Alvin A.
JF-Expert Member
- Oct 14, 2016
- 2,868
- 3,624
- Thread starter
- #81
Sikia wewe mtu, wana waisrael walipopewa nchi ya kaanani hata kama ilikaliwa wao walipewa na wakaichukua rejea bibliaapewe na nani na alikuta watu wakiishi hapo
Waisraeli waitwaa nchi ya Kanaani wakiongozwa na Yoshua. Yehova atumia waamuzi kuwakomboa watu wake kutoka mikononi mwa adui zao
KARNE nyingi kabla ya Waisraeli kuingia Kanaani, Yehova alikuwa ameahidi kwamba wazao wa Abrahamu wangeimiliki nchi hiyo. Wakiongozwa na Yoshua, sasa Waisraeli wako tayari kuimiliki Nchi ya Ahadi.
Mungu aliamua Wakanaani wanastahili kuangamizwa. Walikuwa wameijaza nchi mazoea machafu ya ngono na umwagaji wa damu kimakusudi. Hivyo, majiji ya Kanaani yaliyokuwa yametwaliwa na Waisraeli yalipaswa kuharibiwa kabisa.
KUTOKA 3:6-10
6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu.
7 BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;
8 nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.
9 Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
10 Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri.