fred tarimo
Member
- Oct 3, 2011
- 10
- 5
Mkurugenzi wa mabasi J4 expres bwana Juma Mahende ni nani? Kwanini akatishe maisha ya watu wawili kirahisi namna hiyo...
Chanzo: ITV
==========
Chanzo: ITV
==========
Waliouawa ni Ali Mohamedi na Claudia Sikarwanda. Star TV imeripoti kuwa mmiliki wa mabasi ya J4 Bw.Juma Mahende amewapiga wafanyabiashara wenzake wawili kwa risasi mbele ya ofisi yake na kufariki papohapo.Hatari hii imetokea Mwanza.
Jeshi la polisi limemkamata na kumtia ndani muuaji. Kamanda wa polisi wa Bw.Mkumbo amethibitisha kutokea kwa tukio hili. Ndugu wa marehemu wanasema jamaa waliouawa na muuaji walikuwa wanadaiana 25Milion. Inashangaza na kuhudhunisha kama haya yanaweza kutokea Tanzania.
Roho za wapenzi wetu (hata kama wana makosa) zinapotea kwa namna ya kikatili. Cha ajabu usishangae kukutana mitaani na muuaji akiwa huru.