Mpira wa Afrika na kushindwa kujiandaa

Mpira wa Afrika na kushindwa kujiandaa

Davives

Member
Joined
Feb 2, 2024
Posts
86
Reaction score
106
Wakuu samahani hivi viongozi WA timu zetu wanashindwa kuandaa mbinu za kukabiliana na maamuzi mabovu ya warefa WA hizi mechi kubwa.?

Leo ndio simba kafungwa lakini tulijua kabisa kuwa lazima mwamuzi atakuwa upande WA RS berkane.kwanini simba isingeandaa mbinu ya kukabiliana na hayo yalikuwa yanakwenda kutokea?

Ila poleni makolo timu hamna hamjui kupiga counter attacks gemu ilikuwa yenu hii🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Tatizo simba mmezoea kubebwa na marefa, Simba mmebebebwa mechi kibao. Leo refa kawakazia mnamuona mchawi.

Hata mechi ya kwanza tu na berkane mlipunguziwa magoli kwa kubebwa na marefa.

Kuna mechi za nyuma mnacheza muda usioeleweka yaani mpaka mpate goli ndio mpira unaisha.

Wale wa south nusu fainali simba iliwafunga kwa kubebebwa na Var ila wao wakakataliwa goli lao na var.
 
Fafanua, kivipi Refa alikuwa upande wa Berkane.
Kama suala ni red card, kanuni ziko wazi, Mchezaji rafu wa Simba hakugusa mpira, akitokea nyuma akapiga mguu wa mchezaji wa Berkane, mbele ya macho ya Refa na tayari alikuwa na Yellow card na maonyo kadhaa.

Kuhusu kukataliwa goli, tuilaumu VAR kuwepo uwanjani, maana hiyo ndio ilisema kuna offside wakati huo Refa alishasema ni goli.
 
Chukueni hata jagi
Kombe mbona wamebeba!
Screenshot_20250522-154015_1.jpg
 
Tuambiane ukweli, Simba inabidi kuifumua safu yote ya mbele kuanzia namba 7 hadi 11. Wachezaji pekee wanaotakiwa kubaki pale mbele ni Mpanzu, Mutale na Mavambo baaasi na labda tumfikirie pia Mukwala.

Wengine woote kuanzia Kibu, Chasambi, Balua, Ngoma, Ateba, Awesu wawekwe pembeni.

Simba ili iende hatua inayofuata inahitaji viungo na mawinga walio skilled zaidi, wenye uwezo wa kuupokea mpira, wakapush kwa kupasiana, wakaufikisha mpira eneo la hatari kwa formation na combination plays zinazoeleweka na walio na uwezo wa kubaki na mpira hata wakiwa pressed badala ya kukimbilia kuurudisha kwa mabeki au golikipa.
 
Tuambiane ukweli, Simba inabidi kuifumua safu yote ya mbele kuanzia namba 7 hadi 11. Wachezaji pekee wanaotakiwa kubaki pale mbele ni Mpanzu, Mutale na Mavambo baaasi na labda tumfikirie pia Mukwala.

Wengine woote kuanzia Kibu, Chasambi, Balua, Ngoma, Ateba, Awesu wawekwe pembeni.

Simba ili iende hatua inayofuata inahitaji viungo na mawinga walio skilled zaidi, wenye uwezo wa kuupokea mpira, wakapush kwa kupasiana, wakaufikisha mpira eneo la hatari kwa formation zinazoeleweka na walio na uwezo wa kubaki na mpira hata wakiwa pressed badala ya kukimbilia kuurudisha kwa mabeki au golikipa.
Tatizo ni referee au wachezaji
 
Kwa muda mrefu simba walikuwa slow. Mfano Kamara anakaa na mpira zaidi ya sekunde 30 hajaamua apeleke wapi, Ahoua hali kadhalika. Kibu, Ateba, Nouma hawakufanya chochote. Kagoma anasifiwa sana lakini kiukweli jamaa anacheza rafu sana, akikutana na marefa makini kama Arajiga ni bahati kwake kumaliza mchezo bila red card
 
Wakuu samahani hivi viongozi WA timu zetu wanashindwa kuandaa mbinu za kukabiliana na maamuzi mabovu ya warefa WA hizi mechi kubwa.?

Leo ndio simba kafungwa lakini tulijua kabisa kuwa lazima mwamuzi atakuwa upande WA RS berkane.kwanini simba isingeandaa mbinu ya kukabiliana na hayo yalikuwa yanakwenda kutokea?

Ila poleni makolo timu hamna hamjui kupiga counter attacks gemu ilikuwa yenu hii🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
kefa kayombo huku hana msaada poleni makolo
 
Back
Top Bottom