Moshi Nimewakubali!! David Mosha shtuka!.

Moshi Nimewakubali!! David Mosha shtuka!.

Huyu bwana juzi kazomewa mpaka na watoto wadogo.....
 
Iyo ya yahaya unaishi wapi nimeipenda
 
mi namshangaa sana mosha ni mkazi wa dar lakini anataka ubunge moshi angegombea kinondoni anakokaa kuliko kupambana na jafary kijana mzawa na mkazi

Ni kama Jumanne kishimba! Yeye ni mkazi wa zimbabwe lakini anataka ubunge kahama halafu likizo yake ni anaenda Mwanza
 
Kampeni zinazopigwa hapa spesheli na za aina yake.
Kwanza mabango ya Chadema (UKAWA) yakiwekwa yanaondolewa ndani ya dakika chache...
Sababu ni nzuri kabisa.

David Mosha anatumia nguvu na pesa ambazo kwa kweli zimepata watumiaji...
Hapa Moshi bwana Mosha kaurejesha wimbo wa Yahaya ulioimbwa na Lady Jaydee kwenye chat, ndiyo wimbo hapa...

Ni ngumu sana CCM kushinda ubunge Moshi mjini.
Hawa vijana wanaotoa bango ya Chadema ni wanazi wa chadema completely...wanafanya hivi kupiga hela zaidi za CCM!!
Mchana wako CCM kupiga hela ikifika jioni ni kampeni kali kwa upande wachadema, so ni kama deal flani hivi yakipekee...
Vijana wanaendesha kampeni za Ukawa kwa pesa ya CCM.
Wenyewe hawashtuki.

Mnashinda mitandaoni kusema uongo wenzenu wanashinda kuomba Kura pole sana Sisi tuna chagua Mosha Hapa Moshi tumechoka ubabaishaji
 
Umesema ukweli mtupu.
Ile kauli ya KULA CCM KULALA CHADEMA inatekelezwa kwa vitendo.
Mbunge mtarajiwa,Jaffari Michael anasema vijana wasitoe mabango ya Mosha ili achangie mapato ya manispaa.

Ile ya kutick inaitwa KURA sio KULAA
 
..mbaya sana; unaenda kwa watoto wa mjini huku unajisifu una pesa..! lazime wakuumize, yule anaeonekana mwenzao ndio atakaeshinda, we uliekuja na mapesa yako jiangalie sn..
 
Kwa kweli Yahaya ana kazi.Imebidi anunue nyumba fasta baada ya kuulizwa anaishi wapi! Hata hivyo haikumsaidia sana kwani aliulizwa tena umejiandikisha wapi kupiga kura! Davis Mosha aka Yahaya amejiandikisha Dar na sasa anahaha kuhamisha taarifa zake

Mi mwenyewe nilifikiri kwamba mtu tajiri atashindwaje kuwa na nyumba sehemu anayotaka kuitawala si anunue!
 
Me mutuz hajatia timu huko kumsaidia mfadhili wake anayemuweka mjini?
 
Hiyo ilikuwa ni baada ya kuchakachua sana...

Msijidanganye wanamoshi uchaguzi mkuu msiudharau. Mwaka 2005 ilikuwa almanusra Dr Slaa apigwe chini na Tsere wa CCM huko Karatu. Chukueni tahadhari.
 
Back
Top Bottom