Precise Pangolin
JF-Expert Member
- Jan 4, 2012
- 12,998
- 6,659
Tuheshimu maamuzi yoyote ya mahakama tuheshimu uhuru wa mahakama.
Mnyika akishindwa hatuta heshimu
Tuheshimu maamuzi yoyote ya mahakama tuheshimu uhuru wa mahakama.
Hivi kama Mnyika akishindwa nani atakuwa amemtoa kwenye ubunge?Kumtoa Mnyika Ubungo kwa hila ni kumkaribisha Dr.Slaa a.k.a dokta wa ukweli kumwaga sumu Ubungo. Magamba watapoteza zaidi ya kuvuna katika hili. Kwanza tutashuhudia vita ya nani agombee kwa tiketi ya gambaz halafu baadaye tutaona CDM itarudi mjengoni.
Mliopo korti rum, twambieni nini chaendelea
Hali ya mambo ni nzuri watu hawana munkari kama ilivyotarajiwa hasa wale wa Chadema ndio wengi na wanaonyesha wana matumaini ya Ushindi,
Hukumui haijaanza kusomwa tunaelezwa itaanza mida ya saa 3 hivi,
Polisi kwa mida hii sio wengi sana kwa hesabu hawafiki 50. Kwa ujumla hali ni ya amani kabisa!
Tutawajuza hatua kwa hatua moja kwa moja toka ukumbini!
Updates:
- Basi aina ya coaster lililobeba mashabiki wa chadema ndio linaingia huku likishangiliwa na watu kwa alama ya vidole viwili alimaarufu Amani na Upendo!
- Naaaaam vijana wakazi (FFU) ndio wanaingia kwenye eneo la tukio wakiwa wamevalia kikazi yani kama Baghdad lakini wapo kwa usalama tu hakuna dalili ya vurugu yoyote hali ni yaamani tu!
- Kuna mabishano ya hapa na pale kati ya wananchi na wahudumu wa mahakama, watu wanalalamika kuwa mbona mda unakwenda na hawaruhusiwi kuingia mahakamani! Lakini wamefanikiwa kuwasihii na wananchi wametuliza munkali
- Tunaendelea kusubiri mda ufike tuanze kufuatilia kesi hii!
- Naaaaam tumeshaingia ukumbini tayari kuanza usikilizaji wa kesi hii uendelee! Tumeambiwa tuzime simu lakini MIMI sitazima mwanzo mwisho!
- Tunasubiri jaji aingie na jopo la mawakili wa pande zote wapo tayari!
UPDATES:
Kuna kichekesho kimejitokeza hapa, yani wakati wakuingia ukumbini kuna mbinu iliyotumika na mashabiki wa CDM kuwabana mlangoni wale wa Magamba na wakashindwa kupata siti kilichofuata ni afande kuwatoa nje, wakati wakitolewa nje kuna kuna mwanachadema mashuhuri akaingia ukumbini afande akataka kumuunganisha na wanachadema kutoka nje, unaambiwa ukumbi umelipuka na kusema huyo siti ipoo!
Naaaaaaaaaaam Mh Mnyika ndio anaingia ukumbini anashangiliwa kwa makofi na Pipooooooozi Pawaaaaaaaaaaaaaa!
Updates:
Wakili wa Mnyika ndugu Mbogolo ndio anaingia anasalimiana na mnyika waapiga picha wanaendelea kupiga picha!
Sasa kilichobaki ni kumsubiri jaji tu aingie ukumbini!
Updates:
Jambo la kufurahisha ktk kesi hii nikuwa Mh Mnyika na Hawa Ng'umbi wamekaa pamoja na wanapiga stori kweli, hata alipotokea afisa usalama akataka kuwatenganisha mnyika amemwambia haina tatizo watu pipoooooooooooz!
UPDATES:
M/Kiti wa CHADEMA na Kiongozi wa Upinzani Bungeni Mh Freeman Mbowe aka Sauti ya Zege ndio anaingia anashangiliwa ile mbaya pipooooooozi
UPDATES: Mpaka dakika hii saa nne kamili bado Jaji haja ingia ukumbini, tunaendelea kumsubiri!
UPDATES:
Naaaam jaji ameingia na hukumu inaanza rasmi,
Jaji anaomba radhi kuwa ataisoma hukumu kwa lugha ya kitumwa! Twendeleeee!
Updates:
Jaji anaendelea na mapitio ya mwenendo wa kesi nzima tangu ilipoanza na mpaka ilipo, kimsingi ameanzia kwenye historia ya kampeni,uchaguzi, uhesabuji kura na utangazwaji wa mshindi, sasa anaingia kwenye malalamiko makuu ya mlalamikaji,
Vuteni subira naripoti kwa kificho maana tumeambiwa tuzime simu na kamera zote za wanahabari!
Kwani sheria alisoma Kiswahili chuoni?
Mkuu hukumu inasomwa kwa kizungu hivyo jamaa inabidi atafasiri kwenda kiswahili huku akiwa mafichoni hapo mahakamani. Tumpe nafasi hawezi kuwa kasi kama vile ingekuwa inasomwa kiswahili na yeye hakujificha.Mbona maendeleo ya updates yamepotea? kazi zimesimama tunasubiri akili na mawazo yetu yako huko kwa sasa mkuu.
Hivi kama Mnyika akishindwa nani atakuwa amemtoa kwenye ubunge?
Samahani wadau nilipost hapa nikimjibu Ritz kuheshimu maamuzi ya mahakama, nikadokeza kuwa kesi ya Mhe Lema inaanza kusikilizwa 1st June 2012 lakini kwa ukweli hizo sio habari za kweli!!! Nilisikiliza habairi hizi kwenye radio moja sikumbuki ni ipi hapa Arusha ikitaja hizo tarehe, nikapost bila kuchunguza!! Naomba samahani kwa usumbufu uliowapata wadau waliosoma habari hizi, kiukweli ni kwamba tarehe maalum ya kusikiliza hiyo kesi haija pangwa. Nawaomba radhi hasa Ritz!!!Tuheshimu maamuzi yoyote ya mahakama tuheshimu uhuru wa mahakama.
Tujuzeni jamani mnao kielewa hicho kinyumbani basi? Au ndo wote mmezima simu?