MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,185
- 24,051
Kama humfahamu mtu anayejulikana kama ''mpemba'', ingia kwenye mtandao ya NGO zinazopambana na vita vya ujangili wa nyara za serikali au subiri kesi ya ''Malkia wa pembe za ndovu''.
Ukitaka kumfahamu ''mpemba'' pitia hii thread;
Katibu wa zamani wa Simba Hasonoo kortini kwa wizi wa pembe za ndovu
Watanzania wengi ni wagumu sana kubadilika!
Makamu wa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan kila siku anawambia wabadilike kwa sababu zama zimebadilika lakini wameziba masikio na hawataki kubadilika.
Ndugu yangu Diwani Athumani alikuwa anadhani ni zama zileee ambazo unaweza kuweka uzio katika uchunguzi kwa sababu ya cheo chako au ukaribu wako na Ikulu na hakuna wa kuhoji kwa nini unaweka uzio .
Huu sio muda wa kukumbatia mitandao ya kijangili na kifisadi. Zama zimebadilika sana.
Kwa nini baadhi ya watu hawajifunzi kwa Home Shopping Center ambayo baada ya kunusa hatari iliyoko mbele wakaamua kujifilisi kisheria na kuibuka huku wamevaa ngozi nyingine kibiashara inayoitwa GSM Foundation.
Rais Magufuli kila mara anawaambia kama unafahamu ulikuwa unatenda dhambi za kisiasa na kiuchumi. Huu ni muda wa kutubu na kuachana na dhambi hizo.
Vita vya nyara za serikali imemuondoa Diwani Athumani.
Kuna wengine bado wako mbioni kusombwa na mafuriko.
Ukitaka kumfahamu ''mpemba'' pitia hii thread;
Katibu wa zamani wa Simba Hasonoo kortini kwa wizi wa pembe za ndovu
Watanzania wengi ni wagumu sana kubadilika!
Makamu wa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan kila siku anawambia wabadilike kwa sababu zama zimebadilika lakini wameziba masikio na hawataki kubadilika.
Ndugu yangu Diwani Athumani alikuwa anadhani ni zama zileee ambazo unaweza kuweka uzio katika uchunguzi kwa sababu ya cheo chako au ukaribu wako na Ikulu na hakuna wa kuhoji kwa nini unaweka uzio .
Huu sio muda wa kukumbatia mitandao ya kijangili na kifisadi. Zama zimebadilika sana.
Kwa nini baadhi ya watu hawajifunzi kwa Home Shopping Center ambayo baada ya kunusa hatari iliyoko mbele wakaamua kujifilisi kisheria na kuibuka huku wamevaa ngozi nyingine kibiashara inayoitwa GSM Foundation.
Rais Magufuli kila mara anawaambia kama unafahamu ulikuwa unatenda dhambi za kisiasa na kiuchumi. Huu ni muda wa kutubu na kuachana na dhambi hizo.
Vita vya nyara za serikali imemuondoa Diwani Athumani.
Kuna wengine bado wako mbioni kusombwa na mafuriko.