Ustaadh
JF-Expert Member
- Oct 25, 2009
- 413
- 19
MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, amemjia juu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, akimtuhumu kwa kuendeleza mgawanyiko ndani ya chama na sasa anamtaka afute kauli yake kuwa aliondolewa uspika kwa mizengwe na Kamati Kuu ya chama hicho tawala.
Kutokana na hatua hiyo, ameeleza nia ya kuwasilisha hoja binafsi kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, ili Sitta athibitishe madai yake.
Mgeja aliyasema hayo jana Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu kauli ya Sitta kuwa aliondolewa uspika kwa hila.
"Sitta anapaswa kufuta kauli yake kuwa aliondolewa kwa hila…kikao kilichofanya maamuzi kuhusu nafasi ya uspika ni Kamati Kuu ya CCM, kwa hiyo anamaanisha wajumbe wa kikao hicho wana hila naye.
Kusema hivyo kutasababisha baadhi ya wanachama kukosa imani na kikao hicho," alisema Mgeja.
Mgeja ambaye kwa wadhifa wake ni Mjumbe wa NEC Taifa, alisema CCM hakuna mwanachama aliye juu ya chama na kuwa maamuzi yanayotolewa na vikao halali vya chama yanapaswa kuheshimiwa.
"Nitawasilisha hoja binafsi kwenye NEC ili kumtaka Sitta athibitishe kuwa amefanyiwa hila kwa kuwa kama hakuridhika na uamuzi, alipaswa kukata rufani kwenye vikao husika," alisisitiza Mgeja.
Alimlaumu spika huyo wa zamani kwa kuwa na kauli anayodai zinasababisha mgawanyiko na kuendeleza makundi kwenye chama.
Akizidi kumkosoa, Mgeja alisema hata kauli aliyoitoa Sitta juu ya sakata la Kampuni ya kufua umeme ya Dowans lilikuwa na lengo la kuibua chuki miongoni mwa wananchi, jambo ambalo halikupaswa kufanywa na kiongozi kama huyo mwenye fursa ya kumshauri Rais kutokana na kuwa waziri.
"Uamuzi uliotolewa wa kuilipa Dowans fedha zote hizo kila Mtanzania unamuuma, lakini kauli za kukataa au kupinga huku ikijulikana suala hilo ni la kisheria, ni kutaka kuwapotosha wananchi kuhusu ukweli halisi," alisema Mwenyekiti huyo wa CCM Shinyanga.
Alimpongeza Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa alivyolifafanua suala hilo mbele ya wahariri,
akieleza taratibu na sheria zinapaswa kufuatwa katika masuala yanayohusu sheria, kwani serikali inajali utawala bora.
......................................................
Huyu ni mmojawapo wa 'viongozi' waliokunywa maji ya bendera ya kijani!
Kutokana na hatua hiyo, ameeleza nia ya kuwasilisha hoja binafsi kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, ili Sitta athibitishe madai yake.
Mgeja aliyasema hayo jana Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu kauli ya Sitta kuwa aliondolewa uspika kwa hila.
"Sitta anapaswa kufuta kauli yake kuwa aliondolewa kwa hila…kikao kilichofanya maamuzi kuhusu nafasi ya uspika ni Kamati Kuu ya CCM, kwa hiyo anamaanisha wajumbe wa kikao hicho wana hila naye.
Kusema hivyo kutasababisha baadhi ya wanachama kukosa imani na kikao hicho," alisema Mgeja.
Mgeja ambaye kwa wadhifa wake ni Mjumbe wa NEC Taifa, alisema CCM hakuna mwanachama aliye juu ya chama na kuwa maamuzi yanayotolewa na vikao halali vya chama yanapaswa kuheshimiwa.
"Nitawasilisha hoja binafsi kwenye NEC ili kumtaka Sitta athibitishe kuwa amefanyiwa hila kwa kuwa kama hakuridhika na uamuzi, alipaswa kukata rufani kwenye vikao husika," alisisitiza Mgeja.
Alimlaumu spika huyo wa zamani kwa kuwa na kauli anayodai zinasababisha mgawanyiko na kuendeleza makundi kwenye chama.
Akizidi kumkosoa, Mgeja alisema hata kauli aliyoitoa Sitta juu ya sakata la Kampuni ya kufua umeme ya Dowans lilikuwa na lengo la kuibua chuki miongoni mwa wananchi, jambo ambalo halikupaswa kufanywa na kiongozi kama huyo mwenye fursa ya kumshauri Rais kutokana na kuwa waziri.
"Uamuzi uliotolewa wa kuilipa Dowans fedha zote hizo kila Mtanzania unamuuma, lakini kauli za kukataa au kupinga huku ikijulikana suala hilo ni la kisheria, ni kutaka kuwapotosha wananchi kuhusu ukweli halisi," alisema Mwenyekiti huyo wa CCM Shinyanga.
Alimpongeza Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa alivyolifafanua suala hilo mbele ya wahariri,
akieleza taratibu na sheria zinapaswa kufuatwa katika masuala yanayohusu sheria, kwani serikali inajali utawala bora.
......................................................
Huyu ni mmojawapo wa 'viongozi' waliokunywa maji ya bendera ya kijani!