Nini kifanyike Jeshi la Polisi lianze kutenda haki?

M-mbabe

JF-Expert Member
Oct 29, 2009
13,203
23,020
Siyo rahisi mahali popote duniani kwa mtu awaye yote kuweza kuzuia athari hasi (consequences) za machozi ya watu zaidi ya milioni 50. Never!

Watanzania walilia sana mwaka 2020 kuhusu serekali yetu (hususani rais wa wakati huo Magufuli) kuona kuwa ipo kwenye denial state dhidi ya gonjwa baya la korona (COVID-19).

Hata wataalamu wa afya nguli kabisa nchini tunaowajua (sitaji majina - ni wengi) nao hawa walikuwa wameingia kati kulicheza hili sebene la wanasiasa (aka Magufuli).

Watanzania walikuwa wakilia kwa uchungu mkubwa "Hivi afe nani hapa nchini ndipo serekali yetu ianze kuchukua hatua madhubuti dhidi ya korona?".

Kilio cha uchungu wa Watanzania kikafika kunakohusika, likatokea la kutokea, na sasa hadi chanjo tumekubali kuchanjwa!

Machozi ya Watanzania bado yanatiririka dhidi ya madhira mengine mengi yanayohusiana na serekali yetu kwa sasa kuendeshwa kijeshi. Police State.

Raia wema wanapotoa hisia juu ya maisha yao yanayowazunguka na ambayo ni serekali pekee ndiyo yenye wajibu wa kuyapatia ufumbuzi au kuyasemea - kinachotokea ni majeshi yenye silaha kali dhidi ya raia wasio na hatia. Hoja za kisiasa zinajibiwa kwa mtutu na mabomu. Hoja za kijamii majibu yake ni kubambikiwa kesi za madawa ya kulevya, ugaidi, nk.

Chama tawala kiko likizo - jeshi la polisi ndilo lililoshika hatamu na kufanya siasa kwa niaba ya chama tawala (kumbuka yule askari polisi aliyemwambia Mbowe kule jimboni Hai wakati wa uchanguzi wa 2020 kuwa hata afanye nini hawezi kushinda ubunge, na hapa juzi kati amenukuliwa tena akisema Mbowe kwenye kesi ya ugaidi hachomoki).

Udongo wa ardhi ya mama Tanzania umekuwa "tear-logged" (water-logged) kwa mafuriko ya machozi ya Watanzania zaidi ya milioni 50 wanaolilia haki na uhuru wao.

Ni machozi haya haya ndiyo yaliyolowanisha ardhi ya mama Tanzania mwaka 2020 dhidi ya serekali kutochukua hatua stahiki dhidi ya korona, machozi yaliyopelekea yatokee yaliyotokea na hatimaye sasa hata chanjo ya korona tumeikubali.

Machozi ya Watanzania ya sasa mwaka huu wa 2021 dhidi ya serekali ni "Je, katika huu mvutano uliopo kati ya raia na jeshi la polisi kuhusu masuala ya haki na uhuru - serekali inataka kuona nani wanakufa ndipo ichukue hatua za kuhakikisha jeshi hili linatenda haki kwa Watanzania?". Machozi yatapelekea litokee la kutokea. Litatokea.

Mimi ni mtu niliaye kutoka nyikani.
 
Hilo sio jeshi nimajambazi tuu walio jificha kwajina la police.

Chakufanya ni sisi RAIA kutowaogopa tuu ndio dawa yao tofauti na hapo wataendelea hivi hivi mpaka Yesu aje
 
Mleta mada pole kwa kujifanya unauchungu zaidi na Mbowe kuliko viongozi wa chadema, akiwemo Lisu, Mnyika, Sugu, Msigwa na familia yake kwa ujumla. Hivi unafikiri hao kukaa kwao kimya ni kwa bure?

Ukweli ni kwamba viongozi karibu wote wameshamchoka Mbowe ndan ya chama, na ni hao hao walioenda kupeleka taarifa kwa vyombo vya usalama, navyo bila kusita wakachukua hatua.

Mbowe angekuwa na maono baada ya kucheza boko ya kumleta Lowasa ndan ya chama mwaka 2015 angejiuzuru kulinda heshima yake, au angeachana na tamaa yake ya kuendelea kukalia kiti cha uenyekiti wa chadema ambao unamruhusu yeye kukalia kiti hicho kwa muda usiojulikana.

Na uamuzi wake huo ndio una mcost leo. Acha kusingizia polisi wao wanafanya kazi yao kwa mujibu wa sheria.
 
Siyo rahisi mahali popote duniani kwa mtu awaye yote kuweza kuzuia athari hasi (consequences) za machozi ya watu zaidi ya milioni 50. Never!

Watanzania walilia sana mwaka 2020 kuhusu serekali yetu (hususani rais wa wakati huo Magufuli) kuona kuwa ipo kwenye denial state dhidi ya gonjwa baya la korona (COVID-19).

Hata wataalamu wa afya nguli kabisa nchini tunaowajua (sitaji majina - ni wengi) nao hawa walikuwa wameingia kati kulicheza hili sebene la wanasiasa (aka Magufuli).

Watanzania walikuwa wakilia kwa uchungu mkubwa "Hivi afe nani hapa nchini ndipo serekali yetu ianze kuchukua hatua madhubuti dhidi ya korona?".

Kilio cha uchungu wa Watanzania kikafika kunakohusika, likatokea la kutokea, na sasa hadi chanjo tumekubali kuchanjwa!

Machozi ya Watanzania bado yanatiririka dhidi ya madhira mengine mengi yanayohusiana na serekali yetu kwa sasa kuendeshwa kijeshi. Police State.

Raia wema wanapotoa hisia juu ya maisha yao yanayowazunguka na ambayo ni serekali pekee ndiyo yenye wajibu wa kuyapatia ufumbuzi au kuyasemea - kinachotokea ni majeshi yenye silaha kali dhidi ya raia wasio na hatia. Hoja za kisiasa zinajibiwa kwa mtutu na mabomu. Hoja za kijamii majibu yake ni kubambikiwa kesi za madawa ya kulevya, ugaidi, nk.

Chama tawala kiko likizo - jeshi la polisi ndilo lililoshika hatamu na kufanya siasa kwa niaba ya chama tawala (kumbuka yule askari polisi aliyemwambia Mbowe kule jimboni Hai wakati wa uchanguzi wa 2020 kuwa hata afanye nini hawezi kushinda ubunge, na hapa juzi kati amenukuliwa tena akisema Mbowe kwenye kesi ya ugaidi hachomoki).

Udongo wa ardhi ya mama Tanzania umekuwa "tear-logged" (water-logged) kwa mafuriko ya machozi ya Watanzania zaidi ya milioni 50 wanaolilia haki na uhuru wao.

Ni machozi haya haya ndiyo yaliyolowanisha ardhi ya mama Tanzania mwaka 2020 dhidi ya serekali kutochukua hatua stahiki dhidi ya korona, machozi yaliyopelekea yatokee yaliyotokea na hatimaye sasa hata chanjo ya korona tumeikubali.

Machozi ya Watanzania ya sasa mwaka huu wa 2021 dhidi ya serekali ni "Je, katika huu mvutano uliopo kati ya raia na jeshi la polisi kuhusu masuala ya haki na uhuru - serekali inataka kuona nani wanakufa ndipo ichukue hatua za kuhakikisha jeshi hili linatenda haki kwa Watanzania?". Machozi yatapelekea litokee la kutokea. Litatokea.

Mimi ni mtu niliaye kutoka nyikani.
Katiba mpya!
 
Mleta mada pole kwa kujifanya unauchungu zaidi na Mbowe kuliko viongozi wa chadema, akiwemo Lisu, Mnyika, Sugu, Msigwa na familia yake kwa ujumla. Hivi unafikiri hao kukaa kwao kimya ni kwa bure?

Ukweli ni kwamba viongozi karibu wote wameshamchoka Mbowe ndan ya chama, na ni hao hao walioenda kupeleka taarifa kwa vyombo vya usalama, navyo bila kusita wakachukua hatua.

Mbowe angekuwa na maono baada ya kucheza boko ya kumleta Lowasa ndan ya chama mwaka 2015 angejiuzuru kulinda heshima yake, au angeachana na tamaa yake ya kuendelea kukalia kiti cha uenyekiti wa chadema ambao unamruhusu yeye kukalia kiti hicho kwa muda usiojulikana.

Na uamuzi wake huo ndio una mcost leo. Acha kusingizia polisi wao wanafanya kazi yao kwa mujibu wa sheria.
Uharo kama uharo mwingine.
 
Ushauri wangu ni kwamba Jeshi hili la Polisi livunjwe lisukwe jeshi la Polisi jipya liwe na asilimia kubwa ya Wasomi wa Forensics

Tuwe na Polisi walioenda Shule ambao wakiamrishwa kufanya mambo ya ajabu wanahoji amri hizo na wanakaa upande wa Wananchi ambao ndio waajiri wao kwa Kodi zao.
 
Siyo rahisi mahali popote duniani kwa mtu awaye yote kuweza kuzuia athari hasi (consequences) za machozi ya watu zaidi ya milioni 50. Never!

Watanzania walilia sana mwaka 2020 kuhusu serekali yetu (hususani rais wa wakati huo Magufuli) kuona kuwa ipo kwenye denial state dhidi ya gonjwa baya la korona (COVID-19).

Hata wataalamu wa afya nguli kabisa nchini tunaowajua (sitaji majina - ni wengi) nao hawa walikuwa wameingia kati kulicheza hili sebene la wanasiasa (aka Magufuli).

Watanzania walikuwa wakilia kwa uchungu mkubwa "Hivi afe nani hapa nchini ndipo serekali yetu ianze kuchukua hatua madhubuti dhidi ya korona?".

Kilio cha uchungu wa Watanzania kikafika kunakohusika, likatokea la kutokea, na sasa hadi chanjo tumekubali kuchanjwa!

Machozi ya Watanzania bado yanatiririka dhidi ya madhira mengine mengi yanayohusiana na serekali yetu kwa sasa kuendeshwa kijeshi. Police State.

Raia wema wanapotoa hisia juu ya maisha yao yanayowazunguka na ambayo ni serekali pekee ndiyo yenye wajibu wa kuyapatia ufumbuzi au kuyasemea - kinachotokea ni majeshi yenye silaha kali dhidi ya raia wasio na hatia. Hoja za kisiasa zinajibiwa kwa mtutu na mabomu. Hoja za kijamii majibu yake ni kubambikiwa kesi za madawa ya kulevya, ugaidi, nk.

Chama tawala kiko likizo - jeshi la polisi ndilo lililoshika hatamu na kufanya siasa kwa niaba ya chama tawala (kumbuka yule askari polisi aliyemwambia Mbowe kule jimboni Hai wakati wa uchanguzi wa 2020 kuwa hata afanye nini hawezi kushinda ubunge, na hapa juzi kati amenukuliwa tena akisema Mbowe kwenye kesi ya ugaidi hachomoki).

Udongo wa ardhi ya mama Tanzania umekuwa "tear-logged" (water-logged) kwa mafuriko ya machozi ya Watanzania zaidi ya milioni 50 wanaolilia haki na uhuru wao.

Ni machozi haya haya ndiyo yaliyolowanisha ardhi ya mama Tanzania mwaka 2020 dhidi ya serekali kutochukua hatua stahiki dhidi ya korona, machozi yaliyopelekea yatokee yaliyotokea na hatimaye sasa hata chanjo ya korona tumeikubali.

Machozi ya Watanzania ya sasa mwaka huu wa 2021 dhidi ya serekali ni "Je, katika huu mvutano uliopo kati ya raia na jeshi la polisi kuhusu masuala ya haki na uhuru - serekali inataka kuona nani wanakufa ndipo ichukue hatua za kuhakikisha jeshi hili linatenda haki kwa Watanzania?". Machozi yatapelekea litokee la kutokea. Litatokea.

Mimi ni mtu niliaye kutoka nyikani.
Ninaingia hofu kuwa kuna uwezekano mkubwa polisi na familia zao wataanza kukimbia makazi yao maana watu huku mitaani na vijiweni (wengi wao si wanasiasa) wanaongea kwa uchungu mkubwa kuhusu uonevu unaofanywa na polisi nchini.

Mungu apishie mbali kwa kuwapa viongozi wetu hekima ya kuliona hili waweze kuchukua hatua stahiki kwani nchi yetu haipaswi kuingia kwenye civil and political turmoil miaka 60 baada ya uhuru.
 
Pia labda yafanyike mabadiliko ya Muundo wa jeshi na ya kureport Mamlaka za juu.

Nafasi ya IGP itangazwe isiwe kwa hisani ya kuteuliwa.

Kwa muundo wa sasa kuanzia anavyopatikana na kureport kwake mmnh!
 
Wizara ya Mambo ya ndani ndipo lilipo Jeshi la Polisi. Pamekuwa na malalamiko mengi kuhusu Polisi na mengine yakiwekwa wazi pamoja na picha.

Wanachama wa Chadema waliokuwa Rumande Mwanza wameeleza na kutoa hata majina. Heche ametoa kisa cha mtu aitwaye Marijani na wengine.

Pia pamekuwepo na maelezo ya mateso katika vituo kama kupigwa. Jana tumeona kijana aliyevaa fulana ya Katiba mpya akiwekewa kiatu shingoni!

Waziri wa mambo ya ndani yupo kimya mno kukemea au kuonyesha kuwa anaguswa na haya mapungufu. Tukumbuke kuwa Mwenyezi Mungu ndiye mpanga riziki na hakuna aliyejua ya kuwa Mwinyi aliyejiuzulu uwaziri angekuja kuwa Raisi wa nchi.
Simamia haki!
 
Wanayaona Wanayasikia wana agiza
Mahakama KUU Mbeya emwachia MDUDE wa CHADEMA kwa kuwekewa MADAWA ya KULEVYA na POLISI ni DOSARI KUBWA kwa JESHI nilitarajia RPC MBEYA ANGEWAJIBIKA kwa Kulitia Dosari JESHI kuwa Linawafanyia hivyo RAIA lakini Yupo anachapa kazi

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Simbachawene hebu angalia ile picha kijana amekanyagwa shingoni na askari ndani ya gari hapo Kisutu!
 
Back
Top Bottom