Umehitimisha vizuri juu ya usaliti wa ccm kwa wakulima na wafanyakazi. Usaliti huu ulianzia baada ya chama kuwaweka pembeni wenye chama na kununuliwa na wafanyabiashara wenye kutaka kulinda maslahi yao.Sikio la kufa halisikii dawa! Kama falme zilivyoinuka na kuanguka, anguka kuu la ccm limekaribia! Chama kimekiuka miiko, kimewasahau wakulima na wafanyakazi, kimekumbatia mafisadi, na kinazima kila njia ya sauti ya wanyonge kusikika. Huwezi kujenga nyumba imara yenye msingi dhaifu!
Shida iliyo mbele yetu ni hii, kumnyang'anya tonge la ugali anayekula huleta patashika ya hapa na pale iwezekana hata mapigano. Hawa watu wanataka kuendelea kula ugali wao huku watu wengine wakiendelea kuwa watazamaji!
Watazamaji walio wengi sana, nao walishachoka kuwa watazamaji.