Mojawapo kati ya picha zako

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,651
Reaction score
860,929


Najua ni wazi hujui ni ipi, na inaweza ikatokea umeipiga tu katika mazingira fulani yasiyo na matayarisho yoyote.

Lakini niamini ni mojawapo kati ya picha zako ndio itakayotumika kuwekwa juu ya jeneza lako ama kama ikitokea unasafirishwa ndio itawekwa pale mbele kwenye coaster ...na unajua kwanini huijui?

Ni kwa vile kwanza atakayeichagua si wewe na kwa vile unaogopa kifo na hujui utakufa lini.

Unapotafuta ajira unatakiwa kuleta passport size zenye kuonekana vema! Yani sura yote mpaka masikio.

Kumbuka ni picha hiyohiyo itakayotumika kuwekwa kwenye vyombo vya habari kwa kichwa cha habari chenye maandishi makubwa ANATAFUTWA siku ukilikoroga.

Huwa nikiwaona watu wanapiga picha nakuwa nawaza mengi sana
 
Muda wa kuishi nimdogo ila wa kufa ni mwingi zaidi! acha tujiselfishe
 
Hello Mkuu Mshana Jr, habari za siku?! Naona mambo yako yameanza tena, ila binafsi siogopi kufa na tayari picha ya kwenye jeneza langu nishaiandaa, nawaambia wanaonihusu wanahisi natania, ila naamini siku nikifariki wataiweka hiyo, labda nifariki nikiwa mzee sana, ila sina hofu ya kifo.

Pole kwa msiba uliokupata. Amina!

Ahsante!
 
Kwasisi maustadhat akuuuuu............ hatuwekewi picha wala negative.....dini hairuhusu
 
Dah mshana bwana kwa kupenda mambo ya kufa kufa.... Halafu basi ataungekua unaposti mchana, unasubiri usiku watu tumelala, tumeshtuka kidogo usingizin tunapita Jf tunakutana na mambo yako ya kufa kufa, mara mida ya wanga
[emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji87] [emoji144] [emoji144] [emoji144] [emoji25] [emoji25] [emoji779] [emoji779] [emoji779]
 
Duu asante sana kaka ila una ujasiri wa ajabu Kama wangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…