''Mpemba'' wa meno ya tembo afikishwa mahakamani

''Mpemba'' wa meno ya tembo afikishwa mahakamani

Mambo Haya Yanahitaji Umakini Sana Kuna Muda Watu Wakosa Hata Neno La Kusema!
Yaani Hawa Ndiyo Tuseme Miaka Yote Wanauwa Ama Walijiingiza Kwenye Biashara Ya Ujangiri Bila Hodi.

Itapendeza Tukisikia Wakubwa/Wadogo
Waliko Serikalini/Binafsi
Nao Muda Wakamatwe Ili Tujue Vyombo Vinafanya Kazi
Ikumbukwe Ndani Ya Serikali Juzi Mlisikia Mbalari Hakimu Alimhukumu Mtuhumiwa Kwa Kuchagua
Kulipa Faini Ama Kifungo

Tegemeeni Hukumu Za Ajabu Kwa Kesi Hii Na Hata Malkia Wa Ndovu.
 
Kazi inaendelea, baada ya kuanza octoba 25!
 
Hata log me in ngoma nzito. Lakini ni kwa nini mvuvi avue dagaa na kuacha sangara? Kwani huo ni uvuvi au ni kokoro[emoji2]?
 
Ila sijaona kinara wao mkuu ambaye mpaka meli anazo!!!! Ila yuko kimya sana sijaelewa maana yake katika hili jahazi!!!
 
Mbona mpemba dhaifu..hana taswira kama aliyoieleza Rais..mi naona angeanza na wale Polisi waliotungua helikopta afu fasta wakawabambikia kesi watu "dhaifu" wakafungwa fasta ili kuficha uovu wao
 
Kwa Umri wao na hii vita ya Ujangiri hawaendani nayo kabisa naweza sema ni bambika kesi wahusika waishi salama...
 
Mambo mengine hua yanashangaza sana.Huyu Mpemba haraka haraka anapelekwa mahakamani.Kwani akina Masamaki na mafisadi wengine wako wapi?Mambo mengine,kama mchezo wa kuigiza hivi.Lakini mamlaka iwe makini kwa kuwa wananchi sio wajinga sana.
View attachment 435213
View attachment 435216
View attachment 435217
Mtuhumiwa wa makosa ya kukamatwa na nyara za serikali, Yusuf Ali Yusuf maarufu kama Shehe Mpemba (35) kushoto kwenye picha ambaye alitajwa na Rais John Magufuli kuwa ndiye kinara wa biashara ya meno ya tembo na wenzake Charles Mrutu (37), Benedict Kungwa (40), Jumanne Chima (30), Ahmed Nyagongo (33) na Pius Kulagwa (46) wamefikishwa mahakamani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Thomas Simba na hawakutakiwa kujibu chochote na kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba Mosi, mwaka huu itakapotajwa tena huku watuhumiwa hao wakirudishwa rumande.

Hii ni Hati ya Mashitaka.

kisutu1.jpg

kisutu2.jpg

kisutu3.jpg
 
Nayo yamevaa t-shirt zebye maneno "In God I Trust"...nyambafu zao. Majizi kumbe nayo yanaombaga Mungu eh!!!?
 
Back
Top Bottom