Mndengereko,
Naomba nijibu baadhi ya hoja/lawama ambazo umemtupia David Moyes
Hii issue ya usajili wengi wanamlaumu Moyes but sidhani kama anastahili kulaumiwa,Moyes alivyopewa timu aligundua tatizo kubwa la kiungo la muda mrefu ambalo SAF alishindwa kulifanyia kazi.Wachezaji ambao Moyes alikuwa anawataka (Thiago,Fabregas,Herrera na Mondric) Ukiangalia utagundua hao ndio aina ya wachezaji ambao Man United inapaswa kuwa nao.Kumbuka ukiacha SAF pia David Gill nae aliondoka, baada ya Abromovic kumchukua Peter Kenyon(Mtaalamu wa fitina za usajili) Gill ndio alimrithi nae taratibu akawa mtaalamu kwenye usajili.Mrithi wa Gill
Ed Woodward ni mtu ambae hana kabisa uzoefu na masuala ya usajili huyu ndio mtu wa kulaumiwa kwenye issue ya usajili
Moja ya sababu kubwa ya Man United kufanya vibaya msimu huu ni wachezaji wengi kucheza chini ya kiwango na Kagawa ni mmojawapo.Moyes amewapa nafasi wachezaji karibia wote,mechi ambayo Kagawa alicheza vizuri na Leverkusen the rest mechi kiwango chake still ni average.Msimu huu Kagawa hajafunga goli na hana assist hata moja ingawa unasema game alizocheza UCL timu imeshinda(Rooney ndio ameibeba timu).Ligi ya England inahitaji kasi na nguvu sana kuliko Champions League ndio maana Kagawa anaonekana anacheza vizuri kwenye UEFA kuliko kwenye ligi
Moyes alivyokuja alijaribu kutumia viungo (Cleverley,Kagawa,Giggs,Felaini,) lakini viungo wamechemka ndio maana akarudi kutumia mawinga ambao at least walianza kuonyesha matumaini (Nani,Januzaj,Valencia,Young) at least wamefunga/kutengeneza magoli kuliko viungo ambao wamekuwa butu kufunga/kutengeneza magoli
Nakubalina na wewe kwamba Smalling ni weak link kwenye defence kinachomsaidia ni uwezo wa kucheza zaidi ya nafasi moja but I doubt kama unafahamu kiwango cha Fabio,Fabio alitegemewa sana kuwa msaidizi na baadae mrithi wa Evra lakini kiwango chake kinazidi kuwa kibovu siku zinavyozidi kwenda.Nafikiri umemuona juzi alivyoingia,mwenzake Rafael hana mpinzani beki wa kulia kama akiwa fit
David Moyes kweli anaweza akawa kocha mbovu, moja ya weakness zake ni kufanya sub mbovu, lakini ni mapema sana kumpa mzigo wa lawama zote Man United inavyofanya vibaya.Timu nzima inahitaji reshufle kuanzia defence,midfield na foward nafikiri hii kazi ilipaswa kufanywa na SAF, wachezaji kama Anderson,Giggs,Buttner,Nani,Rio,Cleverley,Smalling,Fletcher,Fabio hawastahili kabisa kuchezea Man United kwa sasa while wachezaji kama Evra,Carick,Rooney,Vidic wanastahili kupatiwa wasaidizi,Kagawa,Felaini,Valencia nao wanapaswa kuimprove viwango vyao