Uchaguzi 2020 Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni; Jeshi la Polisi limeanza vizuri, limalize vizuri Kusimamia Kampeni

Mikono yenye Sugu

Senior Member
Jul 1, 2020
133
215
Pamoja na jeshi la polisi kujitwalia taswira mbaya machoni pa wapenda haki kwa kuonesha upendeleo wa wazi nyakati za nyuma, angalau tokea kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuuwa mwaka huu wameonesha kusimamia weledi na kutotumia maguvu yao kukandamiza washindani wa chama tawala.

Ingawa ni wajibu wao kufanya hivyo kwa mujibu washeria, hata hivyo wanastahili pongezi kwani Watanzania wana muda pasipo kushuhudia ustaarabu huo. Hatutegemei kuona ustaarabu huo ukiwa na ukomo.

Wapenda amani wana shauku ya kuona hali hiyo ikiwa endelevu ili kuweka uhalali wa ushindi kwa yeyote atakayeibuka kidedea kwa uchaguzi wa mwaka huu. Tunatamani kuona atakayeshindwa akikosa pa kushika kusingizia kuwa ameporwa kwa nguvu ya vyombo vya dola.

Kamanda Siro endelea kusimamia hilo, historia itakukumbuka kama mtumishi mwaminifu wa umma uliyesimamia vema nafasi yako.

MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Jeshi la polisi huwa halina tatizo Tatizo huwa linaanzia kwa chama fulani cha Siasa kipo pale ufipa kuleta vurugu
 
Ukweli hata mimi naona mabadiliko makubwa katika utendaji wa jeshi la polisi toka wakati wa kurejea kwa Tundu Lissu. Wamejitahidi kutoingilia shughuli za kisiasa kwa kuwatanya wanasiasa na shughuli zao.

Ila kasoro moja bado ipo ya kuwa kamata watu na kuwaweka ndani kwa muda mrefu bila kuwafungulia mashitaka au kuwapa dhamana bado haijaisha. Hili halina tija wala masilahi kwao na taifa. Mfano hivi wale vijana wa CHADEMA bado wanashikiliwa kwasababu gani mpaka sasa kutokana na kile polisi walicho ita kuogezea maneno kwenye wimbo wa taifa kitu ambacho hata vijana wa CCM walifanya lakini hakuna aliye kamatwa. Kwanini bado wanamshikilia aliye changia uzi wa Mange badala ya kumpa dhamana au kumpeleka mahakamani?

Wakati mwingine ni kama jeshi linajua kabisa hakuna mashitaka ila lina amua kutoa adhabu kwa kuwashikilia ambapo hicho ni sawa na kifungo ambacho hakijatolewa na mahakama. Sirro aangalie hili jambo ukweli lina kera. Kumnyima mtu uhuru kwa kisingizio chote chote kile hakukubaliki. Hivi hao vijana wanashikiliwa kwa uchunguzi gani wanaouchunguza. Mbona nyimbo zipo hadharani wana chunguza nini? Common jeshi la polisi change now! However you are currently doing a good job!
 
Nitawapa sehemu ya Imani yangu kwao kwa kiasi tu kwa hatua ya sasa
 
Ni vigumu sana kukiamini Kisu chenye makali pande zote ,ngumu sana aisee.
 
Wale wakora wanatakiwa waozee jela Haiwezekani waidharau Nchi yetu
Ukweli hata mimi naona mabadiliko makubwa katika utendaji wa jeshi la polisi toka wakati wa kurejea kwa Tundu Lissu. Wamejitahidi kutoingilia shughuli za kisiasa kwa kuwatanya wanasiasa na shughuli zao.

Ila kasoro moja bado ipo ya kuwa kamata watu na kuwaweka ndani kwa muda mrefu bila kuwafungulia mashitaka au kuwapa dhamana bado haijaisha. Hili halina tija wala masilahi kwao na taifa. Mfano hivi wale vijana wa CHADEMA bado wanashikiliwa kwasababu gani mpaka sasa kutokana na kile polisi walicho ita kuogezea maneno kwenye wimbo wa taifa kitu ambacho hata vijana wa CCM walifanya lakini hakuna aliye kamatwa. Kwanini bado wanamshikilia aliye changia uzi wa Mange badala ya kumpa dhamana au kumpeleka mahakamani?

Wakati mwingine ni kama jeshi linajua kabisa hakuna mashitaka ila lina amua kutoa adhabu kwa kuwashikilia ambapo hicho ni sawa na kifungo ambacho hakijatolewa na mahakama. Sirro aangalie hili jambo ukweli lina kera. Kumnyima mtu uhuru kwa kisingizio chote chote kile hakukubaliki. Hivi hao vijana wanashikiliwa kwa uchunguzi gani wanaouchunguza. Mbona nyimbo zipo hadharani wana chunguza nini? Common jeshi la polisi change now! However you are currently doing a good job!
 
Back
Top Bottom