Sawa mkuu. Hata mie earphone huwa hazipo mbali. Sipendi kabisa hata kwangu sina hata cd 1.
:-D:-D:-D
Unaangalia bongo movie kwani wewe ni house girl?
...kuna moja niliikuta sehemu, mtu kaonyeshwa bastola naye katoa ya kwake.ndo umemaliza au bado unaandika tusubiri?manake nahisi kama sijaelewa vile
Hivi watanzania nani kawaroga mpaka vya kwenu hata kama si vizuri mpaka mnavikataa? Hivi ni kweli kwamba hata vichwa vyenu tayari navyo vimebinafisishwa? Acheni ushamba wa kudharau kwenu na kutamani vya nje. Cha ajabu huko Ulaya au America hawashobokei za kwenu kama mnavyofanya nyinyi/ninyi. Mjilaumu wenyewe na mje na suluhu nini kifanyike kuboresha movie za ndani
...kuna moja niliikuta sehemu, mtu kaonyeshwa bastola naye katoa ya kwake.
...jambazi anavua viatu mlangoni.
Mkuu taratibu, umewahi kuangalia filamu za vicent kigosi? Mbona utapata maumivu ya kichwa!
Naweza kusema haupo sahihi hata kidogo,
tamthilia za Itv ambazo zipo mpaka leo zina ubora kuliko hizo bongomovies,
JE Tamthilia hizi hazifanyiki hapa Tanzania?
Kuangalia BONGO MOVIE ni bora uangalia TOM N JERRY mara 100000000000000.......!!!!! Sory kwa wadau
Tukubali tukatae utandawazi pia unachangia sana tuone vyetu havifai. Na hii inatokana na ukweli kwamba tunajifananisha na wenzetu walio tutangulia hatua 1000 mbele yetu. Ulinganishaji huu haupo fair hata kidogo. Nakumbuka Enzi hizo kuna Maigizo ya mambo hayo jahazi ya kaole ya kina bishanga waridi sekioni kusema ukweli ilikuwa inavutia wengi sana kutokana na ukweli kwamba ni wachache sana miongoni mwa wana jamii walikiwa na Access ya kuangalia movie za nje. If am wrong katikati ya miaka ya 2000 hadi 2005 movie za ki Nigeria tulikuwa tuna zi appreciate sana kina Ramsey Noah Geneviev ila ni Wangapi leo wanazikubali hizi movie? Hata za kina bishanga leo hazina mvuto wakati enzi hizo zilikuwa ndo zenyewe. Nilikuwa nawaona wasanii hawafanyi vizuri lakini kusema ukweli tunapojilinganisha na wa nje ni sawa sawa na Timu ya taifa stars Vs Germany au Diamond Vs jay z huu ni uonevu wa hali ya juu. Imagine bongo movie 10 years ago ilikuwaje na imagine itakuwa vipi miaka 10 kutoka sasa.
Nimekusoma mkuu, lakini nini kifanyike ili kuziba ombwe hili la kuiga kila kitu kutoka nje au hata kufanya movie zinazojikita katika masuala mtambuka(cross-cut issues) na si mapenzi tu kana kwamba jamii haina kitu.kingine cha kuifikishia ujumbe?
...na mhusika mkuu lazima awe anamiliki kampuni !Ivi ni lazma kwa movie za kibongo mlinzi awe ka chizi ivi?!
Bongo muvi ni hovyo kabisa tangu afe The Great Kanumba.
Unakuta muvi ina part 1 na 2 ila sasa angalia hyo part tu mbna utakoma na roho yako mfano ni hii muvi inaitwa Bado nipo hai ilioneshwa EATV siku ya jumamosi aisee mule ndani ni hovyo hawajui hata jinsi ya kumaliza muvi. Waigizaji hawajielewi full makelele tu kamera inatikisika hovyohovyo mara sauti ipande na kushuka yaani halafu wanasema wanaibiwa kazi zao mi kwa kazi ipi hadi niibe ujinga huo.
Bora kanumba angekuwa hai ningekuwa naangalia filamu zake maana alikuwa anajua nn anafanya.
:-D:-D:-D
Unaangalia bongo movie kwani wewe ni house girl?
Kwa hiyo na zile unazozipenda...muvi zao ZOOOTEEE ni nzuri..?Ni kulialia, kufokeana, kuonyesha magari, tena kama wapo njiani utasubiri mpaka wafike.
Na kama ni mgonjwa wataonyesha mpk anavyotapika.
... siziwezi aisee !
Nikipata safari ya mbali inayoanzia masaa 6 au zaidi lazima nahakikisha nimechaji betri za simu kama 2 au 3 kwa ajili ya kula muziki laini kwa earphone wakati huohuo nikitembelea mitandao mbalimbali kama jf.
Ivi ni lazma kwa movie za kibongo mlinzi awe ka chizi ivi?!