Lupamba's grandson
JF-Expert Member
- Jan 9, 2015
- 1,232
- 1,192
Ajali ya magari iliyotokea asubuhi ya leo sa 06:46 asubuhi hii maeneo ya Maseyi Morogoro iliyosababisha mabasi mawili na lori la mafuta, Mabasi yote yakielekea upande wa mashariki kama sitakosea Dar es salam. Na lory likiwa linaelekea upande wa Morogoro.
MABASI yaliyopata ajali hiyo ni basi la kampuni ya ABOOD na basi la kampuni ya BM COACH na lori ambapo mabasi haya yalitupita sisi tukiwa kwenye basi la SARATOGA tukitoka Kigoma kwa speed sana yakifukuzana ambapo basi la ABOOD likiwa mbele na basi la kampuni ya BM likifuata hapo nyuma .
Tulipofika mbele tulikuta basi la BM likiwa limepinduka, ambapo watu wote wamenusurika japo kuna majeruhi na kondakta kalaliwa na basi miguu na basi la Abood likiwa limeisha na kuharibika vibaya upande wa nyuma na mbele kwa dereva na baadhi ya majeruhi ,pamoja na lori kuvunjika kiasi kioo cha mbele.
MASHUHUDA: Basi la Abood ndo lililoanza kugongana na lori wakati aki overtake basi la BM ambapo basi lilimshinda nakuingia Ngorongoni dereva wa BM nakupinduka, nikiwa mmoja wawaokoaji sikuweza kupiga picha ila zitakuja maana huwa sina tabia ya kupiga picha ajali kabla ya kuokoa watu kwanza mpka naondoka eneo la tukio kuendelea na safari yangu tumeacha kondakta wa BM bado amebanwa chini ya basi upande wakushoto wa dereva.
Jambo la kumshukuru Mungu lori lile halikuweza kupasuka tank sababu kama lingepasuka tungekuwa tunaongea mengine kwasababu lilikuwa na mzigo wa mafuta kusafirishwa kuwelekea nchi za jirani.