Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,997
Baada ya serikali ya CCM kuwalea na kuwadekeza wezi wa mali zetu; baada ya serikali hiyo kuremburiana macho na mafisadi kwa miongo kadhaa sasa; baada ya kuonesha woga na kutokujiamini mbele ya wale wanaotufanya tuwe duni mbele zao sasa nasema imetosha!
Kama vile utungu wa mama kuzaa nchi yetu ndio imefika na wakati wa mwana kuzaliwa lazima iwe mwaka huu kwani hatuwezi kuendelea kupiga kambi kuzungumzia watu wale wale miaka mitatu sasa! Na wengine tumewazungumzia miaka 10 sasa.
Kuna kundi la Wananchi ambao uzalendo wao ulishawatoka siku nyingi na kwa muda mrefu wamebakia kufurahia mali za nchi yetu. Kundi hili linaendelea kutaka kutawala bila kuhojia au kupigiwa kelele. Wanataka wawe kama yule anayekula kisicho chake na hata ukitaka kupiga kelele anakunyoshea kidole na kukuambia 'shssssssss' Kwamba wewe muibiwa usipike kelele badala yake umuombe aache kula!
imetosha. Kuna kundi la watu ambao ni lazima wachukuliwe hatua au milele tunaweka kwenye notisi kuwa mbele zenu hatugwai na katika altare zenu za ufisadi hatupigi magoti. Tunawashuhudia wale ambao wanatetemeka mbele zenu ambao leo wanajitokeza kuwatetea ati kwa misingi ya "kufuata haki"! Je mlipovunja haki za wananchi wa tAifa hili kuishi katika neema mbona hamkutetea? Mlipogawiana mali ya wana na mabinti wa taifa hili kama urithi wa kizazi chenu mbona hamkupigiwa kelele! Sasa yatosha.
Wafuatao nawatangaza daima kuwa ni maadui wa Tanzania na maslahi yake. Ni maadui wa maendeleo yetu na mmoja mmoja na kama kundi wanaleta mbele yetu hatari iliyo wazi na dhahiri. Kundi la watu hawa wanatakiwa waogopwe makampuni yao yasusiwe na miradi yao isusiwe daima!
1. Benjamin William Mkapa
2. Rostam Aziz
3. Apson Mwang'onda
4. Yusuph Manji
5. Gen (mstaafu). Robert Mboma
5. Vincent Mrisho
6. Anna Mkapa
7. Andy Chande
8. Andrew Chenge
9. Nimrod Mkono
10. Yeyote anayewaunga mkono, kuwatetea, kuwasafisha au kuwaita ni watu safi!
Na kutoka na kundi hilo ushirika wao wa uovu umetandaa kila kona na sekta ya nchi yetu. Ni kundi hili na makuwadi wao wanatufanya tuishi kama wageni katika nchi yetu na majina yao yatajwapo tunatakiwa kutetema kama mitete!
Watu hawa na wale wengine ambao tayari wanajulikana ndio kwa kiwango cha juu kabisa wamefunya urithi wetu kuwa asili ya utajiri wao. Wametumia upole na ukimya wetu kututisha na sasa wanajiandaa kutumia nguvu ya dola ambayo wao wameitengeneza kulinda maslahi yao ili kututisha na kutunyamazisha.
Mara moja na daima nakataa milele kutetemeka mbele ya kundi hili na wapambe wao. Nakataa kufumba macho mambo waliyoyafanya katika Taifa hili na kuogopa hata kuwataja majina ati kwa vile "ni viongozi fulani". Laana hiyo ya woga iwaendee makuwadi wao na uzao wao!
I dare you to sue me!! Please do in any court.. here in the US or at home and I'll come on my own.. .. ukitaka kujua ni nani wa kumsuu.. give me your number I'll call you and give you all my information to assist you. You have to be one of the named siyo wapambe wao!
Kama vile utungu wa mama kuzaa nchi yetu ndio imefika na wakati wa mwana kuzaliwa lazima iwe mwaka huu kwani hatuwezi kuendelea kupiga kambi kuzungumzia watu wale wale miaka mitatu sasa! Na wengine tumewazungumzia miaka 10 sasa.
Kuna kundi la Wananchi ambao uzalendo wao ulishawatoka siku nyingi na kwa muda mrefu wamebakia kufurahia mali za nchi yetu. Kundi hili linaendelea kutaka kutawala bila kuhojia au kupigiwa kelele. Wanataka wawe kama yule anayekula kisicho chake na hata ukitaka kupiga kelele anakunyoshea kidole na kukuambia 'shssssssss' Kwamba wewe muibiwa usipike kelele badala yake umuombe aache kula!
imetosha. Kuna kundi la watu ambao ni lazima wachukuliwe hatua au milele tunaweka kwenye notisi kuwa mbele zenu hatugwai na katika altare zenu za ufisadi hatupigi magoti. Tunawashuhudia wale ambao wanatetemeka mbele zenu ambao leo wanajitokeza kuwatetea ati kwa misingi ya "kufuata haki"! Je mlipovunja haki za wananchi wa tAifa hili kuishi katika neema mbona hamkutetea? Mlipogawiana mali ya wana na mabinti wa taifa hili kama urithi wa kizazi chenu mbona hamkupigiwa kelele! Sasa yatosha.
Wafuatao nawatangaza daima kuwa ni maadui wa Tanzania na maslahi yake. Ni maadui wa maendeleo yetu na mmoja mmoja na kama kundi wanaleta mbele yetu hatari iliyo wazi na dhahiri. Kundi la watu hawa wanatakiwa waogopwe makampuni yao yasusiwe na miradi yao isusiwe daima!
1. Benjamin William Mkapa
2. Rostam Aziz
3. Apson Mwang'onda
4. Yusuph Manji
5. Gen (mstaafu). Robert Mboma
5. Vincent Mrisho
6. Anna Mkapa
7. Andy Chande
8. Andrew Chenge
9. Nimrod Mkono
10. Yeyote anayewaunga mkono, kuwatetea, kuwasafisha au kuwaita ni watu safi!
Na kutoka na kundi hilo ushirika wao wa uovu umetandaa kila kona na sekta ya nchi yetu. Ni kundi hili na makuwadi wao wanatufanya tuishi kama wageni katika nchi yetu na majina yao yatajwapo tunatakiwa kutetema kama mitete!
Watu hawa na wale wengine ambao tayari wanajulikana ndio kwa kiwango cha juu kabisa wamefunya urithi wetu kuwa asili ya utajiri wao. Wametumia upole na ukimya wetu kututisha na sasa wanajiandaa kutumia nguvu ya dola ambayo wao wameitengeneza kulinda maslahi yao ili kututisha na kutunyamazisha.
Mara moja na daima nakataa milele kutetemeka mbele ya kundi hili na wapambe wao. Nakataa kufumba macho mambo waliyoyafanya katika Taifa hili na kuogopa hata kuwataja majina ati kwa vile "ni viongozi fulani". Laana hiyo ya woga iwaendee makuwadi wao na uzao wao!
I dare you to sue me!! Please do in any court.. here in the US or at home and I'll come on my own.. .. ukitaka kujua ni nani wa kumsuu.. give me your number I'll call you and give you all my information to assist you. You have to be one of the named siyo wapambe wao!