Morogoro ni kama imerogwa

Ila Moro napakubali sana. Sio mikoa yote lazima iwe na vurugu kama Dar sijui Katoro. Mikoa mingine inapaswa iwe tulivu kama Moro.
umenena sana,, Katoro Geita pua nyembamba zimejaa kama uko Rusumo πŸ˜†
 
Okay kwahiyo wanaoga Mara chache Sana kwa siku?..
 
Ahmadia, Masika, soko la Kingalu huko kote nakujua hakuna mabadiliko
Kwa hiyo hujaona mabadiliko ya soko la kingalu? Lilikuwa hivyo miaka 15 iliyopita?
Wala hujaona jengo lolote jipya pale mtaa wa Ngoto na mtaa wa Kingo?

Na mtaa wa uhuru je?

Vipi pale pembeni ya Tanganyika Library?

Na maeneo ya stendi ya zamani? Hakuna mabadiliko kwa miaka 15?
 
Uzuri tuna Kahumba na tunatamba nayo, zaidi ya SUA, MZUMBE NA MUM...πŸ™ƒπŸ™ƒπŸ™ƒ
 
Umenikumbusha tulienda msibani Machame,unapita pale kwa Mbowe, mbele kama km 7 hivi,kuna tajiri mmoja amejenga nyumba ya ghorofa 10 na huko ndani ndiyo tulifikia,wanafuga mbuzi tu humo na shamba boy wanaishi humo,na ile nyumba angeijenga sehemu yenye kimji kidogo ingewezekana kufa ofisi za makampuni, mpaka leo huwa sielewi why alijenga kijijini hata kama ni sifa angejenga nyumba ya kawaida tu
 
Mapungufu haya sio ya watu wa Morogoro bali ni ya serikali kukosa kuwa na sera nzuri za kuendeleza miji.
 
Dar es salaam yenyewe ni kijiji kikubwa sembuse hiyo kasoro bahari,ukitaka uijuwe moro we piga misele alafu tia kidole na kitambaa cheupe ndani ya pua zako ndiyo utajuwa hiyo exhaust pipe au tundu za pua.Sema ndiyo hivyo home sweet home.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…