GE2025 Mpina ashinda kesi kuenguliwa kuwa mgombea Urais

GE2025 Mpina ashinda kesi kuenguliwa kuwa mgombea Urais

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo, Luhaga Joelson Mpina ameshidnda kesi yake dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Tume Huru ya Uchaguzi baada ya kuzuiliwa kurejesha Fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea Urais Kupitia chama hicho.

Kesi hiyo iliyoanza kusikikizwa leo mchana Septemba 11, imemalizika kwa Mpina kushinda na ni rasmi sasa atarejesha fomu ya kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho.

Soma Pia:
Wananchi tumesha kataa uchaguzi ...tumesha sema 2025 hakuna uchaguzi wala tanganyika kutawaliwa na mzanzibar siyo sawa ...wazanzibar wamesha jitwalia taifa lao kwa asilimia 99% huku Tanganyika awana chao tena...kampeni za mpina zinatakiwa kuwa no reform no election..hapo samia atajuta ...vyama vya upinzani vilivyo chukua form vilitakiwa kupiga kampeni ya no reform no election...
 
Pia wakakumbuka bila upinzani bungeni itakuajau bora ACT wagombanie urais wapate kura kiduchu za kuwawezesha kupata viti maalum na hiki ndicho ACT wanapigania Viti maalum.
Aisee... Ila kwa inavyoonekana hili ndio lilikuwa lengo toka Awali ila Monalisa ndiye alikuja ku intercept nadhani hakuwa miongoni mwa waliobariki huo mchakato.
 
Pia wakakumbuka bila upinzani bungeni itakuajau bora ACT wagombanie urais wapate kura kiduchu za kuwawezesha kupata viti maalum na hiki ndicho ACT wanapigania Viti maalum.
ACT wanapigania kushika dola wewe, ndio chama pekee cha upinzani kilicho serious kwa sasa.
 
Mahakama ilichosema utaratibu wa kumzuia kurudisha fomu haukuwa sahihi kama kulikuwa na barua ya msajili walipaswa kupokea fomu kisha kwenye mapingamizi ndo utaratibu ungezingatiwa .

Hivgo si sahihi kusema kama ameruhusiwa kuwa mgombea.
 
Huyu ndie Luhaga Mpina kiboko ya mafisadi. Mpenda maendeleo ya watanzania.
 

Attachments

  • image_search_1757602550539.jpg
    image_search_1757602550539.jpg
    18.3 KB · Views: 13
Hii ni planned movie



Soma hapa


I don’t think so. Brawl ya Chura Kiziwi na Mpina siyo ya kuigiza. Utaona jabs zitakazokuwa traded baada ya hapa!
 
Huwezi mshinda Samia, kwa mfumo wa sasa ni taahira pekee anaweza kudhani anaweza kuwa Rais na Samia akashindwa.

ACT are just making numbers. Ndiyo maana wenye akili walijua bila reforms huna lolote zaidi ya CCM kukugawia kura zisizo na athari kwao.
 
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo, Luhaga Joelson Mpina ameshidnda kesi yake dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Tume Huru ya Uchaguzi baada ya kuzuiliwa kurejesha Fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea Urais Kupitia chama hicho.

Kesi hiyo iliyoanza kusikikizwa leo mchana Septemba 11, imemalizika kwa Mpina kushinda na ni rasmi sasa atarejesha fomu ya kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho.

Soma Pia:
Sasa waliotegemea kukosa mpinzani kwenye uchafuzi wa 2025. Itakuwaje.
 
Aisee... Ila kwa inavyoonekana hili ndio lilikuwa lengo toka Awali ila Monalisa ndiye alikuja ku intercept nadhani hakuwa miongoni mwa waliobariki huo mchakato.
Yeah lengo la ACT sio dola maana wanajua hawawezi kuipata ila ni viti maalum ndo maana wamemtafuta mtu mmwenye angalau ushawishi wa kutimiza azma yao. Mpina anatumika kama daraja la kuwafikisha nchi ya ahadi na baadae watamkataa.
 
Sawa uchaguzi ukimalizika na matokeo yakatoka mwambie nauza Reso za macho hapa kariakoo hata za mkopo zipo.
 
Swali la kujiuliza ameruhusiwa kurudisha fomu kwa tume ya uchaguzi je hiyo tume italipitisha jina lake ili agombee hiyo nafasi ya urais mwenye mamlaka ya nani agombee ni tume na si mahakama
 
Back
Top Bottom