Mpinzani Aliyebakia: John J. Mnyika… Wengine Watabakia?

Mpinzani Aliyebakia: John J. Mnyika… Wengine Watabakia?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,092
Reaction score
43,265
Hakuna namna tumpe maua yake. Unapokuta watu uliowadhania ni wapinzani wanageuka na kujiunga na CCM wakati wa uchaguzi ni lazima ujiulize kama walikuwa wapinzani kweli au walikuwa wanatafuta pa kuhemea tu.

Ati leo Joshua Nassari yuko CCM..
Ati leo Wenje yuko CCM
Ati leo Peter Msigwa yuko CCM...


Kazi kwelikweli
 
Hakuna namna tumpe maua yake. Unapokuta watu uliowadhania ni wapinzani wanageuka na kujiunga na CCM wakati wa uchaguzi ni lazima ujiulize kama walikuwa wapinzani kweli au walikuwa wanatafuta pa kuhemea tu.

Ati leo Joshua Nassari yuko CCM..
Ati leo Wenje yuko CCM
Ati leo Peter Msigwa yuko CCM...


Kazi kwelikweli
Sasa hapa kwenye mada hii kuna jipya lipi mkuu ' Mwanakijiji"? Au kwa vile umezungumzia hao wachache tu toka CHADEMA, ambao wote walijulikana toka zamani?
Tunao wakongwe, akina Lipumba, Cheyo; akina Qeen Sendeka (hata sijui kama jina ni sahihi), na wengi wengine; lakini kutomtaja Mbowe kutanifanya nisiwe mkweli kwa kiasi kikubwa
Ndio, akina Mzee wa Kiracha (?) hao walikuwa ni wapinzani wa dhamira ya mioyo yao, au walikuwa ni wachimba dhahabu?

Yule nani yule, Mtikila, alikuwa ni mpinzani, kwa sababu alisimamia jambo ambalo halikuwa na lengo la kumletea manufaa yeye binafsi.

J.J. Mnyika, ni 'principled, mbali kabisa na hizi takataka za akina Wenje, Yericko na wengi wengine waliokuwa wamejazana ndasni ya chama hicho kabla ya ujio wa uongozi mpya.
N.B., Sitakuwa mkweli pia kama siwezi kumtambua binti Halima Mdee aliye "kengeushwa". Huyu ni mpinzani wa kweli.
 
huyu ni mpinzani Aina ya Mbatia
Naelewa maana yako.
Tofauti kubwa kati yake na huyo Mbatia; JJMnyika hajashika mamlaka ya kuendesha chama. Huyu ni mtumishi mwaminifu kwa anaye mtumikia. Sijaona dalili zozote akienda kinyume na masharti hayo; hata wakati wa Mbowe.

Kawawa na Nyerere walweza kufanya kazi pamoja kwa mafanikio makubwa; kwa sababu Kawawa alikuwa mwaminifu katika utumishi wake chini ya uongozi wa Mwalimu Nyerere.

Mbatia ni kesi tofauti kabisa.
 
Mnyika bado uwa simuamini pamoja na yote huyu bado sio mpinzani 100%

Mtanisamehe lakini Kuna siku mtanikumbuka huyu ni mpinzani Aina ya Mbatia
Hapana Mnyika ni mseminari hawezi kugeuka. Yaani hata lile sakata la lowassa hakuhama bali alisusa tu. So atakua mtu wa mwisho kuhama, ndio maana ule uchaguzi alisimamia haki hakuweka uchawa au kumlinda Mbowe.
 
Usimalize maneno, tumpe muda.

Wanasiasa hufanya lolote kwaajili ya maslahi yao binafsi.
Ngoja maslahi yake binafsi yaguswe tuone.
 
Mwamba alikuwa Jabali la siasa za upinzani 😃
1000039861.jpg
 
Kama hadi leo hii huamini upinzani wa Tundu Lissu, na kudhani yupo yupo tu kuhadaa watu, wewe utakuwa ni mtu wa utani mwingi sana wa kusikitisha.
Hata John Heche simtilii mashaka katika upinzani wa sasa.
Hii Chadema ya wakati huu hakuna mamluki au mchumia tumbo atabaki! Kwa sababu mirija yote imekata! Ruzuku wamesitishiwa kwa hila ya Wazanzibari! Kwa hiyo watapukutika wote, na wataokaobaki watakuwa ni washindani wa kweli.

Natamani pia kuona siku moja Halima Mdee anarejeshwa kwenye chama! Pamoja na mapungufu ya kulazimisha kwenda bungeni, lakini bado amejitahidi kubakia kwenye mstari.
 
Mnyika bado uwa simuamini pamoja na yote huyu bado sio mpinzani 100%

Mtanisamehe lakini Kuna siku mtanikumbuka huyu ni mpinzani Aina ya Mbatia
Mkuu mpinzani akiwa anatukana tukana hovyo, ndiyo anaonekana wa maana kama anavyofanya sugu? Upinzani ni hoja zenye mashiko siyo makelele na mitusi
 
Mnyika bado uwa simuamini pamoja na yote huyu bado sio mpinzani 100%

Mtanisamehe lakini Kuna siku mtanikumbuka huyu ni mpinzani Aina ya Mbatia
Hapana. JJ Mnyika ni mtu wa pekee sana. Hana tamaa ya mali wala madaraka. Hana majivuno wala kiburi. Mtu mwenye misimamo imara isiyoyumbishwa kwa ushawishi wa namna yeyote ile.

Nakumbuka enzi zile za Jiwe, alishawishiwa mno kwa ahadi kede kede ili mradi tu aunge mkono juhudi lkn wapi. Hivyo huyu Jamaa ni Mpinzani muaminifu na mkweli.
 
Wapinzani wa kweli kwangu wapo watatu

MTIKIRA

LISSU

HECHE

Hao watu wana misimamo isiyoyumba, wanasimamia kile wanachokiamini na sio wabinafsi..!! Hawana bei
Kutomtaja John Mnyika ni kumkosea heshima ya kutambua kazi zake.
Naelewa kwanini haujamtaja. Sababu yeye siyo mwanaharakati kama uliowataja, Ieleweke hiyo haimfanyi kutokuwa mpinzani wa kweli.
 
Back
Top Bottom