Moyo una mengi

Moyo una mengi

Kukusaidia kwetu wajibu,
Kwa maswali yaso majibu,
Elezea yanayo kusibu,
Waungwana tuweze kujibu

Fukuto Kama motoni,
Kubeba kero moyoni
Furaha tele usoni
Machungu tosha rohoni

We toa yanayokuchoma,
Waungwana tutakusoma
Ushauri bila kukoma
Uchungu upate kukoma
:: Nitetee Mola Wangu


1 Nitetee Mola wangu
Wewe kimbilio langu
Duniani sina changu

2 Hali yangu vangu vangu
Nikulacho ni kichungu
Nimejawa naukungu

3 Siku ya tatu sijala
Na bado ni masajala
Nakesha kwenye jalala

4 Kuyaokota makopo
Ningeupata mkopo
Au ja kazi ya popo

5 Maisha yangu ni duni
Sina kitu mfukoni
Uzito upo kitwani

6 Muda wote ni majozi
Nacheka yaja machozi
Vitamu kwangu ni njozi

7 Njoo wangu muokozi
Nsije fanya udokozi
Kifo kiwe yangu dozi

[emoji2399] Abuuabdillah[emoji1607]
Ibn Kimweri
 
Ni utenzi ama kweli?
Nipa Neema Wadudi


1 Umenishika utungu, Matozi ndani ya maji
Menichoma nungunungu, ninakosa mfariji
Sijui ni lepi fungu, wala sinalo taraji

2 Yanisakama mawazo, usiku kesha silali
Kila yaumi vikwazo, mwisho ungali umbali
Lini nipate tulizo, hakunapo afadhali

3 Ati kukua ni huku, dunia mejaa tabu
Nakula kwa chukuchuku, ambwa natiwa adabu
Napeza kula makuku, ninenepe kama dubu

4 Naenda huku na kule, ila bado yale yale
Amara hii na ile, halitoshi lake bale
Sipati japo uwele, nifurahi nami nile

5 Madeni tele yan'zidi, ulimwengu masumbuko
Nipa neema Wadudi, fuadini machubuko
Mola sijamkaidi, ingali ni sokomoko

[emoji2399]Abuuabdillah[emoji3578]
0744883353
 
Back
Top Bottom