Mnajua kwanini Lowassa anapendwa?

Mnajua kwanini Lowassa anapendwa?

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2008
Posts
55,028
Reaction score
59,657
''Kuhusu suala la umeme, Lowassa alisema Mbunge wa Nyamagana, Ezekia Wenje ni kijana anayefanya uamuzi mgumu kama yeye hivyo alimtaka leo kwenda kwa Meneja wa Tanesco Mwanza ili kujua tatizo, asipopewa majibu ya kuridhisha ampigie simu yeye (Lowassa).''

Maneno haya aliyasema Lowassa akiwa Mwanza, sasa imagine mtu kama huyu ndiye rais wa nchi kuna kulala makazini kweli? Itakuwa ni mchakachaka kila mtu lazima apige kazi kulingana na majukumu yake.
 
Hiyo ndiyo channelling katika majukumu...kitu ambacho Magufuli hana.

I know Magufuli inside out but nachelea kuandika baadhi ya vitu coz vinaweza kunifanya watu wake wa karibu wanijue.
 
Hata hapa Arusha aliagiza hivo hivo, lakini bado Mh Lema haja chukua hatua.
 
Hiyo ndiyo channelling katika majukumu...kitu ambacho Magufuli hana.

I know Magufuli inside out but nachelea kuandika baadhi ya vitu coz vinaweza kunifanya watu wake wa karibu wanijue.

ID yako tu tuneshakujua.....
 
Katika vitu nilivyocheza kama pele ni hii ID ndugu...itawapoteza wengi sana.

Ndio maana ukajiita Gwamahala I,e wa akili kwa kinyakyusa ila wewe kiuhalisia ni mndengereko.....thats good chief...mwaga ugali wa Magufuli basi mkuu.
 
Hata hapa Arusha aliagiza hivo hivo, lakini bado Mh Lema haja chukua hatua.

Ishu sio Lema mkuu,yawezekana Lema alishawaendea jamaa lkn wao wakaleta dharau sababu wanajua ni Order kutoka Upinzani lkn ingekuwa ni Chama Tawala hata km angeagiza mtu mdogo wangetekeleza.
 
Ndio maana ukajiita Gwamahala I,e wa akili kwa kinyakyusa ila wewe kiuhalisia ni mndengereko.....thats good chief...mwaga ugali wa Magufuli basi mkuu.

JF ni stress release tosha...
 
Saa yaja nayo ipo kila mtumishi wa gov atashusha mkia miguuni, acha watuchezee saana na umeme wao poor huduma lakin mwisho waja
 
Mtaongea mengi sana,mtakesha kwenye net huku mkikomalia kuandika jina la lowasa na kulipa sifa kedekede. Lakn itakapo fika oct 30 iakuwa ndo mwisho wa mijadala ya lowasa maana naamin atakuwa si mwanachama tena wa chadema wala ccm atakuwa ni mtu ambaye yupo kwenye msongo wa mawazo asiyejua hatma ya maisha yake.

Kama sio intensive care unit basi takuwa anaongea peke yake huku akitetemeka
 
Mtaongea mengi sana,mtakesha kwenye net huku mkikomalia kuandika jina la lowasa na kulipa sifa kedekede. Lakn itakapo fika oct 30 iakuwa ndo mwisho wa mijadala ya lowasa maana naamin atakuwa si mwanachama tena wa chadema wala ccm atakuwa ni mtu ambaye yupo kwenye msongo wa mawazo asiyejua hatma ya maisha yake.

Kama sio intensive care unit basi takuwa anaongea peke yake huku akitetemeka

Big up mkuu, fisadi hawezi kua kiongozi wa nchi hii, kwanza katudhiaki sisi maskini ambao tunatafuta pesa kwa jasho letu yeye mwizi wa mali za taifa anakuja na vimaneno na uchukia umasikini sasa tuibe kama yeye
 
YES!
Kwa sababu anachukia umaskini wetu na anapanga kuundoa
 
Big up mkuu, fisadi hawezi kua kiongozi wa nchi hii, kwanza katudhiaki sisi maskini ambao tunatafuta pesa kwa jasho letu yeye mwizi wa mali za taifa anakuja na vimaneno na uchukia umasikini sasa tuibe kama yeye

MISHAHARA YA MARAIS BARANI AFRIKA 2015
Wakati Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari akiupunguza mshahara wake muda mfupi baada ya kuingia madarakani mwaka huu, marais wengine wa Afrika wameonekana kujilimbikizia mishahara mikubwa, tofauti na pato ‘kiduchu' la wananchi wao kwa mwaka.
Kwa mujibu wa uchambuzi wa mtandao wa African Review, marais watano wanaoongoza kwa kuwa na mishahara mikubwa kwa mwaka ni Rais Paul Biya wa Cameroon anayelipwa Dola za Marekani 610,000, akifuatiwa na kiongozi wa Morocco, Mfalme Mohammed VI anayelipwa Dola 480,000 na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ni wa tatu akilipwa Dola 272,000.
Rais Jakaya Kikwete ni wa nne kwa malipo ya Dola 192,000 na wa tano ni Rais Abdel Aziz Bouteflika wa Algeria, anayelipwa Dola168,000.
Mtandao huo umebainisha pato la Mtanzania wa kawaida kwa mwaka kuwa ni Dola 1750 sawa na Sh3.5 milioni, linalozidiwa mara 114 na kiasi anacholipwa Rais kwa mwaka.
Madhumuni ya utafiti wa mtandao huo ilikuwa kuangalia kiasi wanacholipwa marais wa Afrika kwa mwaka na kile inachopata taifa husika kwa muda huo.
Pia walilenga kuangalia uhusiano wa viongozi hao na wananchi wa kawaida wanaowangoza.
Kwa mujibu wa mtandao huo, vyanzo vya taarifa za mishahara ya marais hao vilipatikana kutoka mitandao na wanahabari wa nchi husika.
Tofauti na maraisi wengine, Rais mpya wa Nigeria, Muhammadu Buhari, alitangaza punguzo la mshahara wa rais pamoja na wafanyakazi wengine wa Serikali mara alipoingia madarakani.
Rais mwingine aliyefanya hivyo ni Uhuru Kenyatta wa Kenya, ambaye pamoja na makamu wake walipunguza mishahara yao kwa asilimia 20 baada ya kuingia madarakani mwaka 2013.

Mwisho, hapa fisadi ni nani?
 
Mtaongea mengi sana,mtakesha kwenye net huku mkikomalia kuandika jina la lowasa na kulipa sifa kedekede. Lakn itakapo fika oct 30 iakuwa ndo mwisho wa mijadala ya lowasa maana naamin atakuwa si mwanachama tena wa chadema wala ccm atakuwa ni mtu ambaye yupo kwenye msongo wa mawazo asiyejua hatma ya maisha yake.

Kama sio intensive care unit basi takuwa anaongea peke yake huku akitetemeka

Na utabiri wako wa KICHAWI
 
Mnapoteza kumsafisha na kuiona ikulu akiwa mv kigamboni wakati john akitoa maagizo ya kuongoza nchi
 
Back
Top Bottom