Moyo Ulioonja Maumivu

Moyo Ulioonja Maumivu

Mi ngoja nisherehekee mwaka kwanza.
Kesho ntarudi hapa,napata tabu kukubali hiyo 50/50
Mbona hata wanawake wanaoumiza bila sababu wapo wengi tu ... " hii mada ukitaka ui-jadili kwa fact unapaswa kuweka mbali mahaba ya kijinsia ya jinsia yako kando kwanza ... kisha uanze kuzitazama hizi changamoto zinazo sababishwa na hizi jinsia zote 2 katika Jamii .. ndio utakubaliana na mimi .. kinyume na hapo ..utaishia kubishana tu mkuu ..without logic consistent ...

Mkuu wanaume huwa tunaumizwa sana " ila huwa tunaficha" kwa sababu hatutaki kuonekana kuwa sisi ni viumbe dhaifu .. na ndio huwa tunakufa mapema pia kwa sababu huwa tuna ubebesha moyo mambo mengi ambayo mwisho wa siku huwa yanalipuka na kuzalisha maradhi na kuathiri mfumo mzima wa uzalishaji kinga za mwili .(hili haswaa huwa linachangiwa na uwepo wa stress za muda mrefu baada ya kufanyiwa ndivyo sivyo " na nyinyi "

Narudi kwenye msimamo wangu "

Men lier " Woman lier hakuna mwenye nafuu mkuu "

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 59

“Halo meneja! Nipo na mke wangu, sidhani kama nitatoka,” alisema Theo hata kabla ya meneja wake kuongea kitu chochote kile.

“Theo! Una uhakika upo na mkeo?” aliuliza meneja, kwa jinsi alivyouliza, alionekana kama mtu aliyeonekana kukasirishwa.

“Ndiyo! Kuna nini? Mbona umeuliza kana kwamba huniamini?” aliuliza Theo.
“Umeingia Instagram?”

“Hapana!” “Hebu ingia kwanza halafu utaniambia kama upo na mkeo nyumbani ama la,” alisema meneja na kukata simu.
Theo akashtuka, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea ila hilo halikuwa tatizo.

Akainuka na kukaa kitako kitandani kisha kuingia Instagram.
Kwa sababu kulikuwa na watu wengi waliokuwa wameiposti picha ya mke wake, moja kwa moja macho yake yakatua kwa Violeth akiwa hospitalini huku uso wake ukiwa umelowanishwa na machozi.

Kwa jinsi alivyoonekana ilikuwa rahisi kugundua kwamba alichanganyikiwa. Hakujua ni kitu gani kilitokea lakini kwa namna ambavyo mwanamke huyo alivyokuwa, ilimpa picha kulikuwa na jambo baya.

Haraka sana akatoka Instagram na kumpigia simu mke wake, haikuwa ikipokelewa, bila shaka iliachwa nyumbani. Alihitaji kujua ni mahali gani alipokuwa, akaingia tena na kusoma comments za watu kuhusu picha hizo.

Zilimtia hasira kwa sababu nyingi zilikuwa ni za kumzungumzia yeye kwamba alimtelekeza mke wake, alimwacha hospitalini wakati akimuuguza mtoto wao.
“Hospitalini? Akimuuguza mtoto wetu?” alijiuliza Theo huku akionekana kuchanganyikiwa.

Hapo akapata jibu ya kile kilichokuwa kikiendelea, alimkumbuka daktari alipomwambia kwamba mtoto wao alikuwa na tatizo katika moyo wake, tatizo ambalo lingemfanya kupata matatizo muda wowote ule hivyo hakutakiwa kumwambia mke wake.

Moyo wake ulimchoma, aliendelea kusoma na kugundua kwamba alikuwa katika Hospitali ya Dk. Mjuni iliyokuwa Mbezi Beach jijini Dar es Salaam. Hakutaka kuchelewa, hapohapo akasimama, akavaa nguo.

“Unakwenda wapi?” aliuliza Iyanya huku akimwangalia Theo.
“Mke wangu! Namuwahi mke wangu!” alisema Theo.

“Ila mimi ni zaidi ya mkeo kumbuka,” alisema Iyanya.
 
SEHEMU YA 60

Theo hakutaka kuongeza kitu chochote kile, alichokifanya ni kuondoka na kuelekea huko hospitalini. Ndani ya gari alichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya.

Moyo wake ulimpenda mno Violeth, alikumbuka jinsi mwanamke huyo alivyokuwa mzuri, alivyohangaika kumpata, hakutakiwa kumfanyia yote hayo aliyokuwa akimfanyia.

Alisikia hukumu nzito moyoni mwake, aliendesha gari kama kichaa mpaka alipofika hapo hospitalini ambapo moja kwa moja akaelekea ndani, tayari waandishi wa habari walikuwa wamekwishafika tayari kwa kuchukua matukio ya kila kitu kilichokuwa kikiendelea.

Walipomuona Theo, wakaanza kumpiga picha huku wengine wakimsogelea kwa lengo la kuongea naye. Siku hiyo alikuwa mkali kama mbogo, alichanganyikiwa, kitendo cha mtoto wake, Rachel kupelekwa hospitalini pale kilionyesha kabisa hali haikuwa nzuri, na kama angeleta masihara basi wangeweza kumpoteza.

Daktari alipomuona tu, akamsogelea, akamsalimia na kumchukua kuelekea katika chumba alichokuwa mke wake na mtoto, akaingia ndani, macho yake yalipotua kwa Violeth, machozi yakaanza kumtoka moyoni mwake, hakuamini pamoja na uzuri wa mke wake, jinsi alivyompenda leo hii alikuwa akimsaliti.

Haraka sana Violeth alipomuona mume wake, akasimama na kumsogelea kisha kumkumbatia na kuanza kulia tena huku akimwambia kwamba Rachel alikuwa akienda kufa kwa picha ile iliyokuwa kitandani ilimuumiza mno.

“She is going to die...she is going to die,” (atakufa...atakufa...) alisema Violeth huku akilia kifuani mwa Theo.
 
Shangazi nitaftie Theo nna matusi yake mengi sn
Nakusalimia Heri ya mwaka mpya mama kheri na baraka kwako na familia.
SEHEMU YA 59

“Halo meneja! Nipo na mke wangu, sidhani kama nitatoka,” alisema Theo hata kabla ya meneja wake kuongea kitu chochote kile.

“Theo! Una uhakika upo na mkeo?” aliuliza meneja, kwa jinsi alivyouliza, alionekana kama mtu aliyeonekana kukasirishwa.

“Ndiyo! Kuna nini? Mbona umeuliza kana kwamba huniamini?” aliuliza Theo.
“Umeingia Instagram?”

“Hapana!” “Hebu ingia kwanza halafu utaniambia kama upo na mkeo nyumbani ama la,” alisema meneja na kukata simu.
Theo akashtuka, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea ila hilo halikuwa tatizo.

Akainuka na kukaa kitako kitandani kisha kuingia Instagram.
Kwa sababu kulikuwa na watu wengi waliokuwa wameiposti picha ya mke wake, moja kwa moja macho yake yakatua kwa Violeth akiwa hospitalini huku uso wake ukiwa umelowanishwa na machozi.

Kwa jinsi alivyoonekana ilikuwa rahisi kugundua kwamba alichanganyikiwa. Hakujua ni kitu gani kilitokea lakini kwa namna ambavyo mwanamke huyo alivyokuwa, ilimpa picha kulikuwa na jambo baya.

Haraka sana akatoka Instagram na kumpigia simu mke wake, haikuwa ikipokelewa, bila shaka iliachwa nyumbani. Alihitaji kujua ni mahali gani alipokuwa, akaingia tena na kusoma comments za watu kuhusu picha hizo.

Zilimtia hasira kwa sababu nyingi zilikuwa ni za kumzungumzia yeye kwamba alimtelekeza mke wake, alimwacha hospitalini wakati akimuuguza mtoto wao.
“Hospitalini? Akimuuguza mtoto wetu?” alijiuliza Theo huku akionekana kuchanganyikiwa.

Hapo akapata jibu ya kile kilichokuwa kikiendelea, alimkumbuka daktari alipomwambia kwamba mtoto wao alikuwa na tatizo katika moyo wake, tatizo ambalo lingemfanya kupata matatizo muda wowote ule hivyo hakutakiwa kumwambia mke wake.

Moyo wake ulimchoma, aliendelea kusoma na kugundua kwamba alikuwa katika Hospitali ya Dk. Mjuni iliyokuwa Mbezi Beach jijini Dar es Salaam. Hakutaka kuchelewa, hapohapo akasimama, akavaa nguo.

“Unakwenda wapi?” aliuliza Iyanya huku akimwangalia Theo.
“Mke wangu! Namuwahi mke wangu!” alisema Theo.

“Ila mimi ni zaidi ya mkeo kumbuka,” alisema Iyanya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
pole Violeth
SEHEMU YA 60

Theo hakutaka kuongeza kitu chochote kile, alichokifanya ni kuondoka na kuelekea huko hospitalini. Ndani ya gari alichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya.

Moyo wake ulimpenda mno Violeth, alikumbuka jinsi mwanamke huyo alivyokuwa mzuri, alivyohangaika kumpata, hakutakiwa kumfanyia yote hayo aliyokuwa akimfanyia.

Alisikia hukumu nzito moyoni mwake, aliendesha gari kama kichaa mpaka alipofika hapo hospitalini ambapo moja kwa moja akaelekea ndani, tayari waandishi wa habari walikuwa wamekwishafika tayari kwa kuchukua matukio ya kila kitu kilichokuwa kikiendelea.

Walipomuona Theo, wakaanza kumpiga picha huku wengine wakimsogelea kwa lengo la kuongea naye. Siku hiyo alikuwa mkali kama mbogo, alichanganyikiwa, kitendo cha mtoto wake, Rachel kupelekwa hospitalini pale kilionyesha kabisa hali haikuwa nzuri, na kama angeleta masihara basi wangeweza kumpoteza.

Daktari alipomuona tu, akamsogelea, akamsalimia na kumchukua kuelekea katika chumba alichokuwa mke wake na mtoto, akaingia ndani, macho yake yalipotua kwa Violeth, machozi yakaanza kumtoka moyoni mwake, hakuamini pamoja na uzuri wa mke wake, jinsi alivyompenda leo hii alikuwa akimsaliti.

Haraka sana Violeth alipomuona mume wake, akasimama na kumsogelea kisha kumkumbatia na kuanza kulia tena huku akimwambia kwamba Rachel alikuwa akienda kufa kwa picha ile iliyokuwa kitandani ilimuumiza mno.

“She is going to die...she is going to die,” (atakufa...atakufa...) alisema Violeth huku akilia kifuani mwa Theo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi ngoja nisherehekee mwaka kwanza.
Kesho ntarudi hapa,napata tabu kukubali hiyo 50/50

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaa kama haukubali shauri yako ...ila kama nimfuatililiaji mzuri wa mikasa inayo ufika huu ulimwengu kwa kupitia hizi jinsia mbili basi utanielewa tu ...

Kwa nyinyi watu wa imani mnavisa kibao tu ambavyo viko wazi " .... Adamu+eva+shetani=tunda la dhambi ... eva ndiye aliyekuwa sababu ya kupokea ushawishi toka kwa shetani .. ushawishi uliopelekea balaa kubwa mpaka leo hii ...(watu wa imani mnaamini hivi)

Samson na delila ( najua unajua kisa chake)
Malkia creopatra( wa misri )na Julio Cesar ' nadhani itakuwa umesikia kisa chake ...

Hayo nimekutajia matukio yale maarufu zaidi duniani ambayo yapo mpaka kwenye vitabu vya imani na vya history"

Achilia mbali haya matukio ya kawaida ya kina Irene uwoya na marehemu ndikumana"

Wema sepetu na kanumba
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom