Aisee Mkuu bonge la IDEA kaka.
Mungu akubariki kwenye Biashara yako,usisahau kuweka maombi on daily basis ili mungu akuvushe mbali zaidi na akupe uvumilivu wa changamoto ili usimame Imara.
Unajua watu sio tusubirie mpaka wazungu waje waanzishe wakati sie wenyewe vitu vingi vimo ndani ya Uwezo.
Bei zako za vyakula ni rahisi mno.Sie tuliopo Miji ya Biashara tunajua bei za vyakula hasa vyenye ubora wa namna hiyo,na delivery fee yenu ni very cheap.
Wapo watu watawabeza sana kwenye Bei na biashara yenu,ila siku zote kwenye maisha heshim ndoto yako na usikubali kuyumbishwa.Watanzania wengi vijana tuna maisha ya kukariri kwamba akiwa mzungu anauza chakula elf 40 basi ni bora zaidi kuliko mswahili akiuza chakula kile kile elf 10.
Mwambie alietengeneza Logo yenu hongera sana,nimeipenda sana na ujumbe wake unaeleweka
Najua mmejipanga vizuri,ila ningeshauri yafuatayo.
a)Website
Tengenezeni Website,ambayo itakuwa na aina zoote za vyakula mnavyotengeneza.
Na pia iwe na ratiba maalum ya chakula kwa juma katika kila siku,ili mtu ajue siku fulani kuna chakula gani na siku fulani kuna chakula gani,hii itasaidia kuwa na wateja wenye uhakika zaidi,mnaweza kupika hata aina mbili kwa siku,unajua hii inasaidia kwamba ni rahisi wateja kupashana habari kwamba siku fulani kuna kitu fulani,ili hata kama mtu akitoka kwake anajua leo mchana my favorite food ipo.Na wengine huweza hata kupangua ratiba ya chakula cha nyumba ili a meet hiyo flavour.
Lakini ukipika bila mpangilio ilimradi tu upate wateja,utakuwa kama mamalishe wa uswahili tu,We chukua mfano Migahawa ya Wageni hapo Dar,kuna siku ni nyama choma tupuuu,na ukienda watu kibaoooo,na kuna siku swahili flavour yaani nyomi balaa.Utajiuliza kwanini hawapiki vyote siku moja.Jibu ni Creativity
b)Vipeperushi na Mbinu za Ziada za Masoko kwa mazingira yetu
Tengenezeni vipeperushi,hata kama baadhi ya watu wanavichana,ila kwenye 10,basi sita watashika.Na hao ni muhim saana kwako.
-Tembeleeni maofisini,ili mnadi biashara yenu
Hili ni muhim sana ila inabidi kujipanga:-
Tengenezeni siku maalum,ya kutoa offer ya chakula bure,hata kama potion kidogo kwenye yale maofisi makubwa,na hata madogo,kwa wale ambao hawajaijua biashara yenu,ili kuwapa taste.Hii ni mara moja tu,then mnaenda sehem nyingine.
Hii unaweza kuona ni kutupa hela ila hii kwa Migawaha mikubwa duniani ndio wanaifanya na inawainua ile mbaya.
Kujipanga:-
Mnaweza kuwa mmekuja kivingine,na ninajua wapo wenzenu wanafanya kama nyie ila kizamani zaidi.
Sasa Watanzania kama kawaida yetu ya kuiga biashara,wapo watafuata nyayo zenu kama mnavyofanya,na waigaji wengi hawaigi kwa nia njema,Biashara zimejaa fitna saaaana,Sasa jipange na kwa ubora na umakini,na Time management kwenye Orders.Hizo ndio tools zenu kwenye mafanikio.
Biashara hii inachangamoto sana,msikate tamaa,na kuna kipindi ina hasara za ajabu sana,unaweza kupoteza pesa nyingi sana within a single day.
Ziada ya kupunguza Hasara
Ili kukwepa gharama na kukwepa kupoteza wateja hasa kwa chakula ambacho kimebakia.Maana najua chakula kikilala hamuwezi kuwauzi wateja wenu kwa kuwa wengie wanajua.
Sasa kukwepa hasara hiyo,nakushaurini fungueni Mgahawa au vimgahawa uswahili kabisaa,ili chakula kikibakie huko kwenye Mid class,basi mnapeleka siku ya pili kwenye level ya chini ili angalua kurejesha ile gharama ya chakula tu.
Jingine ni Kukopesha chakula:-
Na washauri ingieni kwenye huduma hii ya kukopesha chakula,najua inachangamoto zake,ila ita wa upgrade kwa kiwango kikubwa sana.Hasa makazini ikiwemo maofisini
Unajua watu wengi pesa zao huwa hazipo kwenye mfumo rasmi,unaweza kukuta mtu ameenda kazini na dharura imetokea akaitumia hela,na wakati huo anataka chakula,sasa nawashauri wekeni terms za Wiki,na malipo ya mwezi.
Wapo watu wanapokea Mishahara mikubwa ila unaweza kukuta kwamba kuna duka mtaani anakopa,na ikifika mwezi analipa vizuri tu.Sasa lazima na nyie msome kwa upana biashara yenu.
Sehem isiyo Rasmi sana na ngum kufikirika (Hospitals)
Jaribuni Sana kwenda Mahospitalini,hasa zile Hospitali za Class fulani.
Wapo wagonjwa wenye pesa,na wapo ndugu wa wagonjwa wenye pesa za kuweza kuwahudumia ndugu zao kwa gharama za Chakula.
Unajua Jiji la Dar hakuna kazi ngum sana kama kumuuguza mgonjwa halafu chakula kitoke nyumbani,kila siku watu wanachelewa.Sasa Tambueni kwamba Wagonjwa wote hawana Class inayofanana,wapo Wagonjwa wametoka Level ya Maisha ya Kati.Ushauri wangu juu ya hili ni kwamba,mnafanya survery asubuhi mapema sana,kisha mnajua kwamba wahitaji wenu ni wapi(Hapa kuna changamoto nyingi sana,unaweza kukuta muweka Order ameisha kufa)
Njia ya kufanya juu ya hili la Hopsitali:-Wekeni sahani mbili za chakula cha bure kwa manesi kama wawili hivi.
Hawa ndio watakuwa kama madalali wenu,na niwazuri saaana kwenye ushawishi,we angalia jinsi wanavyotushawishi tukanunue Dawa duka fulani na tunaenda kwa kujua kwamba Dawa za Duka hilo tu ndio zinaponyesha.
Hii njia ya kutafuta soko unaweza kuona imekaa kama ngum au kama haifai,ila mkuu usije kustuka wakati mwenzio kaisha ingia humo,ukabakia kusema ahh nilitaka kufanya na mie kama yule.Ni njia ngum sana,ila kwenye kutafuta hakuna wepesi hata siku moja.
Yangu ni hayo tu mkuu,kwenye mazuri chukua niliokushauri,na kwenye mabaya au upuuzi naomba uniachie na upuuzi wangu kaka.
Mungu akusimamie kwenye Biashara yako na Malengo yako