Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,559
- 3,953
Kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa X (zamani Twitter), Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika amesema hatakuwepo katika kusaini maadaili Uchaguzi ya 2025 na hajateua Afisa au Kiongozi yeyote kwenda kushiriki kwa niamba yake
Ameandika “Katibu Mkuu CHADEMA sitakuwepo kwenye kikao cha tarehe 12 Aprili 2025 cha kushauriana na kusaini maadili ya uchaguzi ya 2025.
Ifahamike kuwa mwenye mamlaka ya kusaini maadili ya uchaguzi kwa niaba ya chama cha siasa ni Katibu Mkuu.
Katibu Mkuu sijateua kiongozi au afisa yoyote kwenda kushiriki kwa niaba yangu katika kikao hicho kitakachofanyika katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mkoani Dodoma.”
Baada ya andiko hilo la Mnyika, pamoja na Heche kwenda kutilia mkazo, CHADEMA imetoa neno kama chama kukubalina na kilichosemwa na Mnyika kama kiongozi anayehusika kuwakilisha chama kwenye jambo hilo.
Pia soma: Pre GE2025 - Vyama vya Siasa vyenye nia ya kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kusaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi, Aprili 12, 2025
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, vyama vya siasa na Serikali wanatarajiwa kusaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi yatakayotumika kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, ambapo chama cha siasa ambacho hakitasaini maadili hayo hakitaruhusiwa kushiriki kwenye uchaguzi huo.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Kailima Ramadhani amesema “Maadili hayo yameandaliwa kwa mujibu wa kifungu cha 162 (1), (2) na (3) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024. Kinaitaka Tume baada ya kushauriana na vyama vyote vya siasa na Serikali, kuandaa na kuchapisha katika Gazeti la Serikali Kanuni za Maadili ya Uchaguzi zitakazoainisha maadili ya vyama vya siasa, Serikali na Tume wakati wa kampeni za uchaguzi na uchaguzi na utaratibu wa utekelezaji wake.”
Hata hivyo, amesema kifungu hicho kinaelekeza kuwa kanuni za maadili zitasainiwa na kila chama cha siasa, kila mgombea kabla hajawasilisha fomu ya uteuzi, Serikali na Tume na zitapaswa kuzingatiwa na wahusika wote waliosaini.
Ameandika “Katibu Mkuu CHADEMA sitakuwepo kwenye kikao cha tarehe 12 Aprili 2025 cha kushauriana na kusaini maadili ya uchaguzi ya 2025.
Ifahamike kuwa mwenye mamlaka ya kusaini maadili ya uchaguzi kwa niaba ya chama cha siasa ni Katibu Mkuu.
Katibu Mkuu sijateua kiongozi au afisa yoyote kwenda kushiriki kwa niaba yangu katika kikao hicho kitakachofanyika katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mkoani Dodoma.”
Baada ya andiko hilo la Mnyika, pamoja na Heche kwenda kutilia mkazo, CHADEMA imetoa neno kama chama kukubalina na kilichosemwa na Mnyika kama kiongozi anayehusika kuwakilisha chama kwenye jambo hilo.
Pia soma: Pre GE2025 - Vyama vya Siasa vyenye nia ya kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kusaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi, Aprili 12, 2025
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, vyama vya siasa na Serikali wanatarajiwa kusaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi yatakayotumika kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, ambapo chama cha siasa ambacho hakitasaini maadili hayo hakitaruhusiwa kushiriki kwenye uchaguzi huo.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Kailima Ramadhani amesema “Maadili hayo yameandaliwa kwa mujibu wa kifungu cha 162 (1), (2) na (3) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024. Kinaitaka Tume baada ya kushauriana na vyama vyote vya siasa na Serikali, kuandaa na kuchapisha katika Gazeti la Serikali Kanuni za Maadili ya Uchaguzi zitakazoainisha maadili ya vyama vya siasa, Serikali na Tume wakati wa kampeni za uchaguzi na uchaguzi na utaratibu wa utekelezaji wake.”
Hata hivyo, amesema kifungu hicho kinaelekeza kuwa kanuni za maadili zitasainiwa na kila chama cha siasa, kila mgombea kabla hajawasilisha fomu ya uteuzi, Serikali na Tume na zitapaswa kuzingatiwa na wahusika wote waliosaini.