Serayamajimbo
Senior Member
- Apr 15, 2009
- 191
- 38
WABUNGE machachari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Zitto Kabwe na John Mnyika, wamesema ni wakati muafaka kwa Watanzania kutafakati namna ya kuipumzisha CCM katika uongozi wa nchi katika uchaguzi ujao kutokana na hali mbaya ya uchumi na ya kimaisha.
Wamesema serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) chini ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete inalizamisha taifa kutokana na hali iliyopo sasa na kusema kuwa endapo haitafanya juhudi za dharura, hali inatakuwa mbaya zaidi.
Akizungumza kwa nyakati tofauti jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mji wa Mombo, mbunge wa Ubungo, John Mnyika, alimtaka Rais Kikwete na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, kutoa kauli ya haraka juu ya mpango wa dharura wa kunusuru uchumi na kutatua tatizo la mfumko wa bei nchini.
Mnyika ambaye pia ni Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, alisema katika miaka zaidi ya sita ya utawala wa Rais Jakaya Kikwete ahadi ya maisha bora kwa kila Mtanzania imekuwa ni ndoto ya kufikirika.
Alisema wananchi walioichagua CCM kwa kurubuniwa na mbinu chafu, kama kuhongwa vyakula, fulana, kofia, sasa wanavuna matunda ya chaguo lao na kuwataka kutumia muda huu kutafakari upya.
"Tumekuja Tanga mwaka huu, ikiwa ni moja ya nafasi ya kutekeleza tamko la Katibu Mkuu, Dk. Slaa, kuwa moja ya kipaumbele chetu mwaka huu ni kunusuru uchumi wa nchi na kukabiliana na gharama za maisha. Tunaitaka serikali kushughulikia vipaumbele ambavyo tumewaonyesha, kuongeza uzalishaji na kutengeneza ajira, ikiwa ni sehemu ya kudhibiti mfumko wa bei," alisema Mnyika.
Aliongeza kuwa kutokana na tamko hilo, wabunge wa CHADEMA kila mmoja kwa nafasi yake, anasimamia hoja hizo za kuongeza uzalishaji na kutengeneza ajira, hali iliyomfanya Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe, kuwasilisha hoja binafsi ya Mkonge, ambayo inalenga kuongeza uzalishaji na kutengeneza ajira katika kilimo.
Alisema licha ya Zitto kuipeleka hoja hiyo kwa maslahi ya wakazi na wakulima wa Tanga, wabunge wa CCM wa mkoa huo waliipinga kwa kile walichoona Watanzania wakiondokana na umaskini nafasi yao ya kuwarubuni itakuwa mashakani.
Akizungumzia viwanda, Mnyika alisema CCM badala ya kufanya ubinafsishaji wamefanya ubinafsi wa viwanda na kutolea mfano Kiwanda cha Tembo Chipboard, ambacho kilikuwa kikipata malighafi kutoka msitu wa Shume, lakini kutokana na sera mbovu na mipango mibovu, uzalishaji umedumaa na kiwanda kimefungwa.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto, alisema kuwa hali ya maisha ni ngumu na inatishia uhai na usalama wa nchi kwa kuwa katika njaa maradhi na umaskini uliokithiri ustaarabu unakosa nafasi.
Aliongeza baada ya Bunge kuikataa hoja binafsi kuhusu zao la mkonge, ni wajibu wa wananchi hao kuwakataa viongozi wasiowatetea kwa vitendo na hata katika masanduku ya kura pindi watakapojitokeza kuomba nafasi za kuwaongoza.
Awali wananchi wa mji wa Mombo walizuia msafara wa Zitto na kuutaka ufike katika mashamba yao wakashuhudie kile ambacho wabunge wa mkoa wa Tanga waliudanganya umma kuwa zao la mkonge haliwezi kuwakomboa kimaisha.
Wakiongozwa na Mwenyekiti wa Mashamba ya Mkonge ya Mwelya, Fredrick Malika, wananchi hao walisema katika heka moja wana uhakika wa kupata sh 800,000.
Awali Zitto ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), aliwaahidi wastaafu wa kiwanda cha mbao cha Mkata Saw Mils kufuatilia malipo yao ambayo hawajalipwa tangu walipostaafishwa.
Akizungumza katika mkutano ya hadhara mjini Mkata akiwa katika ziara ya siku tano mkoani Tanga, Zitto alisema atafuatilia serikalini kujua kama mwekezaji alifuata masharti ya kununua kiwanda hicho na kama uuzwaji uliangalia maslahi ya wafanyakazi.
Nimeitoa:http://freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=33182
Wamesema serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) chini ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete inalizamisha taifa kutokana na hali iliyopo sasa na kusema kuwa endapo haitafanya juhudi za dharura, hali inatakuwa mbaya zaidi.
Akizungumza kwa nyakati tofauti jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mji wa Mombo, mbunge wa Ubungo, John Mnyika, alimtaka Rais Kikwete na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, kutoa kauli ya haraka juu ya mpango wa dharura wa kunusuru uchumi na kutatua tatizo la mfumko wa bei nchini.
Mnyika ambaye pia ni Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, alisema katika miaka zaidi ya sita ya utawala wa Rais Jakaya Kikwete ahadi ya maisha bora kwa kila Mtanzania imekuwa ni ndoto ya kufikirika.
Alisema wananchi walioichagua CCM kwa kurubuniwa na mbinu chafu, kama kuhongwa vyakula, fulana, kofia, sasa wanavuna matunda ya chaguo lao na kuwataka kutumia muda huu kutafakari upya.
"Tumekuja Tanga mwaka huu, ikiwa ni moja ya nafasi ya kutekeleza tamko la Katibu Mkuu, Dk. Slaa, kuwa moja ya kipaumbele chetu mwaka huu ni kunusuru uchumi wa nchi na kukabiliana na gharama za maisha. Tunaitaka serikali kushughulikia vipaumbele ambavyo tumewaonyesha, kuongeza uzalishaji na kutengeneza ajira, ikiwa ni sehemu ya kudhibiti mfumko wa bei," alisema Mnyika.
Aliongeza kuwa kutokana na tamko hilo, wabunge wa CHADEMA kila mmoja kwa nafasi yake, anasimamia hoja hizo za kuongeza uzalishaji na kutengeneza ajira, hali iliyomfanya Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe, kuwasilisha hoja binafsi ya Mkonge, ambayo inalenga kuongeza uzalishaji na kutengeneza ajira katika kilimo.
Alisema licha ya Zitto kuipeleka hoja hiyo kwa maslahi ya wakazi na wakulima wa Tanga, wabunge wa CCM wa mkoa huo waliipinga kwa kile walichoona Watanzania wakiondokana na umaskini nafasi yao ya kuwarubuni itakuwa mashakani.
Akizungumzia viwanda, Mnyika alisema CCM badala ya kufanya ubinafsishaji wamefanya ubinafsi wa viwanda na kutolea mfano Kiwanda cha Tembo Chipboard, ambacho kilikuwa kikipata malighafi kutoka msitu wa Shume, lakini kutokana na sera mbovu na mipango mibovu, uzalishaji umedumaa na kiwanda kimefungwa.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto, alisema kuwa hali ya maisha ni ngumu na inatishia uhai na usalama wa nchi kwa kuwa katika njaa maradhi na umaskini uliokithiri ustaarabu unakosa nafasi.
Aliongeza baada ya Bunge kuikataa hoja binafsi kuhusu zao la mkonge, ni wajibu wa wananchi hao kuwakataa viongozi wasiowatetea kwa vitendo na hata katika masanduku ya kura pindi watakapojitokeza kuomba nafasi za kuwaongoza.
Awali wananchi wa mji wa Mombo walizuia msafara wa Zitto na kuutaka ufike katika mashamba yao wakashuhudie kile ambacho wabunge wa mkoa wa Tanga waliudanganya umma kuwa zao la mkonge haliwezi kuwakomboa kimaisha.
Wakiongozwa na Mwenyekiti wa Mashamba ya Mkonge ya Mwelya, Fredrick Malika, wananchi hao walisema katika heka moja wana uhakika wa kupata sh 800,000.
Awali Zitto ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), aliwaahidi wastaafu wa kiwanda cha mbao cha Mkata Saw Mils kufuatilia malipo yao ambayo hawajalipwa tangu walipostaafishwa.
Akizungumza katika mkutano ya hadhara mjini Mkata akiwa katika ziara ya siku tano mkoani Tanga, Zitto alisema atafuatilia serikalini kujua kama mwekezaji alifuata masharti ya kununua kiwanda hicho na kama uuzwaji uliangalia maslahi ya wafanyakazi.
Nimeitoa:http://freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=33182