Mpinzani Aliyebakia: John J. Mnyika… Wengine Watabakia?

Mpinzani Aliyebakia: John J. Mnyika… Wengine Watabakia?

Watu kama Sugu, Boniface Jacob, Maranja Masese, huwa nawatilia shaka siku zote. Wameamua kukaza tu uchaguzi upite, ila wako mbali na Chadema.

Hatua zao ni kama za Zitto, utawaona mitandaoni zaidi kuliko field. Baada ya Mbowe kufurushwa mamluki wengi wanajitahidi kuficha rangi zao ila mda utawaumbua.
 
Wabongo wanapenda sana siasa za kuamini watu, wanasahau kwamba mwanasiasa ni kama mtu mwengine anaweza kubadili mitazamo yake na akawa na vipaumbele vyake.
Kuna vitu mtu anaweza kubadili misimamo yake...baadhi ya misimamo inahusisha wajihi wa mtu. Kwenye mambo makubwa mtu asiwe na undumilakuwili...kama unasema unapinga ufisadi basi uupinge hata kama anayefanya ni mama yako. Kwenye vitu vidogo wote tunaweza kubadili mawazo.
 
Nadhani issue hapa ni hela zinazotumika kuwanunua hawa watu…

Na hii michezo muasisi wake alikuwa Magufuli…
Na kabla ya Magufuli walikuwa hawahami CHADEMA kwenda CCM kila ukifika uchaguzi.
 
Wapinzani wa kweli kwangu wapo watatu

MTIKIRA

LISSU

HECHE

Hao watu wana misimamo isiyoyumba, wanasimamia kile wanachokiamini na sio wabinafsi..!! Hawana bei
Naona umeanda kujificha juu ya dari wiki moja kabla ya maandamano
 
Mnyika alifanya kazi nzuri sana kuwasainia Covid19 ile barua yao. Atakumbukwa daima kwa ushujaa wake.
Hilo wala halina nafasi kwenye mada iliyopo mezani. Aliyemtoa Nusrat Hanje Gerezani tena usiku ndiye mhusika mkuu wa mambo yote. Na hata wewe una ukweli wote.
 
Kuna vitu mtu anaweza kubadili misimamo yake...baadhi ya misimamo inahusisha wajihi wa mtu. Kwenye mambo makubwa mtu asiwe na undumilakuwili...kama unasema unapinga ufisadi basi uupinge hata kama anayefanya ni mama yako. Kwenye vitu vidogo wote tunaweza kubadili mawazo.
Hapo ni kumpangia mtu na kumuwekea mipaka sijui shida yote hiyo ya nini? Huku kuweka imani kwa watu ndio maana kumefanya kuwe na hiyo biashara ya kuwanunua hao watu na kuna wakati hata mnashindwa kuona au kuyakubali mapungufu ya hao watu mnaowaamini hadi pale watakapo nunuliwa ndio mnakuja kujiona mlifanywa wajinga wakati wote.
 
But you conviniently left out Dr. Slaa: one of the biggest fraudsters opposition parties in the country have ever had. When things didn't go his way he joined CCM under Magufuli, after Magufuli's death, he returned to the opposition parties' side again.
 
I will go one extra..., huenda shida zaidi ni Utofauti wa Kiitikadi kwa wanaopingana Practically Ideologically wote ni walewale..., Hivyo sababu kwa wengi ni Platforms za kupata Kura kwenda Kula huenda kwa sasa shortcut ni hio (Na wengi hawaami sio sababu ya utofauti wa kimawazo bali kuogopa Backlash, na kuhama kwao kutakuwa a Political Suicide....

Kama nilivyosema hapo awali haya yashakuwa magenge.... na nikashauri Haki ya Kikatiba ya kuwa na Mgombea Binafsi ipiganiwe (Leo hii Mpina angeweza kutema Cheche na sio kuzibwa mdomo kwa technicalities za Vyama)

 
Hapana. JJ Mnyika ni mtu wa pekee sana. Hana tamaa ya mali wala madaraka. Hana majivuno wala kiburi. Mtu mwenye misimamo imara isiyoyumbishwa kwa ushawishi wa namna yeyote ile.

Nakumbuka enzi zile za Jiwe, alishawishiwa mno kwa ahadi kede kede ili mradi tu aunge mkono juhudi lkn wapi. Hivyo huyu Jamaa ni Mpinzani muaminifu na mkweli.
Hakika zama zile ushawishi ulikuwa mkubwa sana kumsajili CCM lakini alibaki na msimamo wake dhabiti tofauti na kina Silinde na wengineo Mnyika hakika amenyooka hayumbishwi hata kidogo
 
Naona umeanda kujificha juu ya dari wiki moja kabla ya maandamano
Ushazoea kufichwa basi unaona kila mtu wa kufichwa..!!
Nishakwambia we chawa tafuta kazi mpya tar 29 unaenda kupoteza ajira 😹
 
Kutomtaja John Mnyika ni kumkosea heshima ya kutambua kazi zake.
Naelewa kwanini haujamtaja. Sababu yeye siyo mwanaharakati kama uliowataja, Ieleweke hiyo haimfanyi kutokuwa mpinzani wa kweli.
Mnyika hajawahi kupitishwa kwenye moto mkali km hiyo miamba..!!

Hata hivyo siwezi kupinga mtazamo wako, kila mmoja na kile anachoamini mkuu..
 
But you conviniently left out Dr. Slaa: one of the biggest fraudsters opposition parties in the country have ever had. When things didn't go his way he joined CCM under Magufuli, after Magufuli's death, he returned to the opposition parties' side again.
Dr Slaa sio mnafiki. Asingeweza kuendelea kuwa kwenye genge la wahuni waliompaka kinyesi Lowassa lakini wakaamua kula matapishi yao na kumsafisha Lowassa.
 
Usiwaamini sana mdogo angu, wasije wakakushangaza
Kwa walichopitia na wanachoendelea kupitia hao ni wapinzani wa kweli..!!

Lissu alikataa PESA za duli na akabaki na misimamo yake, wakati Msigwa kashindwa uchaguzi wa kikanda tayari katema bungo.!!

Huyo Mtikila wakaona mpaka wamtafutie ajali ya mchongo.
 
Kwa walichopitia na wanachoendelea kupitia hao ni wapinzani wa kweli..!!

Lissu alikataa PESA za duli na akabaki na misimamo yake, wakati Msigwa kashindwa uchaguzi wa kikanda tayari katema bungo.!!

Huyo Mtikila wakaona mpaka wamtafutie ajali ya mchongo.
Sema huyu Lissu sio wa kupanga naye dili lolote maana lazima ataweka kila kitu hadharani. Kwenye stori yake kuhusu Abdul alinichekesha sana aliposema kwamwambia Abdul akamwambie mama yake amlipe stahiki zake.
 
Sema huyu Lissu sio wa kupanga naye dili lolote maana lazima ataweka kila kitu hadharani. Kwenye stori yake kuhusu Abdul alinichekesha sana aliposema kwamwambia Abdul akamwambie mama yake amlipe stahiki zake.
Lissu mwana hip hop anapiga punchline za kibabe 😹😹
 
Mnyika bado uwa simuamini pamoja na yote huyu bado sio mpinzani 100%

Mtanisamehe lakini Kuna siku mtanikumbuka huyu ni mpinzani Aina ya Mbatia
Mnyika ni katika ukatibu Mkuu wake Chadema imeumia sana.
 
Back
Top Bottom