Kuna mambo mengi nyuma ya pazia kuhusiana na hatima ya Ndalichako ikiwamo mahusiano yake na genge maalumu lenye mahusiano ya siri na nchi moja jirani yenye nia ya kuhujumu mustakabali wa Tanzania ikiwamo elimu na Nyanja nyingine. Kumekuwa na tahadhari kadhaa zilizotolewa kuhusu vikao vya genge hilo lenye nguvu za ajabu na kwa NDalichako kuhusishwa kwake, imekuwa tishio kubwa kwa hatima ya elimu yetu. Kwa sasa bado ni tuhuma na ndio maana ameombwa kupumzika hadi ukweli utakapodhihiri na yeye kuwahi kujihami kwamba anaomba likizo bila malipo ya mwaka mmoja na si kwamba ametakiwa kukaa pembeni.
Tina
===>Sina uhakika na ukweli wa tuhuma hizi,nchi hii ukifanya kazi yako kitaalamu na vizuri na ukiwa mbali na wanasiasa basi wewe hudumu hata siku moja,huyu mama tangu ameingia madarakani kiwango cha uwizi wa mitihani kimepungua kwa kiwango kikubwa sana,na heshima ya bara za la mitihani imeongezeka kwa kiwango cha juu sana.
===>Siasa zimesababisha tunasahau mambo ambayo yanasababisha wanafunzi kufeli nitataja yafuatayo:
a--Udahaili wa walimu kuanzia miaka ya 2000 hapa kulifanyika madudu ya hali ya juu,walimu wengi walifoji vyeti vya shule hasa walimu wa grade A ambao wao ndio wafundishaji au wazalishaji wa mwanzo kabisa wa watoto wetu,kuna walimu wengi sana waliotumia vyeti feki na pia kutumia majina ya watu kupata nafasi za ualimu hawa ndio wauaji wa kwanza kabisa wa watoto wetu.
b--Kufutwa kwa mitihani ya darasa la nne na kidato cha pili,hapa napo pameongza balaa kubwa sana maana wanafunzi wanafundishwa na walimu wabovu halafu wanapitishwa bila mitihani ya darasa la nne na kidato cha pili unategemea hapa patapatikana wanafunzi wa aina gani?
c--Kubadilishwa kwa mitaala bila mpangilio na kufuta au kuunganisha baadhi ya masomo mfano kuna wanafunzi wa hapa hapa nchini hawakuwahi kusoma Physics,Chemistry na Biology haya masomo yalichanganywa sijui yakaitwa nini sijui,kufutwa kwa masomo ya ufundi kwenye shule za ufundi kama Tanga Tech,Moshi Tech,Mtwara Tech,Ifunda Tech,kufutwa kwa masomo ya Commerce na Bookkeeping hii ilitoka kipindi cha Mh Mungai
d--Kupuuzwa kwa Madai ya walimu,hapa ndio panatisha kabisa,hasa kwenye shule za kata na za serikali,hembu jiulize mwalimu ambae amefoji cheti/ametumia jina la mtu,hajui vizuri kufundisha,kugoma anaogopa maana akigoma hapati kazi sehemu nyingine yoyote anaamua kupiga magumashi darasani halafu anakata mitaa kwenda kutafuta pesa ya ziada unategemea nini hapo zaidi ya sifuri tu?
===>Wana JF naamini wahusika wanayaona haya,huyu mama Ndalichako anaonewa tu,amekataa kudhalilisha Phd yake,nafikiri kwa watendaji wengine kuna cha kujifunza hapa,Tumia elimu yako kuisadia nchi hii,sio kuwasaidia wanasiasa kuendelea kututilia vilema vya akili watoto wetu,wasomi wetu msitusaliti na wala msiwasaliti watanzania wenzenu kuweni majasiri wa kukataa kufanya mambo ambayo hayana tija kwa taifa hili.