Mradi wa Bagamoyo ulitakiwa uanze kabla ya Bwawa la Nyerere, Rais Samia umetuheshimisha

JPM alisema aliyoyasema baada ya kuangalia huo mkataba wa bandari ya Bagamoyo

Sasa nyinyi mbona mnaongea ongea tu wekeni hapa huo mkataba ambao JPM alikataa kuusaini ndio mtuambie kuwa aliyoyasema yalikuwa ya uongo hayapo katika mkataba

Sent using Jamii Forums mobile app

Ni kosa la nani kuficha mikataba? Na isitoshe nani alikuwa anamuamini dhalimu, zaidi ya wajinga na wachumia tumbo?
 
NILIAMINI NIKO SAHIHI, LEO MAMA UMETUSHINDIA

Na Yericko Nyerere

Hureeeeee vita vyetu kwa maslahi ya Taifa tumeshinda! Asante Rais Mama Samia suluhu Hassan, nilimpinga Magufuli alipositisha mradi huu kwa hoja dhaifudhaifu na za uongo wa kiwango cha rami. Nikampinga baada ya kufariki baada ya wapambe wake kuendelea kukomaza shingo.

Now naweza kusema Mama umetuheshimisha sisi wataalamu tuliofanya kazi kubwa kujenga hoja na kushauri umuhimu wa mradi huu kwa maslahi ya Taifa kwa uchumi wa Reli ya SGR.

Naomba niwarejeshe nyuma miaka miwili iliyopita 22 December 2019 nilipoandika Makala nikipinga hotuba ya Rais Magufuli akikataa kuendelea na ujenzi wa Mradi ya Bandari ya Bagamoyo, nilipinga hoja alizozijenga Rais ili kuhalalisha katazo lake juu ya mradi husika.

Nilieleza wazi kwamba, Kuna mambo katika nchi yanahitaji uchunguzi kubaini pengine kuna hujuma katika taifa, hii inatokana na michakato mingi muhimu ya kichumi na kijamii imekuwa ikiishia njiani na kuliacha taifa katika hasara kubwa. Hii ni hujuma inahitaji mwarobaini kulitibu.

Mifano ya michakato ambayo kwamiaka mingi imeikuwa ikiishia njiani ni kama vile sekta ya nishati ambapo uzalishaji wa umeme limekuwa jambo linalotumiwa kama mchakato wakuzuka na kufa kwa miaka mingi sana tangu mwaka 1994 ilipokuja kitu kinaitwa umeme wa dharula kuokoa taifa (IPTL), ikafata michakato mingi yenye kuumiza taifa na haikufanikiwa hadi tukafika kuchimba Gesi mtwara tukapoteza mabilioni, gesi hadi Kinyerezi, kufumba na kufumbua mradi umetelekezwa sasa tunaimba mradi wa Bonde la Rufiji. Twende tuendelee..

Serikali ya awamu ya nne ilianzisha mradi wa kimkakati kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara duniani, mradi huu ilikuwa ni kujenga bandari ya Bagamoyo kwa ubia kati ya China na Omani wenye thamani ya dola bilioni 10, Serikali ya Tanzania katika mradi huu ilikuwa haiweki pesa yoyote isipokuwa ardhi na raslimali zingine, huku Uchina na Omani wakiweka mtaji na utaalamu.

Kwamjibu wa mapendekezo ya mkataba wa awali wa mradi huo, ni kwamba kungeundwa chombo maalumu cha nchi zote tatu ambacho kingekusanya mapato ya mradi huu na kusimamia gawio la pande zote, hii inamaana kwamba TRA ya Tanzania isingekuwa na haki ya kukusanya mapato moja kwa moja kutoka katika mradi badala yake ingekusanya gawio toka kwa chombo cha wabia kinachokusanya mapato ya mradi wa nchi zote tatu.

Huu ni moja ya mradi ambo kimsingi ulikuwa umeitangazia dunia vita vya kiuchumi toka kwa washindani wetu ambao ni nchi jirani na zinazotuzunguka. Kwakuwa Afrika yote ingepokelea bidhaa zake toka ulimwenguni hadi Bagamoyo, sawa na ilivyo Dubai ambayo ndio mlango wa Afrika kupokelea bidhaa zake.

Afrika inaingiza bidhaa toka Uchina kwa 88.8% na kiwango cha 98% ya bidhaa hizo zinapita Dubai. Hivyo kujengwa kwa Bandari ya Bagamoyo kungefunga nyia ya Dubai na bidhaa zote za Afrika kutoka China kupita Bagamoyo. Hii inamaana kwamba uchumi wa Dubai na Marekani ambayo ndio mdau mkuu ungemegwa. Mradi huu ulikuwa ndio msingi halisi wa kuanzisha mradi wa reli ya kisasa ya SGR, bila Bandari itakayozalisha mizigo kwa wingi SGR itakuwa ni kwakubeba abiria tu badala ya mizigo.

Serikali ya awamu ya tano katika hali ya kustaajabisha imeutupilia mbali mradi huo kwakutoa sababu ambazo hazina nguvu na zingine za kushangaza sana, mimi naitafsiri kama ni hujuma kwa taifa, izingatiwe kuwa tayari taifa lilishaingia gharama kubwa kuanzia kwenye upembuzi yakinifu, na kusaini mikataba ya awali. Kitendo cha kusitisha katika hatua hii ni kulitia hasara taifa. Moja ya hoja zilizotolewa na rais kama sababu ni kwamba masharti ya wabia nikuwa TRA hairuhusiwi kukusanya mapato, hoja hii ya Rais alikuwa sahihi lakini bahati mbaya alishindwa kufafanua wazi sababu za TRA kutokuwa miusanya mapato ya ubia. Pengine hili Rais alidanganywa.

Pili rais alisema kuwa masharti ya wabia nikuwa Tanzania hairuhusiwi kuendeleza bandari zake zingine. Hoja hii nayo inautata mwingi sana, Bandari zingine zote ziko kwaajili ya ndani, na mradi huu ulikuwa kwa shughuli za kimataifa. Sasa hoja ya kuwa tusikarabati bandari zetu zilizopo ni hoja isiyo na mashiko, Hili inawezekana kabisa Rais hakuambiwa ukweli.

Hoja ya Tatu aliyoitumia Rais Magufuli kukataa mradi ule, ilikuwa kwamba, wabia wanataka wapewe umiliki wa ardhi kwa miaka 99. Hili si la mwekezaji bali la sheria zetu ambazo zinatoa uwekezaji katika ardhi kwa miaka 33 hadi 99. Sasa hoja hii haiwezi kuwa kwa wabia wawili tu kati ya watatu ikiwemo Tanzania yenyewe. Hili nalo kuna uwezekano watu waliamua kumpotosha rais wetu.

Chakusikitisha kwa nchi yangu, Katikati ya mvutano wetu na wabia hadi Rais Magufuli kusitisha mradi, Rais wa Msumbiji Philip Nyusi kwakutumia majasusi wake waliotanda kila pembe ya Afrika na kwingineko, amefanya mageuzi makubwa, amechukua wazo lilelile ambalo limekataliwa Dar es Salaam na wajuvi, amekwenda kulisimika katika Bandari ya Nacala kwakuingia ubia na Wachina kwa Dola bilioni 5 za Kimarekani, hii ni Bandari inayotarajiwa kuwa lango kuu la kiuchumi Afrika.

Wakati hili halijapoa, Mwaka 2017 tu juzi Tanzania tulipowazuia wazungu wasisafirishe madini ghafi na makinikia yao, tuliimba nyimbo kwamba Tanzania itajenga vinu vya kuchenjulia madini hapahapa, na nyimbo ziliimbwa kisiasa zikaitikiwa kishabiki kwa beti za kinafiki kwelikweli. Leo nyimbo haziimbwi, hakuna anayejua kama viwanda vimeshajengwa au laa na hakuna anayehoji hilo kwakuwa ukihojihoji tu basi ukinusurika sana utaenda mochwari au Ubelgiji, tulishazoe vimbunga kwamba vitavuma na kutulia.

Lakini huku sisi tukiwa tumebadili nyimbo sasa tunaimba nyimbo za Standard Gauge nk, Rwanda kwakutumia majasusi wao waliotanda kila pembe ya Dunia, imelichukua wazo lilelile la Tanzania imejenga vinu vya kuchenjulia madini na inatarajiwa kwamba hadi 2024 Rwanda iwe ndio nchi ya kwanza barani Afrika inayosafirisha madini kwa wingi nje ya Afrika. Kumbuka na elewa Rwanda sio mzalishaji wa Dhabu, Almasi wala chochote kiitwacho madini isipokuwa kwenye kilimo cha chai na kahawa huko. Hivyo anategemea viwanda vyake vipokee madini ghafi toka Tanzania, Kongo, Zambia akusanye kodi yake na kugonga muhuri wa madini unaotambulisha kuwa ni madini toka Rwanda nk. Sisi tumelala. Siasa inanguvu bana.

Kwa maoni yangu ninafiki kuna tatizo kubwa kwenye eneo la Ujasusi katika nchi yetu, hasa ujasusi wa Kiuchumi, na hili ndilo lilikuwa msingi wa mimi kuandika Kitabu changu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi. Michakato mingi ya kiuchumi katika nchi hii imekuwa haina mafaa ama inaliacha taifa katika makovu makubwa yasiyozibika. Hii inazaa uhalali wa kuhitaji mageuzi makubwa katika Idara ya Ujasusi nchini kuanzia kwenye ideology, sheria, misingi, kanuni, na mambo anuai ndani ya idara ya ujasusi nchini.

Ujasusi kwa nchi zilizoendelea kama China, Israel, Urusi na Marekani, unafanywa na watu ambao ni smart na wanajengwa kuwa smart ili kuweza kumudu ugumu wa kazi hiyo na kuifanya kazi hiyo kwa mafanikio makubwa. Majasusi katika nchi hizo hawapewi kazi kwasababu ya ujomba ujomba na kujuana.
Ni kweli asilimia kubwa ya information's zenye thamani katika kazi ya ujasusi huwa zinaletwa na "human intelligence" badala ya magazeti, TV na source nyingine za habari.

Kwa maana hiyo basi ni lazima kuwe na watu competent ambao wana uwezo wa kukusanya habari za kijasusi ili tuweze kupata information's za maana na kujenga uwezo wa kuzifanyia kazi informations hizo. Imagine wakati ule wa vita baridi jinsi Directorate 16 ya KGB ilivyoweza kufanya kazi ya kununua sensitive navy information za USA na kuweza kutengeneza balance ya navy fleet bila USA kugundua kwa miaka 17 kupitia kwa Johny Walker junior!

Tanzania kwenye balozi zetu kuna majasusi. Lakini ni majasusi wa aina gani? Wale wa kujua kuongea kifaransa na kireno na lugha nyingine za mataifa ya nje bila upeo wowote wa Technologia? Kama kuna sehemu tunakosea basi ndio hapo. Majasusi wengi wa Tanzania au tunaoambiwa kuwa ni watu wa system wengi katika tafsiri ya kijasusi ni "informers". Ujasusu kama ujasusi hapa Tanzania ni kama hakuna. Usalama wa Taifa au TISS/UWT msingi wao uliounda chombo hiki ni "power defensive", yaani wajibu mkubwa unaelekezwa kwenye kumonitor mwelekeo wa kisiasa Tanzania hasa kuwadhibiti oppositions na elements zote za upinzani na assasinations za elements zozote zinazoonekana kuwa against na himaya ya CCM.

Idara ya Usalama wa Taifa hii tuliyonayo leo ilianzishwa na CCM 1997 kutoka katika muundo wa kijamaa wa chama kimoja, hii ni baada ya kuanzishwa mfumo wa vyama vingi, kwa hiyo bado unaiserve CCM kwanza kisha Taifa linatafsiriwa salama kupitia matokeo ya uimara wa ccm, kama yakifanyika mageuzi ya kimuundo, kisheria, kikanuni na kisera, uimara wa Taifa hautatafsiriwa kupitia uimara wa ccm madarakani, na mambo mengi tunayolalamikia sasa juu ya taifa hayatakuwepo tena. In simple words, taswira kubwa inayoonekana yauhakika ni kazi yao ya kulinda viongozi, kusafiri na viongozi na kuilinda CCM.

Nje ya mambo ya Ujasusi wa Kiuchumi ambao mimi ndio ninaoupigania siku zote uongoze nchi, Naweza kusema Tanzania tuko vizuri katika Ujasusi wa kidola kuliko nchi yoyote pengine Afrika nzima, Hili limefanya kuimeza idara na kuonekana siasa ambazo ndio zinabeba taswira kubwa ya ubora ama udhaifu wa ujasusi Tanzania, Eneo la Ujasusi wa Kidola Tanzania kuna vitengo vya wachapakazi hasa kiko jeshini.., kitengo cha ujasusi ambacho kilikuwa kiko free from politics party ni CMI (central military intelligence). Lakini bahati mbaya muundo na aina ya uongozi wa Magufuli ulikiingiza katika siasa pale kilipofanywa kuwa decision maker wa nchi, lakini upande wa foreign assets ndio wazuri sana wako bize kukusanya taarifa hatarishi dhidi ya nchi...

Kwahatua hii naomba niseme wazi, Mradi wa Bagamoyo ulitakiwa uanze kabla ya Bwawa la Nyerere kule Rufiji ama ungeanza kabla ya SGR, Now sasa nasema taifa linakwenda kushinda vita vya kiuchumi afrika mashariki na kati.

Kuanzia sasa atakayempinga mama nitamloga nitamloga

Kwa undani zaidi Soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi.
View attachment 1830718
Mkataba umeuona? Lengo lako ni kuuza kitabu feki cha kile unachokiita ujasusi wakati hata tahasusi ya ujasusi wenyewe huelewi

Weka mktaba hapa kila mwenyewe akili kubwa apambanue ukweli ni upi sio blah blah za mwanasiasa ambaye lengo lake ni kujihakikishia himaya.
 
Kwahiyo ndio umeanza kujitetea kiivi kwani bandari ni secret formula kama Coca-Cola au
Project ni kubwa mno ile unafikiri ni karatasi moja? Kuna makampuni na taasisi nyingi sana zimelipwa pesa nyingi zimefanya kazi kufanya upembuzi wa mradi kwa muda mrefu wamewasilisha proposal alafu waitoe tu kwako wewe alafu washindani waone weakness za mradi waje na alternative version ya proporsal waokoe hela ya kufanya upembuzi wao?
Eti secret formula, kumbe hujui?
 
Project ni kubwa mno ile unafikiri ni karatasi moja? Kuna makampuni na taasisi nyingi sana zimelipwa pesa nyingi zimefanya kazi kufanya upembuzi wa mradi kwa muda mrefu wamewasilisha proposal alafu waitoe tu kwako wewe alafu washindani waone weakness za mradi waje na alternative version ya proporsal waokoe hela ya kufanya upembuzi wao?
Haya tetea nchi yako iki inaibiwa mradi wenyewe sio wa watanzania investor ni Oman na China yani watanzania wataona kama pambo
 
Haya tetea nchi yako iki inaibiwa mradi wenyewe sio wa watanzania investor ni Oman na China yani watanzania wataona kama pambo
Unajiwazia wewe huoni faida yoyote kwa watoto wa vijukuu vyako kabisa? Au unazani dubai iliibuka tu kama uyoga? Nchi zilizoendelea wanaofaidi matunda hawapo ila walijitoa kwa vizazi vijavyo wewe unaona hasara kwakuwa unajipimia kwa umri wako.acha wajenge hata miaka 99 poa tu. Jamaa lilikua linaongea kwa sababu lilijua miaka 99 halitakua madarakani likapiga chini mradi shwaini kweli yani.
 
Unajiwazia wewe huoni faida yoyote kwa watoto wa vijukuu vyako kabisa? Au unazani dubai iliibuka tu kama uyoga? Nchi zilizoendelea wanaofaidi matunda hawapo ila walijitoa kwa vizazi vijavyo wewe unaona hasara kwakuwa unajipimia kwa umri wako.acha wajenge hata miaka 99 poa tu. Jamaa lilikua linaongea kwa sababu lilijua miaka 99 halitakua madarakani likapiga chini mradi shwaini kweli yani.
Faidi ipi sasa wewe MpK leo accacia umepata faida gani.. Shule 3 zilizojengwa karibu na mgodi.. Mali hiyo ingekuwa tumejenga wenyewe hata kwa pesa za mkopo ingekuwa na maana kinacho chosha zaidi hata ujuzi hutopati kupitia ujenzi huo.. Je in 10 year tunaweza jenga kama hiyo ya bagamoyo pale Tanga kutumia watu wetu. Je kwanini pesa hizo zosingeendeleza bandari ya Tanga kwanini kuwe na bandari za Dar na Bagamoyo karibu swali lengine bandari ya Dar kazi yake itakuwa ni nini. Tanga ndio ingekuwa inafaa zaidi kwasababu ni karibu na mikoa mingi ya kaskazi na kati.
Mkiwa mnashabiki kitu naomba muwe subjective na objective simultaneously sio kuwa na shauku na hisia tuu.
 
Lowasa wakati wa kampeni kupitia UKAWA alisema akishinda urais, mkataba wa hiyo badandari atauvunja na Yeriko alishangilia kauli hiyo ya Lowasa
Labda alikua bado hajauelewa ujasusi wa kidola na kiuchumi unavyofanyika kivitendo tofaut na nadharia anazozijua
 
Kwenye maslahi ya taifa hakuna anaemfikia jiwe....na hapo naamini kwenye hili unamaono madogo..ni suala la muda tu, hata gesi ya mtwara alisikitika sana si yetu tena
 
NILIAMINI NIKO SAHIHI, LEO MAMA UMETUSHINDIA

Na Yericko Nyerere

Hureeeeee vita vyetu kwa maslahi ya Taifa tumeshinda! Asante Rais Mama Samia suluhu Hassan, nilimpinga Magufuli alipositisha mradi huu kwa hoja dhaifudhaifu na za uongo wa kiwango cha rami. Nikampinga baada ya kufariki baada ya wapambe wake kuendelea kukomaza shingo.

Now naweza kusema Mama umetuheshimisha sisi wataalamu tuliofanya kazi kubwa kujenga hoja na kushauri umuhimu wa mradi huu kwa maslahi ya Taifa kwa uchumi wa Reli ya SGR.

Naomba niwarejeshe nyuma miaka miwili iliyopita 22 December 2019 nilipoandika Makala nikipinga hotuba ya Rais Magufuli akikataa kuendelea na ujenzi wa Mradi ya Bandari ya Bagamoyo, nilipinga hoja alizozijenga Rais ili kuhalalisha katazo lake juu ya mradi husika.

Nilieleza wazi kwamba, Kuna mambo katika nchi yanahitaji uchunguzi kubaini pengine kuna hujuma katika taifa, hii inatokana na michakato mingi muhimu ya kichumi na kijamii imekuwa ikiishia njiani na kuliacha taifa katika hasara kubwa. Hii ni hujuma inahitaji mwarobaini kulitibu.

Mifano ya michakato ambayo kwamiaka mingi imeikuwa ikiishia njiani ni kama vile sekta ya nishati ambapo uzalishaji wa umeme limekuwa jambo linalotumiwa kama mchakato wakuzuka na kufa kwa miaka mingi sana tangu mwaka 1994 ilipokuja kitu kinaitwa umeme wa dharula kuokoa taifa (IPTL), ikafata michakato mingi yenye kuumiza taifa na haikufanikiwa hadi tukafika kuchimba Gesi mtwara tukapoteza mabilioni, gesi hadi Kinyerezi, kufumba na kufumbua mradi umetelekezwa sasa tunaimba mradi wa Bonde la Rufiji. Twende tuendelee..

Serikali ya awamu ya nne ilianzisha mradi wa kimkakati kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara duniani, mradi huu ilikuwa ni kujenga bandari ya Bagamoyo kwa ubia kati ya China na Omani wenye thamani ya dola bilioni 10, Serikali ya Tanzania katika mradi huu ilikuwa haiweki pesa yoyote isipokuwa ardhi na raslimali zingine, huku Uchina na Omani wakiweka mtaji na utaalamu.

Kwamjibu wa mapendekezo ya mkataba wa awali wa mradi huo, ni kwamba kungeundwa chombo maalumu cha nchi zote tatu ambacho kingekusanya mapato ya mradi huu na kusimamia gawio la pande zote, hii inamaana kwamba TRA ya Tanzania isingekuwa na haki ya kukusanya mapato moja kwa moja kutoka katika mradi badala yake ingekusanya gawio toka kwa chombo cha wabia kinachokusanya mapato ya mradi wa nchi zote tatu.

Huu ni moja ya mradi ambo kimsingi ulikuwa umeitangazia dunia vita vya kiuchumi toka kwa washindani wetu ambao ni nchi jirani na zinazotuzunguka. Kwakuwa Afrika yote ingepokelea bidhaa zake toka ulimwenguni hadi Bagamoyo, sawa na ilivyo Dubai ambayo ndio mlango wa Afrika kupokelea bidhaa zake.

Afrika inaingiza bidhaa toka Uchina kwa 88.8% na kiwango cha 98% ya bidhaa hizo zinapita Dubai. Hivyo kujengwa kwa Bandari ya Bagamoyo kungefunga nyia ya Dubai na bidhaa zote za Afrika kutoka China kupita Bagamoyo. Hii inamaana kwamba uchumi wa Dubai na Marekani ambayo ndio mdau mkuu ungemegwa. Mradi huu ulikuwa ndio msingi halisi wa kuanzisha mradi wa reli ya kisasa ya SGR, bila Bandari itakayozalisha mizigo kwa wingi SGR itakuwa ni kwakubeba abiria tu badala ya mizigo.

Serikali ya awamu ya tano katika hali ya kustaajabisha imeutupilia mbali mradi huo kwakutoa sababu ambazo hazina nguvu na zingine za kushangaza sana, mimi naitafsiri kama ni hujuma kwa taifa, izingatiwe kuwa tayari taifa lilishaingia gharama kubwa kuanzia kwenye upembuzi yakinifu, na kusaini mikataba ya awali. Kitendo cha kusitisha katika hatua hii ni kulitia hasara taifa. Moja ya hoja zilizotolewa na rais kama sababu ni kwamba masharti ya wabia nikuwa TRA hairuhusiwi kukusanya mapato, hoja hii ya Rais alikuwa sahihi lakini bahati mbaya alishindwa kufafanua wazi sababu za TRA kutokuwa miusanya mapato ya ubia. Pengine hili Rais alidanganywa.

Pili rais alisema kuwa masharti ya wabia nikuwa Tanzania hairuhusiwi kuendeleza bandari zake zingine. Hoja hii nayo inautata mwingi sana, Bandari zingine zote ziko kwaajili ya ndani, na mradi huu ulikuwa kwa shughuli za kimataifa. Sasa hoja ya kuwa tusikarabati bandari zetu zilizopo ni hoja isiyo na mashiko, Hili inawezekana kabisa Rais hakuambiwa ukweli.

Hoja ya Tatu aliyoitumia Rais Magufuli kukataa mradi ule, ilikuwa kwamba, wabia wanataka wapewe umiliki wa ardhi kwa miaka 99. Hili si la mwekezaji bali la sheria zetu ambazo zinatoa uwekezaji katika ardhi kwa miaka 33 hadi 99. Sasa hoja hii haiwezi kuwa kwa wabia wawili tu kati ya watatu ikiwemo Tanzania yenyewe. Hili nalo kuna uwezekano watu waliamua kumpotosha rais wetu.

Chakusikitisha kwa nchi yangu, Katikati ya mvutano wetu na wabia hadi Rais Magufuli kusitisha mradi, Rais wa Msumbiji Philip Nyusi kwakutumia majasusi wake waliotanda kila pembe ya Afrika na kwingineko, amefanya mageuzi makubwa, amechukua wazo lilelile ambalo limekataliwa Dar es Salaam na wajuvi, amekwenda kulisimika katika Bandari ya Nacala kwakuingia ubia na Wachina kwa Dola bilioni 5 za Kimarekani, hii ni Bandari inayotarajiwa kuwa lango kuu la kiuchumi Afrika.

Wakati hili halijapoa, Mwaka 2017 tu juzi Tanzania tulipowazuia wazungu wasisafirishe madini ghafi na makinikia yao, tuliimba nyimbo kwamba Tanzania itajenga vinu vya kuchenjulia madini hapahapa, na nyimbo ziliimbwa kisiasa zikaitikiwa kishabiki kwa beti za kinafiki kwelikweli. Leo nyimbo haziimbwi, hakuna anayejua kama viwanda vimeshajengwa au laa na hakuna anayehoji hilo kwakuwa ukihojihoji tu basi ukinusurika sana utaenda mochwari au Ubelgiji, tulishazoe vimbunga kwamba vitavuma na kutulia.

Lakini huku sisi tukiwa tumebadili nyimbo sasa tunaimba nyimbo za Standard Gauge nk, Rwanda kwakutumia majasusi wao waliotanda kila pembe ya Dunia, imelichukua wazo lilelile la Tanzania imejenga vinu vya kuchenjulia madini na inatarajiwa kwamba hadi 2024 Rwanda iwe ndio nchi ya kwanza barani Afrika inayosafirisha madini kwa wingi nje ya Afrika. Kumbuka na elewa Rwanda sio mzalishaji wa Dhabu, Almasi wala chochote kiitwacho madini isipokuwa kwenye kilimo cha chai na kahawa huko. Hivyo anategemea viwanda vyake vipokee madini ghafi toka Tanzania, Kongo, Zambia akusanye kodi yake na kugonga muhuri wa madini unaotambulisha kuwa ni madini toka Rwanda nk. Sisi tumelala. Siasa inanguvu bana.

Kwa maoni yangu ninafiki kuna tatizo kubwa kwenye eneo la Ujasusi katika nchi yetu, hasa ujasusi wa Kiuchumi, na hili ndilo lilikuwa msingi wa mimi kuandika Kitabu changu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi. Michakato mingi ya kiuchumi katika nchi hii imekuwa haina mafaa ama inaliacha taifa katika makovu makubwa yasiyozibika. Hii inazaa uhalali wa kuhitaji mageuzi makubwa katika Idara ya Ujasusi nchini kuanzia kwenye ideology, sheria, misingi, kanuni, na mambo anuai ndani ya idara ya ujasusi nchini.

Ujasusi kwa nchi zilizoendelea kama China, Israel, Urusi na Marekani, unafanywa na watu ambao ni smart na wanajengwa kuwa smart ili kuweza kumudu ugumu wa kazi hiyo na kuifanya kazi hiyo kwa mafanikio makubwa. Majasusi katika nchi hizo hawapewi kazi kwasababu ya ujomba ujomba na kujuana.
Ni kweli asilimia kubwa ya information's zenye thamani katika kazi ya ujasusi huwa zinaletwa na "human intelligence" badala ya magazeti, TV na source nyingine za habari.

Kwa maana hiyo basi ni lazima kuwe na watu competent ambao wana uwezo wa kukusanya habari za kijasusi ili tuweze kupata information's za maana na kujenga uwezo wa kuzifanyia kazi informations hizo. Imagine wakati ule wa vita baridi jinsi Directorate 16 ya KGB ilivyoweza kufanya kazi ya kununua sensitive navy information za USA na kuweza kutengeneza balance ya navy fleet bila USA kugundua kwa miaka 17 kupitia kwa Johny Walker junior!

Tanzania kwenye balozi zetu kuna majasusi. Lakini ni majasusi wa aina gani? Wale wa kujua kuongea kifaransa na kireno na lugha nyingine za mataifa ya nje bila upeo wowote wa Technologia? Kama kuna sehemu tunakosea basi ndio hapo. Majasusi wengi wa Tanzania au tunaoambiwa kuwa ni watu wa system wengi katika tafsiri ya kijasusi ni "informers". Ujasusu kama ujasusi hapa Tanzania ni kama hakuna. Usalama wa Taifa au TISS/UWT msingi wao uliounda chombo hiki ni "power defensive", yaani wajibu mkubwa unaelekezwa kwenye kumonitor mwelekeo wa kisiasa Tanzania hasa kuwadhibiti oppositions na elements zote za upinzani na assasinations za elements zozote zinazoonekana kuwa against na himaya ya CCM.

Idara ya Usalama wa Taifa hii tuliyonayo leo ilianzishwa na CCM 1997 kutoka katika muundo wa kijamaa wa chama kimoja, hii ni baada ya kuanzishwa mfumo wa vyama vingi, kwa hiyo bado unaiserve CCM kwanza kisha Taifa linatafsiriwa salama kupitia matokeo ya uimara wa ccm, kama yakifanyika mageuzi ya kimuundo, kisheria, kikanuni na kisera, uimara wa Taifa hautatafsiriwa kupitia uimara wa ccm madarakani, na mambo mengi tunayolalamikia sasa juu ya taifa hayatakuwepo tena. In simple words, taswira kubwa inayoonekana yauhakika ni kazi yao ya kulinda viongozi, kusafiri na viongozi na kuilinda CCM.

Nje ya mambo ya Ujasusi wa Kiuchumi ambao mimi ndio ninaoupigania siku zote uongoze nchi, Naweza kusema Tanzania tuko vizuri katika Ujasusi wa kidola kuliko nchi yoyote pengine Afrika nzima, Hili limefanya kuimeza idara na kuonekana siasa ambazo ndio zinabeba taswira kubwa ya ubora ama udhaifu wa ujasusi Tanzania, Eneo la Ujasusi wa Kidola Tanzania kuna vitengo vya wachapakazi hasa kiko jeshini.., kitengo cha ujasusi ambacho kilikuwa kiko free from politics party ni CMI (central military intelligence). Lakini bahati mbaya muundo na aina ya uongozi wa Magufuli ulikiingiza katika siasa pale kilipofanywa kuwa decision maker wa nchi, lakini upande wa foreign assets ndio wazuri sana wako bize kukusanya taarifa hatarishi dhidi ya nchi...

Kwahatua hii naomba niseme wazi, Mradi wa Bagamoyo ulitakiwa uanze kabla ya Bwawa la Nyerere kule Rufiji ama ungeanza kabla ya SGR, Now sasa nasema taifa linakwenda kushinda vita vya kiuchumi afrika mashariki na kati.

Kuanzia sasa atakayempinga mama nitamloga nitamloga

Kwa undani zaidi Soma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi.
View attachment 1830718
Ni kweli kwa hili la ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo na umuhimu wake kwa Taifa kwa leo.
Ila naona una kauli mbili mbili katika mtazamo wako kuhusu ujenzi wa Bwana lá Umeme.

.Mimi sio nabii, lakini angalau nikisema jambo nakuwa nimeona kijacho mbeleni, Naomba nikukumbushe jambo muhimu ambalo niliandika 13 March 2019 katika makala hii chini.

Katika makala hii nilianza kwakusema, "Vita vya Kiuchumi Tanzania chini ya mradi mtambuka wa maporomoko ya Rufiji, siasa ya Mazingira duniani na muundo na mienendo ya Shirika la Elimu, Sayansi na Udhibiti wa Mazingira duniani (UNESCO), vinanipa sababu ya kuiponeza TISS katika ulimbe huu wa vita vya kiuchumi.

Bonde la Rufiji liko kwenye urithi wa dunia kwamjibu wa Shirika la Uhifadhi wa Mazingira (UNESCO), Na hivyo ulinzi wa bonde hili ni kwa sheria za kidunia sio kwa sheria za Tanzania, hapa ndipo ambapo nataka kusifu idara za ujasusi na kumsifu Rais Magufuli kwa kuishinda dunia dhidi ya misimano na sera za mashirika haya ya kidunia ambayo Mwalimu yalimshinda, Mwinyi yalimshinda, Mkapa yakamshinda, Kikwete yakamshinda.

Kwa wiki kadhaa nimekuwa nikipitia nyaraka za kijasusi za mashirika na taasisi mbalimbali ulimwenguni (Realiised docs), nimejiridhisha kuwa vita nikubwa kuliko wengi wanavyofikiri, na ikiwa mradi wa umeme bonde la Rufiji utafanikiwa, basi TISS itaingia kwenye historia ya mashirika bora kabisa ulimwenguni kwa counter intelligence hii. Palipo na uthubutu lazima tupongeze.

Awali mradi huu wa Umeme wa Stiegler's Gorge Ethiopia walikubali kujenga, lakini hakuna maelezo kama waliishia wapi ama walishindwa tenda. Zikawepo taarifa za Waturuki kuwa watajenga, nazo zikaishia hewani. Kisha tukashuhudia Arabb Contractors wa Misri wakisaini mikataba ya ujenzi. Bado ujenzi rasmi haijaanza, lakini hatua tu ya kuthubutu kusaini mkataba ni hatua kubwa inayostahili kupongezwa.

Bunge la Ujerumani liliweka azimo kuitaka serikali ya nchi hiyo kuzuia ujenzi wa mradi huo wa Rufiji na badala yake serikali ya Ujerumani isaidie kujenga vinu vya gesi kwaajili ya nishati ya umeme. Kwakuangazia jambo hili watu wengi wanaweza kujiuliza, itakuwaje nchi ya Ujerumani iingilie masuala ya ndani ya Tanzania? Mifumo ya kijasusi iko hivi, kwamjibu wa Nyaraka za idara ya ujasusi ya nchini Lithium (Anual report 2016) inaonyesha kuwa Ujerumani pekee ina majasusi 11 wa ngazi za juu ndani ya UNESCO, na kwa nadharia hiyo, Ujerumani ikitaka kuzuia miradi yoyote yenye uharibifu wa mazingira inatumia msukumo wa UNESCO.

Kinachoweza kutokea ni kuwa UNESCO inaweza kuiandikia barua ya katazo nchi husika kwamba pale ni sehemu ya Urithi wa Dunia (World Heritage site.) na hairuhuriwi kupajenga. Na wanaonya kuwa ukiwa mbishi na ukaendelea kujenga utakuwa black listed. Na kampuni inayopata tenda ya kujenga nayo inapewa barua na kuonywa kuwa itakuwa black listed na Bank Account zako zitakamatwa. Kwakufanya hivyo wanashinikiza kampuni zijitoe katika mradi husika.

Majasusi hawa wamefanya hivyo kuidhibiti Iran, enzi za Reza Khan kwakutumia mashirika haya ya kidunia , ambayo mengi ni mashirika ya kijasusi. Pia nchi za Panama zimewahi kukumbana na nguvu ya mashirika haya.

Kwa namna yoyote naipongeza Serikali kwa ujasiri huu wa kufunga masikio na kelele za kidunia na kuamua kuanzisha mradi huu uliokwamba tangu miaka ya 60+. Hii ni hatua kubwa sana na ninaamini itaacha legacy kubwa sana kwa rais Magufuli na kwa vyombo vya ujasusi nchini ikiwa utafanikiwa, ingawa hakuna nchi au kikundi kilichowahi kushindana na mashirika haya ya kidunia na kikashinda, zaidi ya hapo labda ziwe ni siasa za kura. Bado naamini tumethubutu pakubwa sana, na katika ndoto tutashinda". Makala iliishia hapo.

Sasa mwaka mmoja na baadaa ya makala hii, Kampuni iliyokuwa ikijenga mradi huo imeandika taarifa hii ambayo inajumuisha ndani yake katazo la UNESCO. Isome hapa kwa lugha ya kitumwa....>>> ElSewedy Electric Co - Council on Ethics

Unaweza kujipa nafasi ya kusoma kwa undani zaidi kitabu cha Ujasusi kujua nama Ujasusi dhidi ya Ujasusi unavyofanya kazi na mifano hai toka katika viunga vya dunia ya ujasusi.

Nunua Kitabu kwa Ofa ya Mwezi Mtukufu na #Corona kwa 25,000 tu popote ulipo. Badala ya bei halisi ya 80,000/=

Nunua kwa Mpesa na Tigopesa 0715865544/ 0755865544 (Yericko Nyerere) kisha tuma majina yako na mahali ulipo.

Kwa Dar kitabu kitaletwa ulipo bure. Nje ya Dar nauli ni 8,000/=
 
Kwa maelezo yako tu, huo mradi ni wa kijinga, yaani bandari ya Dar, Tanga na Mtwara iwe kwa ajili ya bidhaa za ndani tu (ambayo TRA inakusanya mapato) halafu hio bandari ya Bagamoyo ihusike na bidhaa kwenda nje Zambia, Congo, Malawi na Uganda halafu mapato yanakwenda kusokojulikana ( TRA haihusiki)

Uchumi wa TZ kwa miaka mingi unategemea mapato ya bandari kwa biashara ya kimataifa, ndio maana tulijitoa COMESA Baada ya sharti la free trade tukaogopa kukosa mapato ya biashara kimataifa, na sisi ndio lango kuu kwa upande wa bahari ya hindi, kuwakabidhi hayo mapato wachina na waarabu ni ujuha,hapo Kuna harufu kubwa ya rushwa kwa viongozi ili kuizamisha nchi na watu wachache kunufaika.

Acha wachina wajione wajanja kwa kurubuni viongozi wetu uchwala lakini historia itakuja kujirudia
 
Kwa maelezo yako tu, huo mradi ni wa kijinga, yaani bandari ya Dar, Tanga na Mtwara iwe kwa ajili ya bidhaa za ndani tu (ambayo TRA inakusanya mapato) halafu hio bandari ya Bagamoyo ihusike na bidhaa kwenda nje Zambia, Congo, Malawi na Uganda halafu mapato yanakwenda kusokojulikana ( TRA haihusiki)

Uchumi wa TZ kwa miaka mingi unategemea mapato ya bandari kwa biashara ya kimataifa, ndio maana tulijitoa COMESA Baada ya sharti la free trade tukaogopa kukosa mapato ya biashara kimataifa, na sisi ndio lango kuu kwa upande wa bahari ya hindi, kuwakabidhi hayo mapato wachina na waarabu ni ujuha,hapo Kuna harufu kubwa ya rushwa kwa viongozi ili kuizamisha nchi na watu wachache kunufaika.

Acha wachina wajione wajanja kwa kurubuni viongozi wetu uchwala lakini historia itakuja kujirudia
Hii ni bandari ya viwanda ya kuleta mali ghafi kwenye viwanda ndio maana inajengwa sambamba na viwanda zaidi ya mia saba na itatoa ajiri rasmi kwa wazawa zaidi ya laki mbili watanzania tuache kupinga kila kitu.
Mlalamika ajiri ndio hizo ajira zinakuja
 
Leo wachina walijaa mtaani kwetu uku bagamoyo wakipima survey kwenye makazi ya watu...ngoja tujiandae kuhama kuwaachia mji
 
Akili ni kile kinachobakia, ukiondoa nadharia na vitendo vyote vya darasani.
Hili jambo mnalishabikia kwa sababu zenu mnazozijua nyie. Umeme ndiyo msingi mkuu wa maendelea kwa nchi yoyote. Jenga bandari kila kona ya nchi kama huna umeme wa uhakika bandari zako ni bure. Umeme wa uhakika ndiyo chanzo kikuu cha wawekezaji kuwekeza katika nchi yoyote.
 
Back
Top Bottom