Moyo Ulioonja Maumivu

Moyo Ulioonja Maumivu

SEHEMU YA 57

Kama kulia, Violeth alilia sana, moyo wake ulimuuma kupita kawaida, alikaa kwenye kiti pembeni ya kitanda alicholazwa mtoto wake huku akimwangalia tu.
Mpira wa kumpelekea hewa safi ulikuwa mdomoni na puani mwake. Pale alipokuwa mtoto Rachel alitia huruma mno na kila muda ambao Violeth alikuwa akimwangalia, alikuwa akilia tu.

Moyo wake ulichoma kama pasi, hakumkumbuka mume wake, alichanganyikiwa, alikuwa akipambana peke yake kana kwamba hakuwa na mume. Alimpenda mtoto wake, kwake, alikuwa tayari kupoteza kila kitu akiwemo Theo lakini si kumkosa Rachel.

Wakati akiwa humo, tayari kulikuwa na watu walikwishampiga picha kwa lengo la kuziweka kwenye mitandao ya kijamii. Mwanamke huyo alikuwa maarufu mno, habari yake ilikuwa dili kubwa kila kona, kulikuwa na watu wengi ambao walikuwa wakitumwa kwenda sehemu mbalimbali kumtafuta na kupeleka stori lakini hawakuweza kumpata.

Kitendo cha picha hizo kupeostiwa kwenye mitandao ya kijamii kila mmoja aliyeziona alichanganyikiwa, hakukuwa na aliyeamini kwamba yule mwanamke aliyekuwa amevaa nguo ya kulilalia huku uso wake ukiwa umelowanishwa na machozi alikuwa Violeth.

Alikuwa kwenye masikitiko makubwa, watu waliambiwa kwamba alikuwa hospitalini na mtoto wake ambaye alikuwa ameumwa ghafla usiku huo.

Ilikuwa ni vigumu sana kumuona akiwa peke yake, watu wakaanza kuhoji kuhusu Theo, alikuwa wapi wakati huo na wakati alikuwa nchini Tanzania?

Hilo likaanza kujenga picha mbaya kwa kila mtu aliyekuwa akimuona mwanamke huyo akiwa peke yake pale alipokuwa. Watu wakahisi kwamba wawili hao inawezekana walikuwa kwenye ugomvi mkubwa na hawakutaka watu wajue.

“Lakini ishu ya mtoto ni ya wote,” alisema jamaa mmoja huku akiwa ameshika simu yake ambayo alifungua akaunti yake ya Instagram na kuanza kuangalia picha hizo.

Hilo ndilo lilikuwa gumzo, ilikuwa ni saa tano usiku lakini kila mmoja alikuwa na simu yake mkononi kana kwamba ilikuwa mapema kabisa.
 
SEHEMU YA 58

Watanzania wengi waliopenda umbeya muda huo walitaka kukesha kama popo, walikuwa wakilijadili jambo hilo kwa mapana zaidi kwani kwa kile kilichokuwa kimetokea, kiliwaumiza kwa sababu tu huyo Violeth alikuwa mwanamke aliyetulia na kujiheshimu ambaye hakutaka kufuatilia maisha ya mtu yeyote yule.

Muda huohuo Theo alikuwa hotelini akiendelea kula raha na Iyanya, moyo wake ulikuwa na furaha kubwa, kila alipomwangalia msichana huyo, kwa jinsi alivyoumbika na kiwowowo chake cha kizushi kikamchanganya zaidi.
Ilipofika majira ya saa sita usiku, wakamaliza hivyo kukaa kitandani na kuanza kupiga stori.

Mwanaume huyo alimwambia Iyanya ukweli wa moyo wake kwamba alimpenda, hakukuwa na mwanamke zaidi yake, alimpenda zaidi ya mke wake, alimpenda zaidi ya mtu yeyote yule katika dunia hii.

“Why don’t you divorce your wife and marry me?” (kwa nini usimpe talaka mkeo na unioe mimi?) aliuliza Iyanya.
“No! It that won’t happen,” (hapana! Hilo haliwezi kutokea)

“Then you don’t love me,” (basi hunipendi)
“I love you Iyanya! I really love you,” (nakupenda Iyanya! Nakupenda mno)

“Why don’t you want to diveorce your wife for me?” (kwa nini hutaki kumpa talaka mkeo kwa ajili yangu?) aliuliza msichana huyo.

“We are christians! Things don’t work that way.” (sisi ni Wakristo! Mambo hayafanywi hivyo) alisema Theo huku akimwangalia msichana huyo.

Akamsogelea na kumkumbatia. Alimwambia kwamba hata kama hatompa talaka mkewe bado angempenda mpaka kifo chake na kusingekuwa na kitu chochote kile ambacho kingemtenganisha kutoka katika ufalme wake.

Maneno hayo yakamfanya Iyanya kumpenda zaidi Theo, alijiona kuwa na thamani kubwa, mzuri hata zaidi ya Violeth ambaye muda huo alikuwa hospitalini akimuuguza mtoto wake.

Wakati wakijiandaa kulala ndipo simu ya Theo ikaanza kuita, akaangalia jina, alikuwa meneja wake. Hakutaka kuipokea lakini akaona siyo tatizo, alitakiwa kumdanganya kwamba alikuwa na mkewe hivyo ili hata kama alihitaji kumwambia amfuate, asitoke.
 
yaani inabidi mjieleze vzr mueleweke,
Wanaume mnajua kutuumiza pasina sababu,
Sie hungonja mkianza bc sie tunamaliza (kwa wenye ujasiri wa visasi ) hapo ni 80/20
Hapa sasa unataka league " na sio vinginevyo ... wanaume wengi huwa tunapatwa na misuko suko toka kwa wanawake .
Lakini kwakuwa ki-nature yetu huwa hatupendi kuielezea jamii kuhusu matatizo ambayo tunakutana nayo katika mahusiano ambayo huwa yana sababishwa na wanawake .
.. basi dunia inakuta inafahamu machache kuhusu sisi " na kuona kwamba hatuumizwi kivyovyote " kwa sababu jamii inakuwa ina uhaba wa taarifa za manyanyaso zinazo tuhusu ...

So tuko 50/50 hahahaahaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mamaae Theo
SEHEMU YA 58

Watanzania wengi waliopenda umbeya muda huo walitaka kukesha kama popo, walikuwa wakilijadili jambo hilo kwa mapana zaidi kwani kwa kile kilichokuwa kimetokea, kiliwaumiza kwa sababu tu huyo Violeth alikuwa mwanamke aliyetulia na kujiheshimu ambaye hakutaka kufuatilia maisha ya mtu yeyote yule.

Muda huohuo Theo alikuwa hotelini akiendelea kula raha na Iyanya, moyo wake ulikuwa na furaha kubwa, kila alipomwangalia msichana huyo, kwa jinsi alivyoumbika na kiwowowo chake cha kizushi kikamchanganya zaidi.
Ilipofika majira ya saa sita usiku, wakamaliza hivyo kukaa kitandani na kuanza kupiga stori.

Mwanaume huyo alimwambia Iyanya ukweli wa moyo wake kwamba alimpenda, hakukuwa na mwanamke zaidi yake, alimpenda zaidi ya mke wake, alimpenda zaidi ya mtu yeyote yule katika dunia hii.

“Why don’t you divorce your wife and marry me?” (kwa nini usimpe talaka mkeo na unioe mimi?) aliuliza Iyanya.
“No! It that won’t happen,” (hapana! Hilo haliwezi kutokea)

“Then you don’t love me,” (basi hunipendi)
“I love you Iyanya! I really love you,” (nakupenda Iyanya! Nakupenda mno)

“Why don’t you want to diveorce your wife for me?” (kwa nini hutaki kumpa talaka mkeo kwa ajili yangu?) aliuliza msichana huyo.

“We are christians! Things don’t work that way.” (sisi ni Wakristo! Mambo hayafanywi hivyo) alisema Theo huku akimwangalia msichana huyo.

Akamsogelea na kumkumbatia. Alimwambia kwamba hata kama hatompa talaka mkewe bado angempenda mpaka kifo chake na kusingekuwa na kitu chochote kile ambacho kingemtenganisha kutoka katika ufalme wake.

Maneno hayo yakamfanya Iyanya kumpenda zaidi Theo, alijiona kuwa na thamani kubwa, mzuri hata zaidi ya Violeth ambaye muda huo alikuwa hospitalini akimuuguza mtoto wake.

Wakati wakijiandaa kulala ndipo simu ya Theo ikaanza kuita, akaangalia jina, alikuwa meneja wake. Hakutaka kuipokea lakini akaona siyo tatizo, alitakiwa kumdanganya kwamba alikuwa na mkewe hivyo ili hata kama alihitaji kumwambia amfuate, asitoke.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
yaani inabidi mjieleze vzr mueleweke,
Wanaume mnajua kutuumiza pasina sababu,
Sie hungonja mkianza bc sie tunamaliza (kwa wenye ujasiri wa visasi ) hapo ni 80/20

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona hata wanawake wanaoumiza bila sababu wapo wengi tu ... " hii mada ukitaka ui-jadili kwa fact unapaswa kuweka mbali mahaba ya kijinsia ya jinsia yako kando kwanza ... kisha uanze kuzitazama hizi changamoto zinazo sababishwa na hizi jinsia zote 2 katika Jamii .. ndio utakubaliana na mimi .. kinyume na hapo ..utaishia kubishana tu mkuu ..without logic consistent ...

Mkuu wanaume huwa tunaumizwa sana " ila huwa tunaficha" kwa sababu hatutaki kuonekana kuwa sisi ni viumbe dhaifu .. na ndio huwa tunakufa mapema pia kwa sababu huwa tuna ubebesha moyo mambo mengi ambayo mwisho wa siku huwa yanalipuka na kuzalisha maradhi na kuathiri mfumo mzima wa uzalishaji kinga za mwili .(hili haswaa huwa linachangiwa na uwepo wa stress za muda mrefu baada ya kufanyiwa ndivyo sivyo " na nyinyi "

Narudi kwenye msimamo wangu "

Men lier " Woman lier hakuna mwenye nafuu mkuu "

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom