Mnunuzi wa Nyumba au Kiwanja jihadhari, Serikali za Mitaa hawaruhusiwi kusimamia mikataba kisheria

Pia mkuu naona kama umeonesha kwamba kuihusisha serikali za mitaa ni hiari kama unapoamua kumuhusisha Jirani ama rafiki. Lakini huoni serikali ya mitaa ina uzito zaidi ya hao uliowataja?
 
Mie mikataba yangu yote ni hawa watendaji na wenyeviti. Mashahidi ni ndugu zake muuzaji. Nna amani to the maximum maana mawakili hawapo huku vijijini ninakopiga hizi Dili zangu
 
Mkuu naomba ufafanuzi:

1. Kama tayari namkataba wa mwenyekiti. Je, naweza peleka kwa wakili akausatify? Au unashauri nini hapo?
2. Mitaani kuna watu wanaitwa Waandishi wa Umma na sio Mawakili.

Mbona wana leseni za hiyo kazi wakati sio Mawakili Proffessional?
Kwanini serikali inachukua mapato kwa kazi isiyo rasmi?

Naomba elimu kwa hayo mkuu
 
Kuna mambo nitafafanua hapa na kuhoji pia hapa hapa.

1/Suala la Uwepo wa wakili katika mauziano hayo kwanini liwe kwenye Viwanja na Nyumba tu, lakini haujalizungumzia katika mauziano ya vitu vingine pia kama Gari, Simu, Jokofu, Vyakula nk ?

2/Sehemu nyingine watu wanauziana viwanja kwa utaratibu huo wa wenyeviti wa Mitaa na vijiji na mapatano yanapelekwa kusainiwa na kuhalalishwa mahakamani mbele ya Hakimu. Hili kisheria limekaaje? Ni halali ?

3/Katika mazingira ya nchi yetu ambayo zaidi ya 90% ya nyumba na viwanja vinavyouzwa havina hati na vinauzwa kienyeji sana, suala la uwepo wa wenyeviti wa mitaa au vijiji katika mauziano hayo haliwezi kuepukika moja kwa moja ili kumlinda kijamii muuzaji na mnunuzi kupata haki yake stahili mara kunapozuka mzozo.

4/Sheria na Haki ni vitu viwili tofauti hata kama vinashahabiana sana. Kufanya manunuzi ya nyumba au kiwanja kwa misingi ya kisheria ni jambo muhimu sana lakini haliwezi kutoa moja moja Haki ya kijamii kuweza kuimiliki au kuitumia hiyo ardhi ikiwa msingi wa kijamii haukujengwa tangu mwanzo, na hapo ndipo hao wenyeviti ws mitaa(Wenyeji wenye mamlaka!) wanapopata upenyo wa kuhusika katika mauziano hayo.
 
Aisee, umenifumbua akili, ubarikiwe
Huyo ni mchumia tumbo.Amekuvuta umevutika.Mwambie akuandikie na barua ya dhamana utoke mahabusu au gerezani.Look here,Afisa Mtendaji ni Mlinzi wa amani. Anaweza kisimamia hayo mambo. Huyo yupo kibiashara zaidi. Kalagabaho!
 
Huyo ni mchumia tumbo.Amekuvuta umevutika.Mwambie akuandikie na barua ya dhamana utoke mahabusu au gerezani.Look here,Afisa Mtendaji ni Mlinzi wa amani. Anaweza kisimamia hayo mambo.Huyo yupo kibiashara zaidi.Kalagabaho!

We nawe maisha yamekupiga. Kwaiyo ktk alichoandika huyo bwana hakuna cha msingi ambacho umekiona?
 
Ingawa kunaweza kuwa na ukweli kwenye bandiko lako lakini mimi napata uwalakini huenda mnajitafutia soko tu nyie wsnasheria maana kwa muda mrefu na niseme wengi wetu tumekuwa tukiuziana hasa viwanja kwa kupitia serikali za mitaa pasi na shaka na zaidi ya yote wale ndio wanaofahamu eneo husika na mmiliki wake kuliko kuja tu na wakili asiyejua ABC ya eneo husika.

Ndio maana serikali pia inawapa uwezo serikali mfano ya kijiji kutoa Maeneo kwa muwekezaji kwa kiwango fulani kwa kuitambua utendaji kazi wake.

Ushauri wako labda ungekuwa baada ya watu kuuziana kwa mtindo huo pendwa basi nyaraka zipelekwe kwa hao mawakili kwa ajili ya maboresho.
 
Upo sahihi kabisa Mkuu Mimi huwa nawaita na kunieleza historia ya eneo kama lina mgogoro na mipaka ni sahihi basi nawapa hiyo pesa kidogo na si asilimia 10 namwita mwanasheria mambo yanaisha ingawaje hao viongozi wa serikali za mitaa huwa hawapendi na kutishia kuwa ntapata matatizo wakati Mimi najua nachokifanya.
 
Ingawa kunaweza kuwa na ukweli kwenye bandiko lako lakini mimi napata uwalakini huenda mnajitafutia soko tu nyie wsnasheria maana kwa muda mrefu na niseme wengi wetu tumekuwa tukiuziana hasa viwanja kwa kupitia serikali za mitaa pasi na shaka na zaidi ya yote wale ndio wanaofahamu eneo husika na mmiliki wake kuliko kuja tu na wakili asiyejua ABC ya eneo husika

Ndio maana serikali pia inawapa uwezo serikali mfano ya kijiji kutoa Maeneo kwa muwekezaji kwa kiwango fulani kwa kuitambua utendaji kazi wake

Ushauri wako labda ungekuwa baada ya watu kuuziana kwa mtindo huo pendwa basi nyaraka zipelekwe kwa hao mawakili kwa ajili ya maboresho
Umeandika kwa uelewa mkubwa sana.Atakayesoma maoni yako atamaizi ukweli.Tena ukweli mtupu.Mtu ambaye hafahamu uhalali wala historia ya sehemu eti ndiyo asimamie mauziano.Haiwezekani!Kila mtu acheze karibu na sufuria lake la ubwabwa.
 
Nyongeza nyingine kuna watu wanakopeshana kwa riba na wanaandikishana kwa mwenyekiti. Hapo pia hakuna mkataba
Kuna kesi ipo inasema bank au taasiu ya fedha yenye leseni kutoka bank kuu ndo wanaweza kukopesha kwa riba.
 
Basi wengi wameliwa na ikija msako wa pekua pekua ya mikataba yakihalali basi wengi watakuwa hawana nyumba kihalali

Maana imekuwa mazoea kufanya mikataba hii ya kuuziana viwanja , mashamba kwenye serekali za mitaa hadi sasa imekuwa kama ndio sheria .

Lakini nauliza mbona hao wanasheria wenyewe hawakulizungumzia hili mapema ,

Maana kwa hali ilipofikia sasa ni mbali sana kwani kila mtu anajua mikataba inafanyika serekali za mitaa tu kama njia ya kwanza kuuziana na kununua,

Sasa mfano mtu ndio unataka kununua kiwanja au nyumba alafu uje na hii article mitaani humo nadhani kwanza watakushangaa sana
 
Basi wengi wameliwa na ikija msako wa pekua pekua ya mikataba yakihalali basi wengi watakuwa hawana nyumba kihalali

Maana imekuwa mazoea kufanya mikataba hii ya kuuziana viwanja , mashamba kwenye serekali za mitaa hadi sasa imekuwa kama ndio sheria .

Lakini nauliza mbona hao wanasheria wenyewe hawakulizungumzia hili mapema ,

Maana kwa hali ilipofikia sasa ni mbali sana kwani kila mtu anajua mikataba inafanyika serekali za mitaa tu kama njia ya kwanza kuuziana na kununua,

Sasa mfano mtu ndio unataka kununua kiwanja au nyumba alafu uje na hii article mitaani humo nadhani kwanza watakushangaa sana
Ukweli ni kwamba tuna siasa sana kwenye maamuzi yetu. Alichosema wakili ni kitu cha kuwa makini sana. Hatujui kesho yetu ni bora kuwa upande sahihi.
 
Ukweli ni kwamba tuna siasa sana kwenye maamuzi yetu. Alichosema wakili ni kitu cha kuwa makini sana. Hatujui kesho yetu ni bora kuwa upande sahihi.
Uko sawa. Nilimuuliza sasa kwa wenyemikataba ya wenyeviti wanaweza kupeleka kwa mawakili ilikuisatify akachuna mpaka leo.....
 
Na je kuifahamisha serekali za mitaa kuhusu kuuziana nilazima?
Katikati hapo ameandika serikali ya mtaa husaidia kumtambua muuzaji na pia kama kiwanja kina mgogoro au laah. Kwahiyo ni muhimu na hela yeyote itolewayo lazima ipate risiti halali vinginevyo ni takrima au rushwa.
 
Back
Top Bottom