Mpasuko CHADEMA, Nini kifanyike?

Hapana hii ni ya uhakika kabisa kutoka kwa mshuri wa chadema bwana kitila mkumbo ndio alievunja ukimya huu,si habari ya kufikirika kama zile za kina membe,lowassa na sitta kwamba wanautaka urais.

Mkuu wewe ndiye uliyekuwa London na Dr. Mkumbo wakati anasema hayo maneno?
 

Hii kitu mbona iko hapa muda mrefu mpaka slaa mwenyewe tulikua nae akiichungulia nyie mko wapi,sio siri tena hii,amkeni usingizini,yamewakuta safari hii,tunajaribu kuwasaidia.
 
Ndugu yangu hivi huyo namba 5 kweli ana sifa za kugombea urais kweli au umeamua kuwaliwaza wana Chadema.
 

Mkuu tofauti ndio uhai wa chama. Chama kimeishakomaa hivyo kila mtu ndani ya Chama anaamini akipewa kupeperusha bendera ya Chama basi chama kitambeba. Ikulu ni tamu mzee kila mtu anataka awepo pale.
 
Mkuu wewe ndiye uliyekuwa London na Dr. Mkumbo wakati anasema hayo maneno?

kwani kakanusha mkuu,maana nayeye alionekana akichungulia pia iliokuja first time,ni kama zile za lowasa kutuma sms akiwa kitandani ujerumani tu.
 
Huyo Kitila au Mbowe au Slaa, hawajui kama kuna vikao halali vya CHADEMA ambavyo huwa vinapitisha majina ya wagombea katika nafasi za urais na ubunge? Au hivi sasa ndani ya chadema wanateuana tu, kwa hiyo wanahofia kwamba mtu fulani anaweza teuliwa na mwingine asiteuliwe?

Yaani nyie magamba hamuishi kuibua visa vya mitaani na kuvihuisha vionekane vya kweli. No wonder mtaendelea kuaibika pale ukweli unapowekwa hadharani. Ni bahati ilioje kwamba JF hatutumii majina halisi, maana waweza kuwa Wasira au Kikwete weye, na ikawa ni aibu kubwa pale ukweli ukiwa wazi; ndo mnaishia kusema nilikuwa natania, unatania kwenye umati?
 

hapo kwenye red umetafakari kwa umakini au umekurupuka!
 

Kwenye nyekundu hapo, ni mzigo kwa chama hivi sasa. Wakazi wa Arusha wanajuuuta kumchagua. matukio ya uharibifu yamezidi jijini hapa, Watalii wengi hivi sasa hawaendi tena kuhofia usalama wao na sasa wengi wanakwenga mikoa ya morogoro, kigoma na kwingine. Watu wenye busara zao jijini Arusha tunaona kama tumevuliwa nguo kutokana na watu wote wa jiji hili kuonekana kama ni wahuni tu. Ni zaidi ya mwaka mmoja tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu, lakini muda wote huo Mbunge huyo amekuwa akilumbana tu na Meya wa JIJI bila sababu yoyote ya msingi. Hakuna ambalo vijana wamekwishalipata pamoja na kwamba ndiyo waliompa umaarufu huo.
 
Ndugu yangu hivi huyo namba 5 kweli ana sifa za kugombea urais kweli au umeamua kuwaliwaza wana Chadema.

Mkuu huyo namba tano hata ubunge wa jiji la Arusha hatapata tena. Watu wa Arusha wamechoka naye japo bado wanaipenda CDM. Wanasema amekuwa ngumi mkononi mno haangalii maendeleo ya jiji la Arusha. Kuna mtu alinipeleka stend kuu ya mabasi hapa Arusha imebana kweli akaniambia Mbunge na Halmashauri hawana mpango wowote na stend mpya. Pia wanasema hawasikii mipango ya kuindeleza Arusha zaidi ya shari tu.
 
kitila mkumbo-msahuri mkuu wa chadema,sio mwanahalisi.
Weka habari hiyo hapa kama alivyosema..Weka link!
Hiyo uliyoweka hapo juu hamna kitu maana toka jana tumeidiscuss na kuona ni utunzi na usanii wa mtu!
 
Hapana hii ni ya uhakika kabisa kutoka kwa mshuri wa chadema bwana kitila mkumbo ndio alievunja ukimya huu,si habari ya kufikirika kama zile za kina membe,lowassa na sitta kwamba wanautaka urais.

Una uhakika gani kwamba mshauri wa CHADEMA ameyasema hayo?
 

Mkuu huo ni ukweli hata kama watabisha. Mimi binafsi nilikuwa shabiki mkubwa sana wa Lema japokuwa si mpiga kura wa Arusha ila nilimsikia akiongea kwenye kipindi cha Mchakato Majimboni. Niliurahia jinsi alivyokuwa akijieleza na nikasema jamaa akishinda nitakunywa chupa moja ya mvinyo; jamaa akashinda nikanywa mvinyo chupa moja lakini baada ya kuona anayoyafanya ilibidi niutapike mvinyo. Angeacha shari aka concentrate kwenye kuhudumia wapiga kura angeweza kuwa Mbunge wa kudumu lakini kwa hali hii asiombe uchaguzi mdogo hiyo tarehe 5/04/2012.
 

unapima joto eeh, mtasema sana
 
Kabla hujaandika chochote, hebu chukua muda utafakari uelewa wa hadhira yako. Unaoneka mpaka kwenye medula oblangata yako nini lengo la uzi wako. Propaganda huwa hazifanywi hivyo. Jipange upya
 
Mkuu tofauti ndio uhai wa chama. Chama kimeishakomaa hivyo kila mtu ndani ya Chama anaamini akipewa kupeperusha bendera ya Chama basi chama kitambeba. Ikulu ni tamu mzee kila mtu anataka awepo pale.

Aiseee! hapo kwenye red mkuu, tofauti huleta migogoro na mipasuko katika chama vitu ambavyo mwisho wa siku na yaliyoikumba NCCR Mageuzi na wengine.
 
1. Hakuna mpasuko

2. Wewe unatamani kupandikiza mpasuko.

3. Chadema wana utaratibu thabiti hawana haja ya kuweweseka.

4. Dhana hii umeitoa kwenye kinachoendelea CCM, ambayo inawahusu CCM tu hakuna anayeishadidia kwa sababu mwamuzi wa mwisho ni mpiga kura pamoja na rubuni zinazotumiwa.

5. Hujatueleza tufanye sasa ili tunusurike na hili; kwa maana hiyo unachufua hali ya hewa tu.

NAKUSHAURI ZUNGUMZIA MAMBO MUHIMU YA TAIFA, WAACHIE UMBEYA WAMBEYA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…