Movie za Bongo Siziwezi

Sawa mkuu. Hata mie earphone huwa hazipo mbali. Sipendi kabisa hata kwangu sina hata cd 1.

Nikipata safari ya mbali inayoanzia masaa 6 au zaidi lazima nahakikisha nimechaji betri za simu kama 2 au 3 kwa ajili ya kula muziki laini kwa earphone wakati huohuo nikitembelea mitandao mbalimbali kama jf.
 
:-D:-D:-D
Unaangalia bongo movie kwani wewe ni house girl?

Hivi watanzania nani kawaroga mpaka vya kwenu hata kama si vizuri mpaka mnavikataa? Hivi ni kweli kwamba hata vichwa vyenu tayari navyo vimebinafisishwa? Acheni ushamba wa kudharau kwenu na kutamani vya nje. Cha ajabu huko Ulaya au America hawashobokei za kwenu kama mnavyofanya nyinyi/ninyi. Mjilaumu wenyewe na mje na suluhu nini kifanyike kuboresha movie za ndani
 

Mkuu taratibu, umewahi kuangalia filamu za vicent kigosi? Mbona utapata maumivu ya kichwa!
 
Mkuu taratibu, umewahi kuangalia filamu za vicent kigosi? Mbona utapata maumivu ya kichwa!

Nimekusoma mkuu, lakini nini kifanyike ili kuziba ombwe hili la kuiga kila kitu kutoka nje au hata kufanya movie zinazojikita katika masuala mtambuka(cross-cut issues) na si mapenzi tu kana kwamba jamii haina kitu.kingine cha kuifikishia ujumbe?
 
Kuangalia BONGO MOVIE ni bora uangalia TOM N JERRY mara 100000000000000.......!!!!! Sory kwa wadau
 
Bongo muvi ni hovyo kabisa tangu afe The Great Kanumba.
Unakuta muvi ina part 1 na 2 ila sasa angalia hyo part tu mbna utakoma na roho yako mfano ni hii muvi inaitwa Bado nipo hai ilioneshwa EATV siku ya jumamosi aisee mule ndani ni hovyo hawajui hata jinsi ya kumaliza muvi. Waigizaji hawajielewi full makelele tu kamera inatikisika hovyohovyo mara sauti ipande na kushuka yaani halafu wanasema wanaibiwa kazi zao mi kwa kazi ipi hadi niibe ujinga huo.
Bora kanumba angekuwa hai ningekuwa naangalia filamu zake maana alikuwa anajua nn anafanya.
 
Naweza kusema haupo sahihi hata kidogo,
tamthilia za Itv ambazo zipo mpaka leo zina ubora kuliko hizo bongomovies,
JE Tamthilia hizi hazifanyiki hapa Tanzania?

hazikosi part one na part two hata kama ni fupi kiasi gani
 
Kuangalia BONGO MOVIE ni bora uangalia TOM N JERRY mara 100000000000000.......!!!!! Sory kwa wadau

umeongea vizuri saaaana ila hapo mwisho umeharibu,sorry ya nini wakati ni ukweli mtupu jamani?
 
Ivi ni lazma kwa movie za kibongo mlinzi awe ka chizi ivi?!
 

Umeangalia movi za miaka ya 40s za wenzetu km vile Taxi Driver.
Au hata Godfather ya 1972 ?

...sio kweli kuwa tumechelewa, suala ni kuwa hatuko serious in issues
 
Nimekusoma mkuu, lakini nini kifanyike ili kuziba ombwe hili la kuiga kila kitu kutoka nje au hata kufanya movie zinazojikita katika masuala mtambuka(cross-cut issues) na si mapenzi tu kana kwamba jamii haina kitu.kingine cha kuifikishia ujumbe?

Waibuke kina Jengua, Nyama yao, muhogo mchungu, mzee small, king majuto na wengineo wapya tuendeleze tasnia ya maigizo ktk scenario za Kitanzania. Kwa sasa kinachoharibu ni haohao kina kigosi na uwoya kujifanya kuiga mambo ya ulaya halafu wanashindwa kuvaa uhalisia. Mimi kwa sasa natamani mizengwe ya max na zembwela ya kipindi hicho marehem max akiwa hai.
 

hizo ndio naangaliaga. Rip kanumba
 
Ni kulialia, kufokeana, kuonyesha magari, tena kama wapo njiani utasubiri mpaka wafike.
Na kama ni mgonjwa wataonyesha mpk anavyotapika.
... siziwezi aisee !
Kwa hiyo na zile unazozipenda...muvi zao ZOOOTEEE ni nzuri..?
 
Nikipata safari ya mbali inayoanzia masaa 6 au zaidi lazima nahakikisha nimechaji betri za simu kama 2 au 3 kwa ajili ya kula muziki laini kwa earphone wakati huohuo nikitembelea mitandao mbalimbali kama jf.

kuna power bank siku hizi mkuu.huna haja ya kutembea na batri na mbili/tatu.ukiwa safarini unakuwa hewani mda wote.
 
movie ya kibongo zipo nzuri tujifunze kuheshimu vya kwetu.
mfano movie ya KIGODORO.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…