Mpangaji mwenzangu ni mtu mbaya

Mpangaji mwenzangu ni mtu mbaya

Washawasha

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2006
Posts
16,948
Reaction score
13,378
Habari zenu?
Ni hivi nina wachumba wawili tofauti,sasa juzi kaja mchumba wangu Asha na ndugu yake kuja kunitembelea mara mpangaji mwenzangu naye akaja basi tukapiga stori zetu na kupata chakula na vinywaji vya hapa na pale,baada ya hapo mpangaji mwenzangu akaenda kwake na mchumba wangu na ndugu yake nao nikawasindikiza wakaenda kwao.
Jana kaja mchumba wangu Joyce nikamwacha nyumbani na mimi nikatoka kidogo kuna mtu nilikwenda kumuona kumbe yule mpangaji mwenzangu alirudi na kuanza kumwambia huyu mchumba wangu Joyce kuwa ametokea kumpenda yule dada yake aliyekuja naye jana,basi Joyce alimuhakikishia kwamba sio yeye aliyekuja jana ila huyu mpangaji mwenzangu aliendelea kumwuomba amuunganishe na yule dada yake ndipo Joyce akamwambia sio yeye aliyekuja jana na akataka amwambie ni mwanamke gani huyo aliyekuja na rafiki yake pale kwangu? Baada ya kuona hivyo yule mpangaji mwenzangu akatoka bila kuaga,ile kurudi nikakutana na zogo hili na Joyce kaondoka huku amekasirika na kusema nikimwita basi nimuandalie majibu yaliyonyooka.Mpangaji mwenzangu hakulala kwake na hajarudi mpaka sasa,
Nimepanga kumfanyia kitu mbaya huyu mpangaji mwenzangu,
je,nimtende au nisimtende?
Nalog off
 
​Usiishie lupango tu, hasira hasara.
Lupango sintokwenda kwa kweli maana najianda na kuziziba njia zote zitakazonifanya nipelekwe lupango.
Nalog off
 
Mhhhh!!! Umeziziba njia zote halafu umejianika hapa jamvini!!!! Kama hao unaowazungumzia nao ni wanachama hapa wameshajumlisha 1 na 1 na kupata jibu. Hivyo umeshajichoresha hapa jamvini lolote litakalotokea dhidi ya huyo mpangaji mwenzio watakuja kukusomba mzobemzobe.

Lupango sintokwenda kwa kweli maana najianda na kuziziba njia zote zitakazonifanya nipelekwe lupango.
Nalog off
 
Akili ni nywele na kila mtu ana zake. Sasa kila atakae haribu mambo yako ya kuwa na gf wengi utamfanyia 'kitu mbaya'?. Angalia kitu mbaya usije ukafanyiwa wewe.
 
Sasa wewe ndio majanga maana huna akili. Una wapenzi wengi halafu wote unawaleta nyumbani kwanini.
Next watakufumania wote.
 
Mhhhh!!! Umeziziba njia zote halafu umejianika hapa jamvini!!!! Kama hao unaowazungumzia nao ni wanachama hapa wameshajumlisha 1 na 1 na kupata jibu. Hivyo umeshajichoresha hapa jamvini lolote litakalotokea dhidi ya huyo mpangaji mwenzio watakuja kukusomba mzobemzobe.
Dah! kweli nimebugi ila niitaendelea kuangalia ni jinsi gani naweza kumaliza naye au ndio wewe nini mpangaji mwenzangu?
Nalog off
 
Akili ni nywele na kila mtu ana zake. Sasa kila atakae haribu mambo yako ya kuwa na gf wengi utamfanyia 'kitu mbaya'?. Angalia kitu mbaya usije ukafanyiwa wewe.
Akiniharibia lazima alipe tu.
Nalog off
 
Sasa wewe ndio majanga maana huna akili. Una wapenzi wengi halafu wote unawaleta nyumbani kwanini.
Next watakufumania wote.
Mazingira ya kufumaniwa nimeyaziba hawatoweza kunifumania.
Nalog off
 
Mtoa mada pimbi tu mshenzi wa tabia unageuza nyumba za kupanga danguro ningemjua mwenye nyumba ako ningemwambia akupe notisi mapema! Ndo mnaoharibu watoto wetu ngoja nimalizie mjengo wangu
 
Mtoa mada pimbi tu mshenzi wa tabia unageuza nyumba za kupanga danguro ningemjua mwenye nyumba ako ningemwambia akupe notisi mapema! Ndo mnaoharibu watoto wetu ngoja nimalizie mjengo wangu
KKkkkkkk acha roho mbaya kaka,akinipa notisi nitasumbuka kupata mjengo mzuri kama ule.
Nalog off
 
Concern:
Wachumba wawili wanini mkuu? Au dini inakuruhusu kuoa zaidi ya mmoja!?
Ushauri:
1. Hasira hasara na kujichukulia hatua mkononi pia si ruhusa na si busara kwa usalama wako na yeye pia.
2. Rekebisha mahusiano yako na hao. Nijuavyo mimi mchumba ni yule ambaye unajiandaa kumuoa au kuolewa naye. Sasa hapo unajiandaa kumuoa yupi, na umejiandaaje kuikabili disappointment ya utakayemuacha.? Siulizi ili unijibu bali ufikirie upya..kisha wahenga walisemaa..KIJUA NDIO HIKI, USIPOANIKA UTATWANGA MBICHI.
3. Upande mwingine mpangaji wako pengine katumia njia hiyo kukusaidia ku-deal na namba mbili yangu hapo juu.
 
Back
Top Bottom