Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 613
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Amatus Liyumba, amekwaa kisiki tena mahakamani baada ya serikali kushinda rufani dhidi ya uamuzi wa Hakimu Nyigulila Mwaseba aliyelegeza masharti ya dhamana.
Hakimu huyo pia sasa hataendelea tena kusikiliza kesi hiyo.
Jaji Godfrey Shaid alisema kifungu cha 148 (5) cha mwenendo wa makosa ya kijai (CPA) hakielezei kosa la wizi na kusababisha hasara tu hivyo masharti nafuu ya dhamana yaliyotolewa kwa Liyumba yalitolewa kwasababu kifungu hicho kilitafsiriwa vibaya.
Hakimu huyo pia sasa hataendelea tena kusikiliza kesi hiyo.
Jaji Godfrey Shaid alisema kifungu cha 148 (5) cha mwenendo wa makosa ya kijai (CPA) hakielezei kosa la wizi na kusababisha hasara tu hivyo masharti nafuu ya dhamana yaliyotolewa kwa Liyumba yalitolewa kwasababu kifungu hicho kilitafsiriwa vibaya.