si watamla nyama hao? Ebo! hao Warombo, wamelala usingizi period ingawa ungetegemea wawe wameamka kuliko wa Chunya, na Kilimanjaro kuwa na shule nyingi sio kuwa na elimu, hivi na Kisumo si anatoka huko huko Kilimanjaro?

- Majuzi wanacnhi wa Mbeya wamemuonya rais kutompeleka Makamba kwenye uchaguzi wao, na kweli hakuenda sasa utalinganisha hawa Mbeya na huko Rombo wanakompokea fisadi? Kweli huoni kuwa hapa wananchi wa Mbeya wana eilimu kubwa sana hasa ya siasa ya taifa letu!


2.
..cha msingi hapa ni kuwa karibu na kuwaelimisha wananchi wa Rombo kuhusu ufisadi na athari zake. tena tunahitaji kuwa na subira na uvumilivu kwelikweli ukizingatia kwamba Mramba kama mbunge alikuwa karibu sana na wananchi wake.

- Mkuu vipi? Eti kuna mbongo anayehitaji kuelimishwa kuhusu ufisadi wa viongozi wetu? Sasa hawa wa Chunya wameelimishwa na nani? Mramba hajawahi kuwa karibu na wananchi wa jimbo lake, ni majuzi tu akiwa waziri wa Mkapa, ndio ameiba sana na kuanza kuwagawia huko jimboni kwake na kumnunua Kisumo. Hivi Salakana si alimpiga bao huyu mtu wa karibu sana na wananchi wa jimbo lake, au?
 
Huu ni ugonjwa mbaya sana unaotukabili wa Tanzania. It seems to me kwamba Mtanzania anakuheshimu tu pale unapomnyanyasa na kumfedhehesha. The more money you steal from us the more we respect you!! Unbelievable!!!!! Najua watu watasema ni njaa but this is BEYOND njaa kusema kweli...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…