Mpaka sasa sijui sababu ya kuachwa

Mpaka sasa sijui sababu ya kuachwa

Jamaa hana bahati kweli.. anampata dem cash madam bado anamuacha kirais rais hivyo nimeamini upele humkuta asiye na kucha.
 
angekuja naye aongee kuhusu wewe, unaweza ukaona wewe ndo chanzo cha matatizo japo hujijui
Sasa kama simu hataki kupokea , tuongee tatizo ni nini nitajuaje kama mie ndio chanzo
Kwa kifupi alijipanga kufanya aliyonifanyia
 
Sikua cash madam, ila nilijua yeye ndio mwenzangu na matatizo hayana mmoja
Leo kwake kesho kwangu hivyo nilikua najidhiki nilichonacho nampa ili tufichiane aibu ndogondogo

Cha msingi wew anza upya mbona wanaume tupo wengi sana. Kwani wew wa kwanza kutoa kipochi manyoya na usiolewe naye. Swali la uzushi hiv huyo ni boyfriend wako wa kwanza eeehhh yan hauna experiences na sisi wanaume? Na haujawahi face songombingo kama hizo.
 
Kwanza nasikitika kwa mawazo yako dada yangu, labda nikupe elimu hii ndogo juu ya kufiwa na maombolezo

Sikuungi mkono adhima yako ya kutaka mkomoa mwenzio kwa sababu;
1. Hajadhamiria
2. Kafiwa mara mbili

Turudi kwenye elimu.

Ipo hivi kwa wastani ni inamchukua miaka miwili mwanadamu kukamilisha maombolezo (kiimani) nikiwa na maana kuwa roho za wawili hao kuweza kutengana na kuamua kuendelea na maisha mengine.

Kwani hujawai kuona mtu kafiwa na mke au mpenzi akakosa hamu ya kujamiiana kwa hadi miaka miwili?, sasa ndio sawa na huyu mwenzako kumbuka kafiwa na mama yake mzazi na pia bado kafiwa na babu mzaa mama ndani ya mwaka mmoja.

Nikuulize swali, je ulikuwa unamfahamu mama yake na mwenzio?, na je, unafikiri mwenzio hakuwa amemwambia mama yake malengo yake kwako kama wewe ulivyomshirikisha mama yako?

Imagine ndio wewe mama yako angefariki, unajua kuwa ungeumia sana kukumbuka kuwa mama yako hataweza kushuhudia ndoa yako na umpendaye?

Dada yangu jirudi upya na urudishe upendo kwa huyu kijana, tambua kuwa bado yupo kwenye maombolezo na wewe ndio mtu sahihi ambaye ungempunguzia muda wa maombolezo kwa kuifanya roho yake iwe bize kwako.

Ingekuwa labda amechepuka ungekuwa na haki ya hizi lawama ila hivi amepata matatizo una hizi lawama jichunguze upya jitathimini na ujiulize ni wapi umeitoa hii hali ya kutokuwa na huruma.

Mungu si Athuman dada yangu unaweza jikuta umepata pigo kubwa kuliko huyu kijana pengine hata ukawapoteza wazazi wote wawili kwa mpigo alafu upo na mhuni atakayekutosa hapo hapo utalia na kusaga meno ukimkumbuka huyu jamaa ambaye wakati huo atakuwa karibu na wewe ila ndio hivyo ameshaoa mwanamke mwingine na ana familia yake. BEWARE my sister.
 
@SweetieLee,We Dada Umeongea Point tupu.. Hongera kwa kua na upeo Mkubwa wa kuchanganua Mambo
 
Mgeni wa Jiji,

Nashukuru kwa ushauri mkuu, naomba niuchukue kama ulivyo
Kuhusu mama yake alikua anatambua malengo yetu kila tulichofanya yeye alikua anajua
Shida inakuja ama napata doubts kwamba mbona pale pale alivyofiwa misiba yote hiyo alikua kawaida tunawasiliana kama kawaida iweje ssa hivi aniwekee ukuta wa mawasiliano

Kingine mie pia nilifiwa na babu yangu hakuhudhuria msiba wala arobaini na alisema nitakuja kwenye arobaini siku aliyosema anakuja nampigia hakupokea wala kujibu txt mpk leo

Pengine nakosea kumuhukumu ila nahisi pengine anatumia changamoto hizi kama kichaka cha kujifichia
Mie pia nachoka naanzaje kumtafuta kwa mazingira hayo
Msaada wako mkuu
 
Cha msingi wew anza upya mbona wanaume tupo wengi sana. Kwani wew wa kwanza kutoa kipochi manyoya na usiolewe naye. Swali la uzushi hiv huyo ni boyfriend wako wa kwanza eeehhh yan hauna experiences na sisi wanaume? Na haujawahi face songombingo kama hizo.
Hata sio wa kwanza
Sina experience na haya ninayopitia
 
Change your lifestyle, means kuanzia mavazi, kama unasuka kata nywele ziwe fupi, pendeza kweli kweli jiachie u-relax sawa tena ikiwezekana nenepa, ila usimpige vijembe kwenye status za whatsapp. Ataumia kweli kweli tena ataomba mrudiane maana wanaume ndy walivyo ndg.
 
mtakahela,

Pole mkuu sasa umeweka habari vizuri zaidi, hapa nitakuuliza maswali machache yatakayosaidia kukupa mwanga wa hatma yenu

1. Vipi huyu mwenzako anao ndugu wa karibu unaowasiliana nao au uliokuwa unawasiliana nao mf. Wadogo zake au mkubwa wake

Kama ulikua/unawasiliana na ndugu zake wao wanamuongeleaje ndugu yao je mabadiliko aliyonayo ni kwako tu au kwenye kila nyanja ya kimaisha (amepoteza dira ya maisha?) kama amepoteza dira ya maisha basi jua tatizo ni kubwa unapaswa kumsaidia kurudi kuwa kawaida

Ila pia kama amepoteza dira kwako pekee hili ni tatizo kubwa zaidi (kwa uhusiano wenu) na utalijua hili kupitia ndugu zake kama wanakwepa kukwambia wazo la ndugu yao juu ya hatma yenu basi jua labda mpo wawili au zaidi au pia huwenda ameamua kutokuoa kabsa baada ya maswahibu yaliyotokea.

Wanadamu tupo tofauti sana ila kwa ukubwa naona huyu mwenzio amepata matatizo ya kimtazamo unajua anaweza kuwa hakuja kwenye msiba kwenu kutokana na hofu ya kukumbuka aliyoshuhudia kwenye msiba wa mama yake na mbaya zaidi ukute alikuwa ndio anayemuuguza wanaume ni very week emotionally ila wengi hawajui hili.
 
Mgeni wa Jiji,

Ahsante mkuu,
Ndugu zake wakaribu ninao wasiliana nao sana ni shangazi zake
Na pia sijawahi kuwadokezea kuhusu mabadiliko ya mtoto wao.
 
Muachie mungu tu maana hata ukilipiza hutapata kitu.
"revenge isn't a passion,it's a disease,it eats at your mind and poisons your soul."
 
Back
Top Bottom